Ushauri kuhusu Fursa za kazi za muda(Vibarua) zilizopo Sweden

mkuu shida ya Sweden Scholarship lazima ulipe application fee for addmision
Kiongozi mmoja mkubwa mstaafu hapa Nchini aliwahi kusema " Ukitaka kula sharti ukubali kuliwa".

Kwahiyo kutoa admission fee ya takribani Tsh 230,000 ili upate Scholarship ya mamilioni siyo hasara kubwa Mkuu.!
 
Kiongozi mmoja mkubwa mstaafu hapa Nchini aliwahi kusema " Ukitaka kula sharti ukubali kuliwa".

Kwahiyo kutoa admission fee ya takribani Tsh 230,000 ili upate Scholarship ya mamilioni siyo hasara kubwa Mkuu.!
Sasa hapo siinakuwa probability ya schorship maana unaweza kutoa hiyo hella na huna uhakika wakupa scholarship
 
Sasa hapo siinakuwa probability ya schorship maana unaweza kutoa hiyo hella na huna uhakika wakupa scholarship
Mkuu, katika maisha usiogope ku-take risk. Tafiti zinaonesha kuwa watu wengi waliofanikiwa katika maisha haya wengi wao walifanya maamuzi magumu(ku-take risk).
 
Wakuu habari za Majukumu!

Kuanzia mwezi August natarajia kuwa Sweden. Nimepata Scholarship ya kusoma masters. Hivyo, kwakuzingatia hali yetu kiuchumi sisi Wabongo, tunapopata fursa moja basi hujaribu kuangazia hapa na pale kuhusu fursa nyingine zaidi.

Muda ambao nitakuwa free, haswa wakati wa research na wakati mwingine ambapo masomo yanakuwa hayajachanganya, nataka niwe nafanya kazi ya muda (Part time job). Kwakuwa JF ni wajuvi wa kila jambo chini ya jua hili, naomba mwenye kujua ABCD kuwa nitakapofika nipate vipi channel ya kufanya kazi yoyote.

Nipo tayari kufanya kazi yoyote hata kama ni kukatia ng'ombe nyasi za kuwalisha, kusambaza magazeti, kuosha magari au kufanya usafi. Muhimu iwe ni kazi halali na iniingizie kipato. Angalau kwa mwezi niweze kutengeneza SEK 10,000.

Nitakuwa kwenye mji unaoitwa "Umea". Chuo nachoenda ni "Umea University ".

Sihitaji professional works hivyo naomba nisiulizwe mimi ni mtaalamu wa mambo yapi.

Mwenye ushauri wa kwamba, niachane na masuala ya kuulizia kazi na nikazingatie tu masomo naomba ushauri huo auache kwanza kwa sasa, awape nafasi wadau wenye connection ya kazi kwanza.

................ . UPDATES................

Wakuu, nashukuru sana kwa wanaoendelea kutoa ushauri kuhusu mada yangu, ila kwa uchunguzi mdogo nilioufanya, inaonesha wadau huko Sweden wapo wengi na wanajuwa connections za hapa na pale kulingana na uhitaji wangu. Ila wana hofu kubwa ya kumkaribisha mtu na akawa mzigo kwake. Wanaona wakishatoa msaada basi itakuwa juu yao kuwa responsible kwa wanaye msaidia. Wengine wana hofu na kudhani huenda suala la shule ni geresha tu na nataka kuzamia kama wazamiaji wengine.

Kwa muktadha huo, naomba kuthibitisha kuwa mie siyo mzamiaji bali naenda kimasomo. Na sitohitaji kukaa/kuishi kwa mtu, na ikiwezekana sitolazimika kuonana na atakayenipa connection. Muhimu tu ni kupata connection na kujuwa kazi zipi zitapatikana na nitazipataje. Ikumbukwe sitohitaji Professional works kutokana na usumbufu wa kuzipata. Nahitaji non-skilled jobs. Karibuni kwa ushauri Mkuu.
Wakuu, nashukuru sana kwa wanaoendelea kutoa ushauri kuhusu mada yangu, ila kwa uchunguzi mdogo nilioufanya, inaonesha wadau huko Sweden wapo wengi na wanajuwa connections za hapa na pale kulingana na uhitaji wangu. Ila wana hofu kubwa ya kumkaribisha mtu na akawa mzigo kwake. Wanaona wakishatoa msaada basi itakuwa juu yao kuwa responsible kwa wanaye msaidia. Wengine wana hofu na kudhani huenda suala la shule ni geresha tu na nataka kuzamia kama wazamiaji wengine.

Kwa muktadha huo, naomba kuthibitisha kuwa mie siyo mzamiaji bali naenda kimasomo. Na sitohitaji kukaa/kuishi kwa mtu, na ikiwezekana sitolazimika kuonana na atakayenipa connection. Muhimu tu ni kupata connection na kujuwa kazi zipi zitapatikana na nitazipataje. Ikumbukwe sitohitaji Professional works kutokana na usumbufu wa kuzipata. Nahitaji non-skilled jobs. Karibuni kwa ushauri Wakuu.
 
Mkuu, wewe unaenda kama Mwanafunzi hauna Haja ya ku panic Wala Nini. Kila kitu ukifika kule kitaa kaa sawa. Kama vipi unaweza kuwasiliana na International office ya Chuo chako. Hakika watakusaidia.

Pia Kama mwanafunzi utahitaji kufanya Kazi masaa 20 tu kwa wiki, na kipindi Cha summer so wewe ukiingia kule utapata vibali kila kitu halafu utachagua Kazi ipi ufanye. Wewe jua Ukiingia Sweden utakuwa na uhakika wa Kazi.

Cha msingi jipange na Safari tuu. Mambo mengine utayakuta huko huko.
 
Mkuu, wewe unaenda kama Mwanafunzi hauna Haja ya ku panic Wala Nini. Kila kitu ukifika kule kitaa kaa sawa. Kama vipi unaweza kuwasiliana na International office ya Chuo chako. Hakika watakusaidia.

Pia Kama mwanafunzi utahitaji kufanya Kazi masaa 20 tu kwa wiki, na kipindi Cha summer so wewe ukiingia kule utapata vibali kila kitu halafu utachagua Kazi ipi ufanye. Wewe jua Ukiingia Sweden utakuwa na uhakika wa Kazi.

Cha msingi jipange na Safari tuu. Mambo mengine utayakuta huko huko.
Nashukuru sana Mkuu. Naendelea kufumbuka zaidi..
 
Vizuri, ila international office itakupa taarifa zote kuhusu suala la kupata Kazi. Wasiliana nao. Wao watakupa mwongozo Mzuri.
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom