mtanzania in exile
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 1,335
- 1,183
Eeee ndugu wacha kusema maneno bila kuwa na uhakika na unachokisema, utasemaje kuwa wayahudi hawana uraia pacha ilhali inajulikana fika kuwa wapo tele hususan matajiri wakubwa wa kiyahudi waishio nchi kama france, uk na usa wana uraia pacha? Israel inawafurahia kabisa kabisa wananchi wao kuwa na uraia pacha na wako kirahisi kuwapa uraia wale mayahudi ambao wamezaliwa nje ya nchi na ambao wanataka uraia wa kiyahudi. Kama utakumbuka hivi karibuni israeli wamempa uraia yule tajiri anaemiliki chelsea kirahisi kabisa, ili kumwezesha kuingia na kutoka katika nchi za europe na pia kuweza kuinvest nchini isarael.Kwa vipi uamue kuwa na double face?
Kwa nini usichague nchi moja tu na kuchukua uraia wake??
Jambo lipi linakuzuia kuchagua sehemu moja ya kuishi mpaka ulazimike kuishi na pasi mbili za kusafiria? Unajaribu kuficha au kupata nini cha ziada??
Kwenye makala umesema wengi wa wanaopinga uraia pacha hawajahi kuishi nie ya nchi. Hili nalo siyo kweli na hata kama lina ukweli bado halizuii kuibuka kwa maswali yanayohoji motive ya kutaka uraia pacha!!
Kama ni diaspora kuchangia nchini kwao mbona watahudi wanaweza bila kuwa na uraia pacha???
Tuache propaganda uchwara za kusingizia diaspora wakipata uraia pacha wataweza kuisaidia nchi hilo halina ukweli!
Ama hayo masuali yako ya mwanzo, sina haja ya kukujibu, ila tu ikiwa hamtaki kutowa uraia wa pacha sawa, lakini wacheni kukaa kila siku kutowa wito kwa walio nje waje kusaidia Tanzania. Wao wameshatoa sharti lao ni kuwa muwaruhusu kuwa na uraia pacha, kama hamtaki basi! Wao wataendelea kuwasaidia familia zao nyumbani na nyie endeleeni kuwaruhusu wachina na wageni wengine kuja tanzania kuekeza na kuwanyanyasa ndugu zetu!