Ushauri kwa Askofu Gwajima: Jiuzulu Ubunge utakuwa shujaa. Huwezi kumtumikia Mungu na kuendesha shughuli za siasa Tanzania

Hana sababu ya kujiuzulu. Wale wanafiki walikuwa wanamsakama. Chanjo ya Covid ina matatizo,yeye hana sababu ya kujiuzulu. Ushauri wako ni mbaya.
Aende Bungeni aongee kuhusu mambo mengine. Kwenye pulpit aongee mambo mengine. Hakuna haja ya kuitaja Covid 19 vaccine na kusababisha mabomu ya machozi yarushwe Kanisani.
Sidhani kama wafuasi wake wanataka ajiuzulu.
Hakuna mtu amemtishia maisha. Ajiuzulu tu kwa sababu watu wanaongea blah blah? Maneno mangapi ya wazabizabina wewe unavumilia mtaani?
 
Wewe waka maandiko hapa. Ubishi wa hadithi hapana.

Ni wapi Bwana Yesu alisema "Ya Mungu Mwachieni Mungu na ya Kaisari mwachieni kaisari?", weka andiko. Halafu kama wewe ndiye unatunga hiyo sheria, wakisha acha ya Mungu na ya kaisari, wafanye ya nani?

Katiba ya Marekani ni Biblia yako?

Biblia inasema mabwana wawili., hapa unaaply vipi hili andiko? Katika suala la siasa na uchungaji, mabwana wawili hapa ni nani na nani?

Weka mistari ya Biblia "citations:, " ili tukupe maarifa ambayo huna.
Maarifa unayotaka kunipa,ni maarifa ya ujuzi wa binadamu,hekima ambayo mtume Paulo ameiita ni upumbavu mbele za MUNGU, kusema kweli madaraka ni matamu na fedha ni tamu pia,hii inapelekea kiongozi wa kanisa kugombea vyeo vya kisiasa.hakuna justification hapo.
 
Ndugu Pastor Gwajima, siasa za Tanzania hususani chama chako pendwa zimejaa unafiki, wabunge wengi wanatetea matumbo yao na hivyo hulazimika kuwa wanafiki ili wapate wanachokitaka!

Kwako wewe, Kama Mtumishi wa Mungu , hukupaswa kuingia katika siasa bila kupima hali ya unafki na uongo uongo unaendelea katika chama chako, utapotea kiroho, utawapotosha na wafuasi wako!

Bila shaka, wewe ndiye chanzo Cha Spika Ndugai kuropoka eti yesu alikuwa na mke, haya mambo yanadhalilisha ukristo, yanaonesha ni jinsi gani katika ukristo mtu yoyote anaweza kuwa pastor na kwamba ana elimu kuwazidi wale walioenda kusomea masuala ya thiolojia mpaka level ya PhD!

Ili ufanye siasa za Tanzania kistaarabu, lazima uwe mnafiki na Mungu hataki wanafiki!

Nakushauri Jiuzulu Ubunge, ili ukamtumikie Mungu katika roho na kweli , ukitubia dhambi ya kujiunga na chama hicho Cha majambazi, mkashirikiana kupora uchaguzi 2020!

Usipojiuzuru, wewe hutakua na Nia njema na waumini wako, utazidi kujifedhehesha na Mungu atakushusha Kama jinsi ilivyo Sasa ambavyo watu wanakushusha!
Gwajima hawezi kujiuzulu wala hamtumkii Mungu wala yeyote isipokuwa tumbo lake. Hivyo, wito kama huu ni maudhi kwake.
 
Chama kinamfukuza,uhujumu uchumi na uchochezi vinamhusu.


Aaah wapi!

Hayamfiki !

Wamfukuze unataka wayafumue ya wale wabunge 19 walofukuzwa uanachama?
Unataka waonekane wanafanya double standard?

Kwani wewe unachuki binafsi na Gwajima?

Mojawapo ya wanamchukia Rev Gwajima ni wachawi maana wanamuona huwa anawaharibia mipango yao ya uharibifu wa maisha ya watu!
 
Yaani Gwajiboy unamwita Rev? Pumbavu


Ndio ni Rev.kabisa pasina shaka!

Wanadamu wote wanamapungufu sema yanazidiana.

Viongozi wa dini wote wanamapungufu.

Niambie kina nani ni wakamilifu?

Unaijuamienendo yao?

Wengine wachawi, wafugamajini, waasherati, wazinifu, walevi, washirikina n.k

Kwa hiyo wewe husuda yako iko kwa Gwajima tu?
 
Ndugu Pastor Gwajima, siasa za Tanzania hususani chama chako pendwa zimejaa unafiki, wabunge wengi wanatetea matumbo yao na hivyo hulazimika kuwa wanafiki ili wapate wanachokitaka!

Kwako wewe, Kama Mtumishi wa Mungu , hukupaswa kuingia katika siasa bila kupima hali ya unafki na uongo uongo unaendelea katika chama chako, utapotea kiroho, utawapotosha na wafuasi wako!

Bila shaka, wewe ndiye chanzo Cha Spika Ndugai kuropoka eti yesu alikuwa na mke, haya mambo yanadhalilisha ukristo, yanaonesha ni jinsi gani katika ukristo mtu yoyote anaweza kuwa pastor na kwamba ana elimu kuwazidi wale walioenda kusomea masuala ya thiolojia mpaka level ya PhD!

Ili ufanye siasa za Tanzania kistaarabu, lazima uwe mnafiki na Mungu hataki wanafiki!

Nakushauri Jiuzulu Ubunge, ili ukamtumikie Mungu katika roho na kweli , ukitubia dhambi ya kujiunga na chama hicho Cha majambazi, mkashirikiana kupora uchaguzi 2020!

Usipojiuzuru, wewe hutakua na Nia njema na waumini wako, utazidi kujifedhehesha na Mungu atakushusha Kama jinsi ilivyo Sasa ambavyo watu wanakushusha!
Naunga mkono hoja!!.
 
Bila shaka , yawezekana umekurupuka bila kukaa na kutafakari Nini ambacho nmeshauri!

Gwajima sio mtu wa Kwanza kuwa pastor, wapo ambao walikua magwiji kuliko yeye, lakini hawakuwahi kujiingiza katika vikundi vya wanafiki!
Mfano mzuri Ni Daudi! Anatwambia katika
Zaburi 26:4
Sikuketi pamoja na watu wa ubatili,
Wala sitaingia mnamo wanafiki.

Kwa Nini??
Wanafiki wamefananishwa na makaburi yaliyopakwa chokaa huku ndani wakirundika uchafu wa Kila aia Kama jinsi ilivyo katika chama chako pendwa Cha kijani!

Mathayo 23:27
Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote.

Swali Ni je?, Daudi alikosea kutojishikamanisha na wanafiki??
Unashindwaje kupata tafsiri ya moja kwa moja ya andiko ulisomalo?

1. Unajua/unakubali kwamba Daudi alikuwa mfalme? Mwanasiasa wa ngazi ya juu katika taifa?

2. Kwa hiyo kama Daudi aliposema hakuketi na wadanganyifu wala kuambatana na wanafiki, alikuwa na maana ya kutokuingia wala kuhusika na nafasi za siasa na uongozi wa nchi kaam unavyolazimisha wewe, alipoandika hiyo mistari, aliacha ufalme? Allijiuzuru nafasi yake ya ufalme?

3. Au kwa maana yako ni kwamba katika Israel hapakuwa na wanafiki wala waharifu kwa wakati ule?

4. Kwa kukusaidia, andiko ulilolinakiri, halina maana ya kutokushiriki katika masuala ya uongozi wa kitaifa, ndiyo maana Daudi hajawahi kujiuzuru uongozi pamoja na kuzingirwa na kila aina ya watu waovu na wengine wakiwa katika familia yake.

5. Anapoongea kuambatana maana yake ni kushiriki, kubariki, kukubaliana ama kufanikisha ama kuungana, na kuunga hoja za uovu na unafiki. Na hicho ndicho anachokifanya Gwajima. Haungani na uovu wala unafiki wowote na ndiyo sababu ya vikao, adhabu, matusi na kila aina ya kudhikishwa anachofanyiwa na watu wenye uovu ndani yao.

6. Je, "Bunge, Serikali ama mamlaka za uongozi wa Taifa", ni magenge yalilyoasisiwa kufanikisha hila, unafiki na uovu kama vyama vya freemason, umoja wa wachawi, magenge ya majambazi, jumiya ya kigaidi hadi umhukumu mtu anayejiunga nayo anafanya machukizo mbele za Mungu? Naomba ujibu hoja hii. Kwa kusaidia, kuwepo kwa watu wanafiki, waovu na waharibifu bungeni ama serikalini, ni kweli wanaweza kuwepo tena yamkini wakawa wengi kuliko wenye haki kama ianvyoonekana. Lakini utambue kwamba makusudi ya uwepo wake si uharifu nandiyo sababu Gwajima anajitahidi kurekebisha ili yamkini wakumbuke misingi ya uwepo wao.

7. Uanposema watu wa Mungu wasiingie Bungeni wala serikalini kwa kuwa kuwa uovu, nani aongoze taifa? Kwa hiyo tuachie sera na mihimili yote ya taifa iundwe kwa misingi ya kishetani? Wewe uishi maisha gani? (Kwa mantiki mnayoitaionyesha hapa).

DAUDI ALIGOMA KUKUBALIANA, KUAMBATANA NA KUKETI KATIKA UNAFIKI NA UAHRIBIFU, NA NDICHO KITU GWAJIMA ANAFANYA.
Na kwa nyongeza:-
1. Daniel 3: 30 "Kisha mfalme akawakuza Shadraka, na Meshaki, na Abednego, katika wilaya ya Babeli". Hawa hawakuwa watumishi wa Mungu?

2.Mwanzo 41:40
Wewe ndiwe utakayeisimamia nchi yangu, na watu wangu wote watakuwa chini ya amri yako. Mimi tu ndiye mkuu kuliko wewe kwa kuwa nakalia kiti cha kifalme. Je, hapa Yusufu, hakuwa mtumishi wa Mungu?

3. Mithali 29: 2 Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua. (Hapa anamaanisha watu wa Mungu wasiwe viongozi?

4. Hao waamuzi wote kina Nathan, Debora, Gideon, Jotham, na wengien wengi katika maisha yao ya siasa, hawakuwa watu wa Mungu?

NAOMBA MTAFUTE MAARIFA ZAIDI YA KUMJUA MUNGU NA NENO LAKE, BADALA YA KUPOTOSHA WATU.
MWACHENI GWAJIMA AFANYE KAZI YA MUNGU NDANI YA NCHI KWA KUWA MUNGU AMEMPA UWEZO HUO.
 
Na kanisa lishaanza kujadiliwa huyu ataishia jela

Hata Bwana wake aliyemwita na kumpa kazi hiyo naye alikwenda, jela na akahukumiwa kifo, na hukumu ikatekelezwa ya kumuua lakini siku ya Tatu akaibuka Mshindi. Milele ni mshindi na ndiye anayewapeleka puta wenye hila dhidi yake na watu wake. Kwa misingi hiyo hiyo, suala la jela siyo geni kwa Gwajima na siyo tatizo kwake na wote wamjuao Mungu. Sema lingine. Lakini mwisho wa siku Kristo ni Mshindi.
 
Unashindwaje kupata tafsiri ya moja kwa moja ya andiko ulisomalo?

1. Unajua/unakubali kwamba Daudi alikuwa mfalme? Mwanasiasa wa ngazi ya juu katika taifa?

2. Kwa hiyo kama Daudi aliposema hakuketi na wadanganyifu wala kuambatana na wanafiki, alikuwa na maana ya kutokuingia wala kuhusika na nafasi za siasa na uongozi wa nchi kaam unavyolazimisha wewe, alipoandika hiyo mistari, aliacha ufalme? Allijiuzuru nafasi yake ya ufalme?

3. Au kwa maana yako ni kwamba katika Israel hapakuwa na wanafiki wala waharifu kwa wakati ule?

4. Kwa kukusaidia, andiko ulilolinakiri, halina maana ya kutokushiriki katika masuala ya uongozi wa kitaifa, ndiyo maana Daudi hajawahi kujiuzuru uongozi pamoja na kuzingirwa na kila aina ya watu waovu na wengine wakiwa katika familia yake.

5. Anapoongea kuambatana maana yake ni kushiriki, kubariki, kukubaliana ama kufanikisha ama kuungana, na kuunga hoja za uovu na unafiki. Na hicho ndicho anachokifanya Gwajima. Haungani na uovu wala unafiki wowote na ndiyo sababu ya vikao, adhabu, matusi na kila aina ya kudhikishwa anachofanyiwa na watu wenye uovu ndani yao.

6. Je, "Bunge, Serikali ama mamlaka za uongozi wa Taifa", ni magenge yalilyoasisiwa kufanikisha hila, unafiki na uovu kama vyama vya freemason, umoja wa wachawi, magenge ya majambazi, jumiya ya kigaidi hadi umhukumu mtu anayejiunga nayo anafanya machukizo mbele za Mungu? Naomba ujibu hoja hii. Kwa kusaidia, kuwepo kwa watu wanafiki, waovu na waharibifu bungeni ama serikalini, ni kweli wanaweza kuwepo tena yamkini wakawa wengi kuliko wenye haki kama ianvyoonekana. Lakini utambue kwamba makusudi ya uwepo wake si uharifu nandiyo sababu Gwajima anajitahidi kurekebisha ili yamkini wakumbuke misingi ya uwepo wao.

7. Uanposema watu wa Mungu wasiingie Bungeni wala serikalini kwa kuwa kuwa uovu, nani aongoze taifa? Kwa hiyo tuachie sera na mihimili yote ya taifa iundwe kwa misingi ya kishetani? Wewe uishi maisha gani? (Kwa mantiki mnayoitaionyesha hapa).

DAUDI ALIGOMA KUKUBALIANA, KUAMBATANA NA KUKETI KATIKA UNAFIKI NA UAHRIBIFU, NA NDICHO KITU GWAJIMA ANAFANYA.
Na kwa nyongeza:-
1. Daniel 3: 30 "Kisha mfalme akawakuza Shadraka, na Meshaki, na Abednego, katika wilaya ya Babeli". Hawa hawakuwa watumishi wa Mungu?

2.Mwanzo 41:40
Wewe ndiwe utakayeisimamia nchi yangu, na watu wangu wote watakuwa chini ya amri yako. Mimi tu ndiye mkuu kuliko wewe kwa kuwa nakalia kiti cha kifalme. Je, hapa Yusufu, hakuwa mtumishi wa Mungu?

3. Mithali 29: 2 Wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi; Bali mwovu atawalapo, watu huugua. (Hapa anamaanisha watu wa Mungu wasiwe viongozi?

4. Hao waamuzi wote kina Nathan, Debora, Gideon, Jotham, na wengien wengi katika maisha yao ya siasa, hawakuwa watu wa Mungu?

NAOMBA MTAFUTE MAARIFA ZAIDI YA KUMJUA MUNGU NA NENO LAKE, BADALA YA KUPOTOSHA WATU.
MWACHENI GWAJIMA AFANYE KAZI YA MUNGU NDANI YA NCHI KWA KUWA MUNGU AMEMPA UWEZO HUO.
Aya mkuu, muda utatwambia, tutarudi Tena kwenye uzi huu!

Nadhan, umeona hatua inayofuata gwajima ametengenezewa mazingira ya kufikishwa kwa DCI na DPP!
 
Ndio ni Rev.kabisa pasina shaka!

Wanadamu wote wanamapungufu sema yanazidiana.

Viongozi wa dini wote wanamapungufu.

Niambie kina nani ni wakamilifu?

Unaijuamienendo yao?

Wengine wachawi, wafugamajini, waasherati, wazinifu, walevi, washirikina n.k

Kwa hiyo wewe husuda yako iko kwa Gwajima tu?
Kwanza futa kuwa nina husda, pili hata kama ni Padre au nani lazima nimshushe hicho cheo pindi nikijua ujinga anaofanya kama Gwajiboy aka Askofu Rashidi. Nakuomba usitumie Rev ukiwa unamlifaa mtu kama Gwajiboy.
 
Hata Bwana wake aliyemwita na kumpa kazi hiyo naye alikwenda, jela na akahukumiwa kifo, na hukumu ikatekelezwa ya kumuua lakini siku ya Tatu akaibuka Mshindi. Milele ni mshindi na ndiye anayewapeleka puta wenye hila dhidi yake na watu wake. Kwa misingi hiyo hiyo, suala la jela siyo geni kwa Gwajima na siyo tatizo kwake na wote wamjuao Mungu. Sema lingine. Lakini mwisho wa siku Kristo ni Mshindi.
Waganga njaa utawajua tu.....
 
Back
Top Bottom