mvukiyefrancis
Member
- Dec 8, 2012
- 31
- 8
Wana JF, Poleni na kazi ya kuelimisha wajasiliamali. Mimi nina kuku takribani 300, ni wale wekundu wa kisasa wa MAYAI. Tangu mwezi huu wa sita uanze, kuku hao wameacha kabisa kutaga. Leo ndo nimeokota only yai moja tu. Nashindwa kuelewa sababu. Mimi niko MBEYA eneo la ITUHA. Kwa upande wa kuku wa kienyeji, wao wanakwenda vizuri sana na idadi ya mayai yanaridhisha sana. Hao kuku wa mayai wa kisasa wana miezi 2 tu tangu waanze kutaga. Naombeni ushauri au labda ni kwa ajili ya kipindi hiki cha baridi au vinginevyo? Niokoeni imenichanganya sana . NAOMBA USHAURI hata kwa simu o752 345066 au 0715 274128 .