Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Uhalifu wa EPA, ESCROW na wizi mwingine mwingi wenye kutia hasira kichwani wahusika ni hao hao wazalendo wanaojifanya wanaipenda sana Tanzania.
Magaidi wanatandikwa risasi dunia nzima hilo ni tatizo la kidunia haliwezi kutatuliwa na uraia pacha.
Hao wenye miji Tanzania na kwao wanaendeleza sehemu zote mbili. Kuna wachezaji wa Nigeria na mataifa mengine ya magharibi wanaziwakilisha vyema nchi za asili za Baba zao, wale wachezaji wa ndani peke yao wasiokuwa diaspora hawawezi kuunda timu za mataifa zenye ushindani mkubwa.
Tunalalamika kwamba ardhi yetu itachukuliwa na wageni, hivi sasa hatuna uraia pacha na bado kuna malaki ya heka ambayo ni mapori matupu hayajaendelezwa!!.

Hakuna shinikizo lolote kuhusu uraia pacha, ni asili ya binadamu kuwa sehemu ya nyumbani alipozaliwa kabla ya kuuishi ughaibuni kwa miaka mingi.

Ni muda wa kubadilisha hii mitazamo ya kijamaa inayotudanganya kwamba tutaibiwa na wageni kile kilicho chetu, hao wageni wenye damu za kitanzania wanaweza kuja na ufanisi mkubwa kuliko mazoea yetu ya miaka yote.

Kamanda, unaongea point....Ubarikiwe!
 
Umasikini wako unatokana na mtizamo wako.kwa taarifa yako wazungu wanakuja tanzania wanatajirika,wewe unalilia kwenda kwao ili utajirike.
Ndugu yangu umasikini ni fikira na si mahali ulipo.Hata ukipata huo uraia pacha ukaenda ukaendekeza ngono na ulevi bado utaendelea kulalamika
sema utabadilisha style ya kulalamika.

Uraia pacha ni muhimu mno kamanda....utakuja kuyaona matunda yake....kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.


Kamanda, hao sio wajinga waruhusu uraia pacha, wameona ina faida mno na ndio maana nchi zao zimeendelea....
 
Mkuu Kwanza nimekupa Like,

Pili Ukiona Mada za Uraia Pacha tafadhali usisahau Kuweka Comments mkuu!
Tena Ya -ve sana.
Bila Hivyo hawa watu watatushinda hawa...
Hoja zao ni Binafsi zinaangalia maslahi yao na Sio ya Taifa.
Tanzania Itaendelezwa na Watanzania Wazalendo!
Hata Ambae yupo Nje akitaka Kuendeleza afanye tuu si Kuna Ndugu zake huku?
Awasaidie kama anataka,Kwani Lazima awe na Uraia mara mbili(Pacha)
Anataka Kusaidia asaidie sababu Kuna Baba mkubwa ,Dada,Shangazi nk !
Hayo Mengine ni Ubinafsi.

Huu ni ubinafsi na roho mbaya....nchi zilizoruhusu uraia pacha sio wajinga, na ndio maana wanaendelea, wewe utabaki na kaubinafsi kako.....
 
Kuzuia uraia pacha ni roho mbaya na ushamba wa baadhi ya watu wetu hasa viongozi wanaoogopa wana diaspora kuja kuwanyang'anya nafasi zao tokana na kuwa na ujuzi na uzoefu zaidi. Bila hiyo, hakuna sababu ya msingi hata moja. Mbona magabacholi wanakuja na kuchezea mali zetu wakisaidiana na mafisadi wetu. Hivi akina Andrew Chenge, Edward Lowassa, Jakaya Kikwete, Nazir Karamagi, James Rugemalira, Dr Dau, Anna Mkapa, Daniel Yona, Peter Noni, na mafisadi wengine waliojazana nchini wana uraia wa nchi mbili? Acheni wivu wa kipiumbavu na uvivu wa kufikiri. Kama nchi tajiri kama Marekani, Canada na nyingine zinaruhusu wanuka umaskini wetu kuchukua uraia wao na kubaki na wetu sisi tuna nini zaidi ya pepo la fitina na roho mbaya?

Uchangiaji wko umekaa kisiasa sana , naeza pata maelezo ni magabacholi wa wap na lin wamekuja kula mema ya nchi yetu chini ya baraka za watunga sheria zetu ? ( Proof ; reference ) @ hatutaki story zavijiweni
 
Uchangiaji wko umekaa kisiasa sana , naeza pata maelezo ni magabacholi wa wap na lin wamekuja kula mema ya nchi yetu chini ya baraka za watunga sheria zetu ? ( Proof ; reference ) @ hatutaki story zavijiweni
Nenda kwenye mitaa ya Dar na miji mingi uone hawa wabaguzi wambao pamoja na kuletwa na wakoloni kutunyonya walikataa kuchanganyikana nasi. Hili halihitaji utafiti wala kujificha nyuma ya siasa. Magabacholi wapo wengi tu. Napenda sana kutumia jina la magabacholi hasa nikizingatia wanavyowabagua waswahili wenzetu waitwao Jarawa kwenye visiwa vya Andaman ambao wanawatumia kama wanyama kufanya utalii.
 
Uraia pacha ni muhimu mno kamanda....utakuja kuyaona matunda yake....kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.


Kamanda, hao sio wajinga waruhusu uraia pacha, wameona ina faida mno na ndio maana nchi zao zimeendelea....
Ikumbukwe kuendelea kwa mtu au taifa kuna factors nyingi sana zinazohusika.
Kuna nchi nyingi duniani zimeendelea sana kwa kutumia raslimali zilizopo nchini mwao,vipi hapa kwetu,raslimali zimetutoa?
au napo tunakwamishwa na kutokuwa na uraia pacha?
Mimi naona kwanza tuwekeze kwenye kuwa na mioyo ya kizalendo tukifanikiwa ndo tuingie huko kwenye upacha.
 
Huyu Malamula ameanza kuni-disappoint sana. Ilikuwaje akapewa hii nafasi?
Wewe ni wale wenye roho ya korosho ambao walishindwa kwenda majuu na kuwaonea wivu wenzao kiasi cha kuwawekea pini kwa sababu tu ya roho mbaya na ujinga au?
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametoa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha!

Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balozi Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana. Na karibu wote wanaobisha au kupinga uraia pacha hawajui maana ya uraia pacha na taratibu za mtu kuwa raia pacha. Si watu wa kusikilizwa katika msingi huu, waelimishwe kwanza, kutia ndani na wabunge.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​




Tanzania iko tofauti na hizo nchi na mifano yote hiyo.Tatizo nchi yako hauijui ndio maana unalalamika


Haitakuja kutoka in your lifetime na Mulamula hauwezi

Unazungumza 85% wasiotaja vs 0.2% wanaotaka...usiulize najuaje


Kuna mengi ya kufanyia kazi kuanzia umaskini na sio uraia pacha

usipoteze muda humu, it will nevee happen TZ
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametoa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha!

Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balozi Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana. Na karibu wote wanaobisha au kupinga uraia pacha hawajui maana ya uraia pacha na taratibu za mtu kuwa raia pacha. Si watu wa kusikilizwa katika msingi huu, waelimishwe kwanza, kutia ndani na wabunge.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​

Mheshimiwa Malamula sijui kama ni Raia Pacha, namsihi aanze taratibu.

URAIA PACHA SI WA KUCHAGUA, NI WA KURUHUSIWA NA NCHI YA PILI KWA MASHARTI YAO. Kabla hujapewa uraia pacha wa USA, ni lazima ule kiapo kifuatacho, hadharani:

Full Oath of Allegiance to the United States

“I hereby declare, on oath, that I absolutely and entirely renounce and abjure all allegiance and fidelity to any foreign prince, potentate, state, or sovereignty, of whom or which I have heretofore been a subject or citizen; that I will support and defend the Constitution and laws of the United States of America against all enemies, foreign and domestic; that I will bear true faith and allegiance to the same; that I will bear arms on behalf of the United States when required by the law; that I will perform noncombatant service in the Armed Forces of the United States when required by the law; that I will perform work of national importance under civilian direction when required by the law; and that I take this obligation freely, without any mental reservation or purpose of evasion; so help me God.”

Hii ni ya USA, kuna ya Israel, Ujerumani, India, nk. Kwa ufupi, hakuna nchi inayokupa Uraia wake kama wewe ni Raia wa nchi ingine. Tumepewa mifano ya South Africa (apartheid), Kenya (Mungiki, maumau), Rwanda (Genocide), Ethiopia (Dergue), hizi si nchi za kulinganusha nazo.

Tumeambiwa mashoga na mafisadi na majambazi na malaya eti tunao wengi si raia pacha. Hawa wapo kila mahali, mambo yao hayahusiki.

Mheshimiwa Balizi: hiyo ramani ya AFRICA ni ya nchi ZINAZOOMBA uraia pacha: naomba nipe ramani ya nchi ZINAZOOMBWA na KURUHUSU uraia pacha, nchi za EU, USA, JAPAN, INDIA, ISRAEL, AUSTRALIA, RUSSUA, CHINA.
 
Mheshimiwa Balizi: hiyo ramani ya AFRICA ni ya nchi ZINAZOOMBA uraia pacha: naomba nipe ramani ya nchi ZINAZOOMBWA na KURUHUSU uraia pacha, nchi za EU, USA, JAPAN, INDIA, ISRAEL, AUSTRALIA, RUSSUA, CHINA.
Unaelewa urataibu wa uraia pacha kweli? Nchi zinaomba uraia pacha kwa nani? Na nchi zinaombwa uraia pacha na nani?

Siku zote nimesema, wengi wanaobisha juu ya suala la uraia pacha hawajui hata utaratibu wa uraia pacha ukoje.

Kwani nani amesema ncho zote zinazoruhusu uraia pacha zinashurutishwa na kiapo cha uraia cha Marekani? Na sisi Tanzania tukiweka kiapo kama cha Marekani, so what? Acha Wamarekani wao ndio wawakatalie Watanzania kuoma uraia wa Marekani kwa ajili ya sisi kuwa na kiapo kama chao. Hakuna sheria Marekani inasema huwezi kuomba uraia wa Marekani kwa kuwa kiapo cha nchi yako kiko sawa na cha Marekani
 
Unazungumza 85% wasiotaja vs 0.2% wanaotaka...usiulize najuaje
Inawezekana hao 85% wasiotaka ni vihiyo kama wewe, ndio maana tulikubali mfumo wa vyama vingi japokuwa 80% walipinga. Tukipoiga kura ya kukubali au kukataa chanjo ya Korona, inawezekana wajinga wakawa wengi zaidi upande fulani. usiokubalika na werevu. Tunaijua nchi yetu, ina tatizo la ujinga, umasikini na maradhi, sasa lazima tukumbuke kuwa wajinga nao huwa wana uhuru wa kutoa maoni yao ya kijinga, lakini sio lazima tuwasikilize.
 
Wewe ni wale wenye roho ya korosho ambao walishindwa kwenda majuu na kuwaonea wivu wenzao kiasi cha kuwawekea pini kwa sababu tu ya roho mbaya na ujinga au?
I say, hadi leo kuna watu wanaabudu kwenda majuu!!! Pole sana Mkuu. Umechelewa sana.
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametoa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha!

Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balozi Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana. Na karibu wote wanaobisha au kupinga uraia pacha hawajui maana ya uraia pacha na taratibu za mtu kuwa raia pacha. Si watu wa kusikilizwa katika msingi huu, waelimishwe kwanza, kutia ndani na wabunge.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​

I concur 200%. I am one of the affected and i hate the fact that when i come to Tanzania to visit i am taken as a foreigner (this thing hurts) why because i couldn’t keep both nationalities. I love my country alot and i wanna do alot but my hands are tight cuz at the end of the day i am just a “foreigner”. Born, raised and grew up in Tanzania, now i am a foreigner. Most countries surrounding us allow dual citizenship, it’s high time Tanzania grew out of old mindset and be open minded, that way investors will even feel okay to come. That’s all. Until then i will hope and pray.
 
Naunga mkono HOJA.

Hofu ya wapingaji ni kuwa nchi ikiruhusu uraia pacha, wataochukua uraia huko kwingine wanaeza kuwa Wazalendo zaidi huko jambo ambalo si kweli.

Mchina akija Tanzania akanunua uraia, hawezi kuipenda Tz kuliko huko alikozaliwa.

Damu ni nzito kuliko maji, wahenga walisema..
Ni makosa kulingalisha uraia wa kuzaliwa na ule wa kununua ili upate maslahi fulani.

Ni vizuri Uraia pacha uruhusiwe wananchi wawe huru kupata fursa nyingi huko nje
Jamani, uraia pacha hauuzwi, labda kama nchi iamue tuwe na utaratibu wa kuuza uraia pacha. Kwa hiyo Mchina hawezi kuja Tanzania kununua uraia pacha.

Kigezo cha kwanza cha kuwa raia pacha kwa kawaida ni kwamba huyo Mchina awe ameishi Tanzania mfululizo kwa kipindi kisichopungua miaka 5, au awe ameoa/ameolewa na Mtanzania na kuwa katika ndoa kwa zaidi ya miaka 3, nk. Hivyo ni vigezo tutaamua wenyewe, hakuna mtu wa kutupangia. Tunaweza hata kuwa na sharti kwamba Mtanzania mwenye uraia pacha asigombee nafasi ya kisiasa kama ubunge na uraisi, au asitumike katika nafasi za vyombo vya usalama kama JW, TISS na polisi. Ni uamuzi wetu.

Kwa hiyo uraia pacha hautolewi kama kununua nyanya sokoni, unakuja kwa masharti ambayo kila nchi inaweka.

Ni kweli kuna nchi zimeweka masharti kwamba ukiingiza nchini kuanzia USD 250,000 una qualify kupewa uraia. Na nchi kama Norway wakati fulani ilikuwa ukioa au kuolewa na Mnorway basi unakuwa raia wa Norway moja kwa moja, wakaja wakabadilisha kwamba lazima uishi na mkeo/mumeo kwa angalau miaka 3, na kuwe na uthibitisho kuwa kweli mnaishi kama mume na mke.

Kwa hiyo watu wengi hawaelewi suala la uraia pacha, wanadhani watu watakuja kuununua Tanzania bila vigezo. Haiko hivyo

Watu watakaopata uraia pacha kirahisi ni Watanzania wenyewe, sio raia wa nje, na hao Watanzania kupata uraia pacha na nchi nyingine inategemea masharti ya nchi wanayotaka kuchukua uraia wa pili
 
I say, hadi leo kuna watu wanaabudu kwenda majuu!!! Pole sana Mkuu. Umechelewa sana.
Siyo kuabudu wala nini. Acha vijana wenzako walioweza kwenda kule wapate haki yako badala ya roho ya korosho. Majuu patabaki kuwa majuuu as long as Afrika bado tuna mijitu yenye roho zenye kutu kama wewe.
 
Mkuu Ingawa sina Hoja kali kama Zako ila Uraia Pacha utatuua...wahinndiu watachukua kila tuu kuanzia ajira...
Hapa Tuu sasa hivi wao ndio wanaongoza kwa Uraia Pacha wa Uingereza,Canada na India na hapa Bongo wamebadilisha sana Visa/Permit to work Wengine wanaishi zaidi ya Miaka 10
Kufanya Kazi eti ya Expert anabadilisha tuu cheo,Leo hiki kesho kile ili isibumbuluke...Uhamiaji ni sheeedah,Wahindi Shikamooni...
Mmewakomoa sana migration hadi Wameshiba tena wanawasaidia namna ya Kuishi
Kwani wahindi sasa hawachukui na hawana uraia pacha? Mkiwaendekeza watawamaliza hasa ikizingatiwa kuwa wanawatumia nyinyi manajiona wazalendo kuibia taifa. Waliokaa nje hawababaishwi na wahindi. Kwani huko nje wote wanaonekana people of colours. Wapo kwenye kapu moja katika kubaguliwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom