Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,428
Disclaimer;
Mtoa ushauri huu ni mwana CCM anayeamini katika demokrasia. Anaamini CCM imara itatokana na uwepo wa upinzani bora kwa kuwa CCM itapata kioo cha kujitazama, na kufa kwa upinzani kutasababisha CCM isiwe na pa kujipimia na hivyo ubora wake kuyumba.Kama Simba ikipotea kabisa, hatuwezi kuwa na Yanga tunayoijua leo, bali tutakuwa na kitu kingine kabisa.
Hivyo ushauri huu haulengi kusaidia vyama vya upinzani kushinda kiti cha urais Tanzania bara kwa kuwa hilo kwa sasa haliwezekani (kutokana na sababu mbalimbali) lakini angalau kusaida vyama hivyo kubaki kwenye ramani baada ya uchaguzi wa oktoba.
================
‘Facts nne (4) za wazi sana (Hizi ukiona mtu anabisha ni kwa kuwa tu anatumia uhuru wake wa kidemokrasia. Ni kama mtu anavyoweza kubisha kuwa dunia sio duara)
Kwanza, kwa hali ilivyo kuna dalili za wazi sana kwa CHADEMA kupoteza karibu viti vyote vya ubunge bara, na Zbar hawana dalili ya kupata kiti hata kimoja.(ili kuepuka kutanua sana mjadala hatutajadili sababu moja moja kwa kuwa zipo wazi sana tayari)
Pili, ACT wana dalili ya kutopata kiti hata kimoja bara lakini kupata viti kadhaa Zbar
Tatu, kwa upande wa urais bara, Rais Magufuli ana uhakika wa kishinda kwa 99%. Kwa sababu ambazo pia ziko wazi sana. na
Nne, Vyama vya upinzani vyenye ushawishi kiasi kwa bara kwa sasa ni CHADEMA na ACT, wengine ushawishi wao uko chini sana.
Kwa nini CHADEMA wamsimamishe Membe na ACT wasisimamishe mgombea?
Kwanza, Lissu ndie mpinzani pekee anayeweza kum challenge rais Magufuli kwa kiasi fulani, japo pia hawezi kumshinda kwa sababu mbalimbali. Kwa bahati mbaya lisu yuko ulaya na ndege haziruki kutoka ulaya kwa sasa. Kwa hiyo upo uwezekano ukafika wakati wa kuchukua fomu na Lissu kakwama ulaya.
Pili, kuhusu mbowe; kwa tukio lililotokea Dodoma, iwe maelezo yaliyotolewa kwa upande wa polisi ndio kweli au maelezo yaliyotolewa upande wa Mbowe ndio kweli; tukio kama lile kutokea kwenye kipindi hiki linamfanya Mbowe kuonekana hayuko serious vyakutosha na hivyo sio ‘presidential material’.
Tatu , kuhusu Msigwa; Kwa tukio la kumsingizia mzee Kinana kuwa anaua tembo (huku akijua ametunga tu kichwani kwake kwa hila) na asiombe msamaha kwa miaka na miaka hadi ahukumiwe mahakamani huku akijua anasababisha usumbufu usio wa lazima, linamfanya asiwe ‘presidential material’.
Nne, kuhusu Nyalandu; huyu kalelewa na CCM, kawa waziri wa muda mrefu na hana ushawishi wa kutosha kwenye level ya urais Tanzania bara.
Tano, Kuhusu Zitto; kwa sababu mbalimbali kiwango chake cha kuaminika kimepungua kwa sababu mbalimbali. Hivyo, akigombea urais hawezi kupata hata 10% ya kura. Aidha, hataungwa mkono na CHADEMA, na ndani ya ACT hakuna mtu mwingine ambaye ni ‘presidential material’ kwa Tanzania bara anayeweza kuwa na ushawishi zaidi ya Zitto.
Kwa nini Membe?
Kwa sababu ukimuacha Lisu, upande wa vyama vya upinzani hakuna mtu mwingine Tanzania bara mwenye haiba ya urais inayomkaribia Membe. Kwa mantiki hiyo, ijapokuwa Membe hatamshinda Rais Magufuli; angalau atasaidia CHADEMA kujipatia % fulani la kura ambayo itasaidia waendelee kupata ruzuku japo kidogo na uwepo wao uendelee kuonekana.Ikombukwe hapo tayari watakuwa washapoteza viti karibu vyote vya ubunge!
Ingawa ni kweli kwamba Membe bado anaiwazia CCM, lakini ni kweli pia kwamba kwa sasa hana uwezekano tena wa kugombea kupitia CCM. Sasa kwa kuwa tatizo la Tanzania sio CCM kama chama bali mtu mmoja mmoja, CHADEMA wakimtumia Membe ili awabusti sio jambo baya kwa kuwa ana haiba chanya zaidi ukilinganisha na wengine wengi waliotajwa hapo juu.
Kwa upande wa ACT, viti kadhaa watakavyopata Zbar, vitawasaidia kuendelea kuonekana na kupata ka - ruzuku kidogo katakako wasaidia ku ‘savaivu’.
Najua wapo watakaobisha, kutukana, na kubeza ushauri huu, ila ushauri huu unazingatia zaidi ‘facts’ ziwe za kuvutia au za kuudhi. Ni hiari ya wahusika kuufuata na wapate namna yenye uafadhali ya kuendelea ku ‘savaivu’ kwenye kipindi cha 2021 -2025, au wapuuze halafu wawe kama TLP, NLD n.k Kama watapuuza na kufikia hatua hiyo, CCM itakosa pakujitizama hiyo nayo utendaji wake unaweza kuathirika kwa namna hasi na kwa kuwa kitakuwa ndicho chama kinachounda serikali, taifa nalo linaweza kukabiliwa na changamoto kadha wa kadha ambazo pengine zingeepukika kwa kufuata ushauri huu.
Kuna wazo kwamba CCM inaweza ikaamua kuwaachia vyama vya upinzani viti kadhaa kwa makusudi ili viendelee kuwepo. Hiyo ni kweli lakini sishauri vyama vya upinzani kutegemea favor kutoka CCM. Wanaweza wasipewe hiyo favor na ikawagharimu sana.
Mtu anaweza kusema kwa nini vyama vya upinzani visipewe ushauri utakaowawezesha kushinda? Jibu ni kwamba ushauri huo walishapewa sana na kuelezwa kwamba pamoja na changamoto za nje zinazowakabili, changamoto kubwa zinazowakwamisha ziko ndani ya vyama vyao wenyewe. Kwa bahati mbaya hilo hawajaliamini hadi sasa na kwa kuwa hawajaliamini na wanadhani changamoto zinazowakabili ni ‘100% external’; hawajachukua hatua na muda uliobaki ni mfupi mno ambao hauwezi kuwatosha tena. Ndio maana ushauri unaowezekana kwa sasa anagalau ni ule wa kuwawezesha waendelee ku ‘savaivu’ lakini sio kushinda.
Tunawashukuru sana kwa kuelewa.
Mtoa ushauri huu ni mwana CCM anayeamini katika demokrasia. Anaamini CCM imara itatokana na uwepo wa upinzani bora kwa kuwa CCM itapata kioo cha kujitazama, na kufa kwa upinzani kutasababisha CCM isiwe na pa kujipimia na hivyo ubora wake kuyumba.Kama Simba ikipotea kabisa, hatuwezi kuwa na Yanga tunayoijua leo, bali tutakuwa na kitu kingine kabisa.
Hivyo ushauri huu haulengi kusaidia vyama vya upinzani kushinda kiti cha urais Tanzania bara kwa kuwa hilo kwa sasa haliwezekani (kutokana na sababu mbalimbali) lakini angalau kusaida vyama hivyo kubaki kwenye ramani baada ya uchaguzi wa oktoba.
================
‘Facts nne (4) za wazi sana (Hizi ukiona mtu anabisha ni kwa kuwa tu anatumia uhuru wake wa kidemokrasia. Ni kama mtu anavyoweza kubisha kuwa dunia sio duara)
Kwanza, kwa hali ilivyo kuna dalili za wazi sana kwa CHADEMA kupoteza karibu viti vyote vya ubunge bara, na Zbar hawana dalili ya kupata kiti hata kimoja.(ili kuepuka kutanua sana mjadala hatutajadili sababu moja moja kwa kuwa zipo wazi sana tayari)
Pili, ACT wana dalili ya kutopata kiti hata kimoja bara lakini kupata viti kadhaa Zbar
Tatu, kwa upande wa urais bara, Rais Magufuli ana uhakika wa kishinda kwa 99%. Kwa sababu ambazo pia ziko wazi sana. na
Nne, Vyama vya upinzani vyenye ushawishi kiasi kwa bara kwa sasa ni CHADEMA na ACT, wengine ushawishi wao uko chini sana.
Kwa nini CHADEMA wamsimamishe Membe na ACT wasisimamishe mgombea?
Kwanza, Lissu ndie mpinzani pekee anayeweza kum challenge rais Magufuli kwa kiasi fulani, japo pia hawezi kumshinda kwa sababu mbalimbali. Kwa bahati mbaya lisu yuko ulaya na ndege haziruki kutoka ulaya kwa sasa. Kwa hiyo upo uwezekano ukafika wakati wa kuchukua fomu na Lissu kakwama ulaya.
Pili, kuhusu mbowe; kwa tukio lililotokea Dodoma, iwe maelezo yaliyotolewa kwa upande wa polisi ndio kweli au maelezo yaliyotolewa upande wa Mbowe ndio kweli; tukio kama lile kutokea kwenye kipindi hiki linamfanya Mbowe kuonekana hayuko serious vyakutosha na hivyo sio ‘presidential material’.
Tatu , kuhusu Msigwa; Kwa tukio la kumsingizia mzee Kinana kuwa anaua tembo (huku akijua ametunga tu kichwani kwake kwa hila) na asiombe msamaha kwa miaka na miaka hadi ahukumiwe mahakamani huku akijua anasababisha usumbufu usio wa lazima, linamfanya asiwe ‘presidential material’.
Nne, kuhusu Nyalandu; huyu kalelewa na CCM, kawa waziri wa muda mrefu na hana ushawishi wa kutosha kwenye level ya urais Tanzania bara.
Tano, Kuhusu Zitto; kwa sababu mbalimbali kiwango chake cha kuaminika kimepungua kwa sababu mbalimbali. Hivyo, akigombea urais hawezi kupata hata 10% ya kura. Aidha, hataungwa mkono na CHADEMA, na ndani ya ACT hakuna mtu mwingine ambaye ni ‘presidential material’ kwa Tanzania bara anayeweza kuwa na ushawishi zaidi ya Zitto.
Kwa nini Membe?
Kwa sababu ukimuacha Lisu, upande wa vyama vya upinzani hakuna mtu mwingine Tanzania bara mwenye haiba ya urais inayomkaribia Membe. Kwa mantiki hiyo, ijapokuwa Membe hatamshinda Rais Magufuli; angalau atasaidia CHADEMA kujipatia % fulani la kura ambayo itasaidia waendelee kupata ruzuku japo kidogo na uwepo wao uendelee kuonekana.Ikombukwe hapo tayari watakuwa washapoteza viti karibu vyote vya ubunge!
Ingawa ni kweli kwamba Membe bado anaiwazia CCM, lakini ni kweli pia kwamba kwa sasa hana uwezekano tena wa kugombea kupitia CCM. Sasa kwa kuwa tatizo la Tanzania sio CCM kama chama bali mtu mmoja mmoja, CHADEMA wakimtumia Membe ili awabusti sio jambo baya kwa kuwa ana haiba chanya zaidi ukilinganisha na wengine wengi waliotajwa hapo juu.
Kwa upande wa ACT, viti kadhaa watakavyopata Zbar, vitawasaidia kuendelea kuonekana na kupata ka - ruzuku kidogo katakako wasaidia ku ‘savaivu’.
Najua wapo watakaobisha, kutukana, na kubeza ushauri huu, ila ushauri huu unazingatia zaidi ‘facts’ ziwe za kuvutia au za kuudhi. Ni hiari ya wahusika kuufuata na wapate namna yenye uafadhali ya kuendelea ku ‘savaivu’ kwenye kipindi cha 2021 -2025, au wapuuze halafu wawe kama TLP, NLD n.k Kama watapuuza na kufikia hatua hiyo, CCM itakosa pakujitizama hiyo nayo utendaji wake unaweza kuathirika kwa namna hasi na kwa kuwa kitakuwa ndicho chama kinachounda serikali, taifa nalo linaweza kukabiliwa na changamoto kadha wa kadha ambazo pengine zingeepukika kwa kufuata ushauri huu.
Kuna wazo kwamba CCM inaweza ikaamua kuwaachia vyama vya upinzani viti kadhaa kwa makusudi ili viendelee kuwepo. Hiyo ni kweli lakini sishauri vyama vya upinzani kutegemea favor kutoka CCM. Wanaweza wasipewe hiyo favor na ikawagharimu sana.
Mtu anaweza kusema kwa nini vyama vya upinzani visipewe ushauri utakaowawezesha kushinda? Jibu ni kwamba ushauri huo walishapewa sana na kuelezwa kwamba pamoja na changamoto za nje zinazowakabili, changamoto kubwa zinazowakwamisha ziko ndani ya vyama vyao wenyewe. Kwa bahati mbaya hilo hawajaliamini hadi sasa na kwa kuwa hawajaliamini na wanadhani changamoto zinazowakabili ni ‘100% external’; hawajachukua hatua na muda uliobaki ni mfupi mno ambao hauwezi kuwatosha tena. Ndio maana ushauri unaowezekana kwa sasa anagalau ni ule wa kuwawezesha waendelee ku ‘savaivu’ lakini sio kushinda.
Tunawashukuru sana kwa kuelewa.