Ushauri kwa CDF Jenerali Mkunda na Serikali kuhusu uendeshaji wa Shule za Jeshi

KaziIendelee

JF-Expert Member
Oct 30, 2013
327
229
Awali ya yote nampongeza sana Mhe. Rais wetu, mpendwa wetu Mama SAMIA SULUHU HASSANI kwa kazi nzuri anayoifanya na wasaidizi wake. Pia nampongeza sana aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya ulinzi mstaafu kwa kazi kubwa aliyoifanya na nampongeza sana Mkuu mpya mteule wa majeshi ya ulinzi kwa uteuzi wake.

Baada ya utangulizi wangu huo, naomba nijikite katika kushauri kwa Serikali, Mkuu mpya wa majeshi na wasaidizi wake kuhusu namna ipi bora ya uendeshaji wa shule za sekondari za majeshi.

1. Nashauri waalimu wote ambao sio askari wanaofanya kazi katika shule hizo waajiriwe na serikali ili kulipunguzia jeshi gharama za uendeshaji na ikifanyika hivyo hata ada zinaweza kushuka na ikawa msaada kwa watoto wengi wa kitanzania kupata taaluma na kulelewa kinidhamu kuwa wazalendo wa Taifa letu.

2. Non teaching staff kama wapishi waendelee kulipwa na jeshi kulingana na makubaliano yao.

3. Pia kuwepo na mchanganyiko katika nafasi za kiutawala kwa maana ya raia na askari ili kuleteta chemistry nzuri ya kiutendaji kuepuka uendeshaji wa taasisi ya kitaalumu kwa imla.

Huo ndiyo ushauri wangu.

Kazi Iendelee.
 
Yaani private school walimu mshahara walipwe na serikali km hvyo na wanafunzi wa serikali nao waje kusoma hapo Bure mwanafunzi anafaulu kwenda makongo au jkt
 
Yaani private school walimu mshahara walipwe na serikali km hvyo na wanafunzi wa serikali nao waje kusoma hapo Bure mwanafunzi anafaulu kwenda makongo au jkt

Sent from my TECNO KG5j using


Zile shule ni nusu serikali nusu private kwa uelewa wangu mdg hvyo si dhambi kufanya hvy ikawa sehemu ya mchango wa serikali km zile shule kwasbb naamini jeshi lina kazi kubwa sana ya kulinda nchi yetu
 
Inaonekana una dharau sana mtoa mada,yaani umekaa ukafikiria ukaona jeshi haliwezi kuwa na walimu wa kuwepo kwa taaluma inayotakiwa kwenye hizo shule ndyo maana unataka mchanganyiko?.

Halafu kuhusu hao walimu ambao ni non military servants hawahusiani kabisa na serikali kwasababu hizo shule mapato yake hayaendi serikalini,sasa iweje serikali iwalipe?
 
Inaonekana una dharau sana mtoa mada,yaani umekaa ukafikiria ukaona jeshi haliwezi kuwa na walimu wa kuwepo kwa taaluma inayotakiwa kwenye hizo shule ndyo maana unataka mchanganyiko?.

Halafu kuhusu hao walimu ambao ni non military servants hawahusiani kabisa na serikali kwasababu hizo shule mapato yake hayaendi serikalini,sasa iweje serikali iwalipe?
mapato hayaend serikalin? mhh kamba. kwa hyo haztoi kodi?
 
mapato hayaend serikalin? mhh kamba. kwa hyo haztoi kodi?
Kodi inayolipwa ni kiasi gani inayoweza kufanya serikali ikawalipa hao non military servants?

Au kama ni kigezo cha kulipa kodi basi na walimu wanofundisha private schools walipwe na serikali kwasababu pia hizo shule zinalipa kodi serikalini
 
Jeshi inahusiana vipi na serikali kiutendaji.
shule za jeshi zibaki za jeshi
shule za serikali zibaki za serikali
shule za ccm zibaki za ccm
shule za dini zibaki za dini
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom