Ushauri kwa CHADEMA

Kaniki1974

JF-Expert Member
Dec 2, 2008
352
22
Nawashauri CHADEMA kuhakikisha hawaibiwi kura huko Busanda kwani wizi wa kura ndio njia pekee iliyobaki kwa CCM sasa kupora ushindi Busanda. Hivyo CHADEMA please msifanye uzembe kabisa katika kulinda upigaji na kuhesabiwa kwa kura. Kumbukeni ushindi wa Busanda utapelekea ushindi Biharamulo. Chondechomde msibweteke.

Last time Mbeya vijijini mliboa kwa uzembe wa kipuuzi.

Wana JF wapenda mabadiliko tuwashauri hawa washinde Busanda. Mawazo yenu please.
 
Nawashauri CHADEMA kuhakikisha hawaibiwi kura huko Busanda kwani wizi wa kura ndio njia pekee iliyobaki kwa CCM sasa kupora ushindi Busanda. Hivyo CHADEMA please msifanye uzembe kabisa katika kulinda upigaji na kuhesabiwa kwa kura. Kumbukeni ushindi wa Busanda utapelekea ushindi Biharamulo. Chondechomde msibweteke.

Last time Mbeya vijijini mliboa kwa uzembe wa kipuuzi.

Wana JF wapenda mabadiliko tuwashauri hawa washinde Busanda. Mawazo yenu please.
pia wawe karibu na wananchi na kuwaelimisha zaidi, mfano kuweka tv kwenye stategic position na kutangaza sera zao hata kwa kutumia generator na kuonyesha ubaya wa uongozi wa ccm, wa uwaibia rasilima na kuwapa kiduchu ili kuwadanganya, pia kutokuwa nma maendeleo kutoka na uongozi mbovu wa ccm, ukija uchaguzi ndio wanajifanya kila kitu kiko katika mipango blah blah, njia nyingine ni kuwaelemisha watu kama sokoni na wanafunzi walio na umri wa kupiga kura, na hata waalimu ambao miaka nenda miaka rudi hawathaminiwi na ccm, ila wakati wa uchaguzi
 
pia wawe karibu na wananchi na kuwaelimisha zaidi, mfano kuweka tv kwenye stategic position na kutangaza sera zao hata kwa kutumia generator na kuonyesha ubaya wa uongozi wa ccm, wa uwaibia rasilima na kuwapa kiduchu ili kuwadanganya, pia kutokuwa nma maendeleo kutoka na uongozi mbovu wa ccm, ukija uchaguzi ndio wanajifanya kila kitu kiko katika mipango blah blah, njia nyingine ni kuwaelemisha watu kama sokoni na wanafunzi walio na umri wa kupiga kura, na hata waalimu ambao miaka nenda miaka rudi hawathaminiwi na ccm, ila wakati wa uchaguzi


sure, kama vile wahubiri injili tunavyofanya!
 
Ushauri mwingine: CCM wanapita wanatangaza kuwa wananchi wasikaribie helikopter ya CHADEMA kwani itawalipukia kama mabomu ya mbagala, sasa hapa ndipo pa kuwapatia CCM " JE CHADEMA WAKISEMA KUWA CCM WALILIPUA MABOMU MBAGALA MAKUSUDI ILI WAWATISHE WANANCHI WATAKUWA WAMEKOSEA?" Ikumbukwe kuwa watu walikufa kule Mbagala sasa hii ni busara kwa CCM kutumia tukio hilo lililotokea wakati wao wakiwa wanacontrol jeshi kuwatishia wananchi?

19th May 2009



headline_bullet.jpg
CCM yaonya italipuka kama Mbagala
headline_bullet.jpg
Yaasa wananchi kuhudhuria mikutano

headline_bullet.jpg
Nguzo za umeme zasambazwa jimboni

headline_bullet.jpg
Chama tawala sasa wabadili mbinu




CCM%20Busada.jpg

Mgombea wa kiti cha Ubunge jimbo la Busanga kupitia Chama cha Mapinduzi, Lolesia Bukwimba akiwainamia wanakijiji cha Nyachiluluma kilichopo wilaya ya Geita.

Busada1.jpg

Wananchi wakimsikiliza mgombea wa CHADEMA katika kampeni za kugombea kiti cha Ubunge wa jimbo la Busada.

remove.jpg

box_on.jpg

box_off.jpg

add.jpg




Habari zilizozagaa katika jimbo la Busanda kwamba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kitaanza kampeni zake wiki hii kwa kutumia helikopta, zimeongeza homa ya uchaguzi na wapinzani wao wamezua jambo kuhusu usafiri huo.
Chadema ambayo imekuwa na utaratibu wa kutumia helkopta katika kampeni zake, inadaiwa kwamba itatumia usafiri huo katika wiki hii ya lala salama kabla ya kupigwa kura Jumapili ijayo katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimboni humo.
Kutokana na taarifa za helikopta kusambaa Busanda, makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametahadharisha wananchi kuhudhuria mikutano yenye helkopta hiyo kwa madai kwamba litalipuka.
Gari la matanzo la CCM juzi na jana lilikuwa likiranda katika mitaa jimboni humo likiwaonywa wananchi kutokuhudhuria mikutano ya helikopta, kwani wanaweza kulipukiwa kama mabomu ya Mbagala.
Magari ya CCM yaliyofungwa spika yamekuwa yakitoa matangazo kwamba helikopta hiyo inaweza kulipuka kama mabomu ya Mbagala jijini Dar es Salaam ajali iliyotokea Aprili 29, 2009 na kuua watu 26 na kujeruhi kadhaa.
"Mkihudhuria mikutano ya Chopa (helikopta) linaweza kulipuka kama mabomu mnayoyasikia huko Mbagala," alitangaza mkereketwa mmoja katika gari ya matangazo.
Hata hivyo tofauti na vishawishi hivyo, wananchi wengi wanaonekana kuwa na shauku ya ujio wa Chopa.
Jana Chadema walitangaza kwamba helikopta wanatakayotumia itawasili leo jimboni humo kwa lengo la kumnadi mgombea wao, Finias Magesa.
Akitumia helkopta hiyo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, anatarajia kufanya mikutano mitano kwa siku.
Nguzo za umeme zasambazwa Busanda
Wakati hayo yakitokea watu waliojitambulisha kama wafanyakazi wa Tanesco, wamemwaga nguzo za umeme katika maeneo ya Bukondo na kuwaeleza watu kwamba kuna mpango wa kuwapelekea umeme.
Hatua hiyo imelalamikiwa na vyama vya upinzani jimboni hapa, kwa vile ina lengo la kuwaghilibu wananchi.
Mgombea wa ubunge kwa tiketi ya Chadema Mhandisi Finias Magesa, alisema watu hao sio wafanyakazi wa Tanesco, bali ni makada wa CCM.
Akihutubia wananchi wa Kata ya Lwamgasa Magesa alisema hatua hiyo ya CCM ni utapeli, kwa vile hakuna umeme unaoweza kufikishwa sehemu, bila kwanza eneo husika kupimwa.
"Sasa kama wanaleta umeme kwa nini nguzo zianze kumwagwa Bokondo, badala ya kuanzia kule Geita umeme unapotoka, huu ni utapeli wa CCM na wala sio Tanesco," alisema.
Katika hatua nyingine Tanzania Labour Party (TLP) kimetangaza kumuunga mkono mgombea wa CUF, Oscar Ndalahwa.
Uamuzi huo ulitangazwa mjini hapa na Katibu wa Chama hicho wilayani Geita Emanuel Silas.
"Sisi TLP tumeamua kukipigia debe chama cha CUF katika uchaguzi wa Busanda," alisema Katibu huyo.
Polisi: Hatujapokea malalamiko ya Chadema
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi nchini limesema halijapokea malalamiko kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) dhidi ya Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Geita, Shaban Kimea kwa madai ya kuisaidia CCM, katika kampeni zake za kuwania kiti cha ubunge jimbo la Busanda.
Msemaji wa Jeshi hilo, Juma Ally, alisema jana kuwa ofisi yake haijapokea malalamiko kutoka kwa mtu binafsi, taasisi au chama chochote kuhusu madai kwamba OCD Kimea amekuwa akikisaidia CCM katika kampeni zake.
"Inawezekana labda malalamiko yao wamepeleka kwa Tume ya Uchaguzi, lakini ofisi yetu haijapokea malalamiko dhidi ya OCD wa Geita," alisema na kuongeza:
"Malalamiko hayo yametolewa na nani na lini…ofisi yangu haijapokea malalamiko yoyote kuhusu OCD huyo. Unajua Jeshi la Polisi ni kubwa na lina utaratibu wake wa kupokea malalamiko, pengine inawezekana malalamiko hayo yamewasilishwa kwanza kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, lakini hapa ofisini kwangu hayajafika."
Wiki iliyopita, Chadema kilitoa malalamiko katika mikutano ya hadhara ya kampeni za uchaguzi mdogo wa kiti cha ubunge katika jimbo la Busanda, kikimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekata Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema, kumhamisha OCD wa Wilaya ya Geita kwa kile walichodai kuwa anakiuka taratibu za kampeni za uchaguzi kwa kukisaidia chama tawala kiweze kushinda katika uchaguzi huo mdogo.
Inadaiwa kuwa polisi wilayani humo wamekuwa wakiwatawanya wanachama wa Chadema pale wanapokusanyika katika ofisi zao kwa mikutano ya ndani na wakati mwingine kuwakamata wanachama wake kwa madai ya kuleta vurugu.
Vipigo vyaendelea kutolewa
Katika hatua nyingine vipigo vimeendelea kutawala mikutano ya hadhara ikiendeshwa na walinzi wa mikutano ya CCM.
Katika mkutano wa CCM uliofanyika jana saa 4:30 asubuhi kijiji cha Nyachiluluma wilayani humo kumnadi mgombea wake Lolesia Bukwimba, wafuasi wanaodhaniwa kuwa ni wa Chadema walipata kipigo kutoka kwa walinzi hao wa CCM.
Wakati mkutano huo ukiendelea, walipita vijana watatu wakiwa na pikipiki huku wakipeperusha bendela ya Chadema karibu na eneo hilo, lakini waliporejea walinzi hao wa CCM wanaojiita Green Guard, walimkamata mmoja wao na pikipiki yake na kuanza kumpiga kisha kumpeleka katika gari lao.
Wakati tukio hilo linatokea, hapakuwepo na askari yeyote kama wanavyoonekana katika mikutano inayofanyika mijini ambako mara zote Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wametanda wakiwa na silaha za moto na mabomu ya machozi.
Katika mkutano huo, Mbunge wa Same Mashariki na Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC), Anne Kilango Malecela, aliwaambia wananchi wa kijiji hicho kuwa wasisikilize maneno ya wapinzani kuwa CCM ni mafisadi.
Kilango alisema hakuna serikari yoyote duniani ambayo haina viongozi ambao siyo waadilifu: "Nakiri katika chama changu kuna mtu mmoja mmoja ambao wanafanya mambo ya ufisadi. Ila sisi wenyewe katika chama huwa tunasemana na ndio maana nipo hapa kumuunga mkono mwanamke mwenzangu muchagueni kwani yeye sio fisadi."
Naye Mbunge wa Ilemela na Mjumbe wa NEC, Anthony Dialo, aliwataka wanakijiji hao kutowachagua watu wanaotaka kura kwa kutoa chumvi na fedha.
Mgombea huyo, Bukwimba, akijinadi huku amechuchuma akiomba kura, alioambia wanachi hao wamchague ili aendeleze mambo mazuri aliyoacha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Faustine Rwilomba Kabuzi.
Alisema ataendeleza sekta ya elimu, kilimo na kwa wafanyabiashara ndogo ndogo kwa kuwatafutia mikopo ili kukuza biashara zao.
CCM wabadili mbinu
Katika hatua nyingine, CCM jana kiliahirisha mkutano wake uliopangwa ufanyike eneo la CCM Centre na sasa wanaendesha vikao vya ndani.
Wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu Bara, George Mkuchika, waliamua kufanya mkutano wa ndani, uliowajumuisha baadhi ya wazee na vijana wafanyabiashara.
Katika mkutano huo, habari zinasema kwamba Mjumbe wa kudumu wa Kamati kuu ya CCM, John Malecela, alishindwa kuwazoa wafanyabiashara 50 wa Soko la Katoro, ambao alikutana nao katika mkutano wa ndani.
Malecela alifika eneo hilo jioni akiwa na gari namba T 509 AFZ aina ya Toyota Land Cruiser, akiwa amefuatana na baadhi ya wapiga debe wa CCM.
Katika mkutano huo Malecela alisema ameamua kuwaita wafanyabiashara hao na kufanya nao mkutano wa ndani kwa lengo la kuwashawishi wakisaidie CCM.
Aliwaahidi wafanyabiashara hao wakichague CCM kwa vile kwa kutumia kofia yake ya chama tawala, itahakikisha inaboresha soko hilo na kuondoa kero zote zilizopo.
Hata hivyo mkutano huo wa ndani ulifichuka na kuwa kama wa hadhara baada ya wafanyabiashara hao kupiga makelele ya kusema wamechoka na CCM.
Mmoja wa vijana hao, Marando Malya, alimuuliza kama wao vigogo wamefikwa maji ya shingo, wakiingia vijana si watazama kabisa.
"Mheshimiwa sasa kama ninyi mpo maji ya shingo tukiingia sisi wadogo si tutazama kabisa?"alihoji Malya hali iliyozua ashangiliwe kwa nguvu.
Kutokana na ugumu huo, kikao hicho kiliahirishwa.

Imeandikwa na Simon Mhina, na Edwin Mjwahuzi (Busanda) na John Ngunge (Dar).




CHANZO: NIPASHE
 
Kama ni kweli kwamba wana CCM wanawashauri watu wa Busanda wasikusanyike mbele ya helikopta kwa sababu italipuka basi wamefilisika kisera zaidi ya nilivyokuwa nafikiria.
 
Kama ni kweli kwamba wana CCM wanawashauri watu wa Busanda wasikusanyike mbele ya helikopta kwa sababu italipuka basi wamefilisika kisera zaidi ya nilivyokuwa nafikiria.

Ndugu yangu umechelewa kulijua hili....
 
Ushauri mwingine: CCM wanapita wanatangaza kuwa wananchi wasikaribie helikopter ya CHADEMA kwani itawalipukia kama mabomu ya mbagala, sasa hapa ndipo pa kuwapatia CCM " JE CHADEMA WAKISEMA KUWA CCM WALILIPUA MABOMU MBAGALA MAKUSUDI ILI WAWATISHE WANANCHI WATAKUWA WAMEKOSEA?" Ikumbukwe kuwa watu walikufa kule Mbagala sasa hii ni busara kwa CCM kutumia tukio hilo lililotokea wakati wao wakiwa wanacontrol jeshi kuwatishia wananchi?


,,,Yote kwa yote,hawa wapinzani wangekua wanaumoja wao,hakika MNYAMA angeangukia PUA safari hii,manake hali ni mbaya kweli,kuanzia huko KATORO mpaka hukoo UNGUJA katika jimbo la MAGOGONI,tatizo wao ndo wanazigawa KURA hawa wapinzani.
 
,,,Yote kwa yote,hawa wapinzani wangekua wanaumoja wao,hakika MNYAMA angeangukia PUA safari hii,manake hali ni mbaya kweli,kuanzia huko KATORO mpaka hukoo UNGUJA katika jimbo la MAGOGONI,tatizo wao ndo wanazigawa KURA hawa wapinzani.
Asante kwa kuliona hili, huu ndio ungekuwa ushauri kwa chadema waachane na umaarufu wa chama, waangalie kukubalika kwa mgombea wao, kama yuko juu ya wa cuf, waishauri cuf ivunje kampeni, wajiunge na Chadema. Na kama ni mgombea wa CUF yuko juu, Chedema wavunje kambi. Yaani Busanda ni ushindi wa wazi wa wapinzani ila mgawanyo wa kura za Chadema na CUF, yaani kitendo cha Chadema na CUF kuvutana ili kupokonyana Busanda, kutapelekea jimbo hilo kuwaponyoka wote na kudondokea mikononi mwa CCM.
 
eee bwana haya ndiyo maneno ila sisi wote tujitahidini kufichua njama za uibaji kura tu ndio unaotuangusha maana, last time hapo arusha wasingepata hata mmoja si huyu wa mjini wala arumeru. kilichotumika ni masunduku yaliyojaa yametangulizwa kwa hiyo tukakosa. sijui tutafanyaje wtz jamani hee wanatuibia hata kura mbali na pesa.
 
Nawashauri CHADEMA kuhakikisha hawaibiwi kura huko Busanda kwani wizi wa kura ndio njia pekee iliyobaki kwa CCM sasa kupora ushindi Busanda. Hivyo CHADEMA please msifanye uzembe kabisa katika kulinda upigaji na kuhesabiwa kwa kura. Kumbukeni ushindi wa Busanda utapelekea ushindi Biharamulo. Chondechomde msibweteke.

Last time Mbeya vijijini mliboa kwa uzembe wa kipuuzi.

Wana JF wapenda mabadiliko tuwashauri hawa washinde Busanda. Mawazo yenu please.

Shida kubwa ya Mbeya Vijijini ni kwamba mgombea

aliyekuwa chaguo la wanaMbeya na wanaMageuzi, kijana

kipenzi wao, Sambwee Shitambala Gaya alitolewa katika

hatua za mwisho kabisa baada ya kudaiwa kujiapisha kwa

kutumia kampuni yake ya uwakili, badala ya kwenda

mahakamani.

Matokeo yake ni kwamba wananchi walisusa hata kwenda

vituoni kupiga kura.

Wazo ulilotoa bwana KANIKI WA 1974 ni la msingi sana.

Bila kufanya hivyo, MNYAMA ATASHINDA KWA KISHINDO!
 
Hivi hawa vibarua wetu wa TBC1 wanatutaka nini Watanzania? Mbona wanazidisha kuwabeza wazalendo wa Chadema katika nchi yetu kwa kujaribu kuwajengea picha mbaya kwa Watanzania? Haki ya nani siku yao itafika tu.
 
mimi hata kama angekuwa panya bora ashinde hicho kiti kuliko CCM!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom