Biashara ya samaki

Majigo

JF-Expert Member
Feb 23, 2012
5,519
1,825
thumb-1920-355173.jpg


Wakuu kwa mtu yeyote mwenye ujuzi kuhusu biashara hii hasa samaki wa maji baridi huko Dodoma.

Soko lake vipi lina upinzani mkubwa?

Mimi niko Mbeya. Nawasilisha kwa salamu na shukrani kwenu!


WADAU WENGINE WANAOHITAJI KUJUA KUHUSU BIASHARA HII
Salamu wana JF.

Nimepata mchongo, kuna mtu toka nchi za northern Africa anataka nifanye nae biashara ya samaki. Yaani namtumia samaki toka huku TZ kwa ndege.

Swali langu ni je, kama unataka ku-export samaki ni vibali gani vinatakiwa? Je unaweza ku-export kama individual bila kuwa na kampuni hasa kwa kuanzia?

Kama kuna mzoefu naomba anisaidie.

Pia kama kuna mtu anazo samaki toka lake victoria tunaweza kuongea jinsi ya kufanya hii biashara.

Asanteni sana
Wakuu,
Kwa wale wataalam wa biashara ya samaki wabichi naomba mwongozo wenu wa namna ya kuendesha hiyo biashara.
  1. Ni kiasi gani cha mtaji kinahitajika?
  2. Ni wapi ambapo soko ni zuri kwa biashara hizi?
  3. Kuna tofauti yoyote ya biashara hizo za samaki wabichi kutegemeaa na maeneo ya bishara?
  4. Mambo gani ya muhimu nahitajika kuzingatia?
Naombeni maoni na ushauri pia.
Asanteni.
Team Watafutaji
Kama title inavyosema hapo juu, naomba kufahamu hii biashara kwa undani kidogo, yaani recently tuliambiwa kuwa kwa kipindi hiki cha miaka mitano samaki wetu wameongezeka urefu/ukubwa.

Sasa basi nikawa interested kufahamu kama mtu anaweza kununua samaki (Sato/Sangara) kutoka kwa Wavuvi in bulk na kuziuza kwa makampuni ambayo tumeambiwa wanasafirisha kwenda nje ya nchi moja kwa moja.

Au kuanza kuvua na kuuza moja kwa moja kwa haya makampuni badala ya kununua kama middleman.

Moja, je ni changamoto gani kubwa zipo kwenye hii sekta?

Pili, upatikanaji wa vibali ukoje!?

Tatu, je hivi viwanda vinanunua hao samaki kwa mfumo gani? Cash on delivery au on credit?

Nne, je mtu anaweza kuingia mkataba na hivi viwanda ili kuwa-supply mzigo?

Tano, ni fursa gani (fursa ndani ya fursa) zinaweza kupatikana kwenye hii biashara?

Sita, modality yao (kama ipo), ipoje? Je wanaweza kukudhamini vifaa ili mzigo uwapelekee wao na kukatana kidogo kidogo?

Saba, ni viwanda (kwa majina) vipo kati ya Mwanza, Bukoba na Musoma au around maeneo hayo ambao wanaweza kupokea mzigo?

Nane, je upatikanaji wa samaki una msimu? High season na low seasons?

Maswali yangu hayajakaa kwa mtiririko maalum hivyo tusaidiane tu kadiri tutakavyoona inafaa.

Kwa hili tutaweza kusaidiana na kuwasaidia vijana wetu/wenzetu pia

MICHANGO YA WADAU KUHUSU BIASHARA YA SAMAKI
MAMBO 3 UNAYOHITAJI KUFAHAMU KATIKA BIASHARA

Mkuu katika uanzishaji wa biashara kuna vitu vi3 vya msingi unatakiwa kuvijua au kuwa navyo
1. Capital
2. Market
3. Knowledge

Capital: Ya kuanzisha Bucha/Samaki unahitaji kuwa na Fremu ya kisasa yenye A/C,Mashine ya Kukata Nyama(Unaweza kununua sido) hapo Vifaa A/C+Mashine+Fremu(kodi 6months) unahitaji si chini ya 1.2m,Mtaji wa kilo 500 nyama sh 2.3m,mtaji wa samaki kilo 100,Sh 500,000/=,Deepfreezer kubwa 400,000/=,Stand za vyuma pamoja na Hooks 100,000/=,Grand Total~4.5m

Market: Inabidi butcher lako litageti soko la mama ntilie/wauza chips na makazi ya watu,mama ntilie ndio wanunuaji wakubwa wa nyama kwani wanapika Supu na pili mboga kwa wateja,wauza chips stake wanatengenezea mshikaki!

Knowledge: Mkuu hapa inabidi uwe unaamka saa 3 kwenda kufata nyama au uwe unaagiza kwenye vigari vile special kwa ajili ya kubebea nyama,saa kumi na 1 alfajiri uwe upo buchani unaanza kuuza,uhifadhi wa samaki na nyama inayolala unabidi uhuzingatie,Nyama kilo moja ni kuanzia 6000 hadi 7000 na samaki sato kilo 8000 hadi 9000 wakati sangala 7000 hadi 8000.

Kazi ni kwako mkuu.
NI WAZO ZURI, SONGA MBELE
Ni wazo zuri mkuu songa mbele. Ila jitahidi ujue ni samaki ya aina gani utakuwa unapeleka kutoka Mwanza kwa sababu samaki aina ya sangara ni bei kubwa sana mwanza kwa sababu ya kuwepo kwa viwanda, so wasi wasi wangu usije ukawanunua then ukienda kuuza wananchi wako wakaona ni bei kubwa. Jaribu kuangalia samaki aina ya sato na wengine ila sangala fikiria mala mbili kabla ya kuuza.

Kama utakuwa unanunua Mwanza tafuta ofisi weke frige na kuwa unakusanyia mzigo hapo hata kwa muda mfupi. Jambo lingine jitahidi kujiridhisha na usafiri wa kudumu. Haya malori hayafai kabisa yameisha tia watu hasara. hata samaki wakiwa wamekaushwa gari ikiharibika usababisha hasara sana. Ila hizo ni changamoto ambazo ukizijua mapema ni vyema kuzitafutia ufumbuzi haraka.

Kama utapata soko zuri za sangala uko arusha, kumbuka sangala mwanza anakuwa na thamani kwa vitu vikuu viwili.

Kwanza mnofu kwenye viwanda na pili ndani ya sangala tumboni kuna kitu wanaita bondo sijajua kama ni kiswahili au la ila nimezoea kusikia wanaita hivyo, hii kitu ni hela sana kwa sangala alie mkubwa. watu wa Arusha usiwauzie na hilo bondo litoe na ukaliuze Mwanza kwa Wachina hela nzuri.

Nahisi usingize ngoja nilale nitakupa data kesho tena.
PACKAGE NZURI NA MTINDO WA DELIVERY NI MUHIMU
Wazo zuri ndugu, kama walivyopita washauri wengine. Kwanza unatakiwa utembelee eneo husika na kuangalia uhitaji gharama za usambazaji, pia kwa ushauri wangu kwa kuwa arusha ni jiji kubwa package yako na deliver transit inabidi iendane na mandhari ya sehemu unayopeleka, e.g serena hotel uki delivery kwa head hiyo ni soo. Usafi ni kitu muhimu katika biashara ya chakula. ili ufanye biashara yenye tija obseve this.

1. Tafuta sare yako ili uonekane uko serious na kazi yako
2. Kama una usafiri hata (pikipiki yenye refrigerator) kwa ajiri ya ku distribute orders
3. Kumbuka utahitaji watu wa kukusaidia ili kuendana na mda wa order husika
4. Je, utakuwa unauza kwa jumla au reja reja

All the best.
UTOFAUTI WA SANGARA NA SATO
Bei ya sangara na sato inatofautiana. Sato siku zote iko juu. Kwenye kipindi cha mvua samaki wanapatikana wengi na kwa Bei nafuu. Kipindi hiki samaki sangara kilo kwa jumla ni 4500. Wakati sato anaenda mpaka 5500.

Samaki wanapimwa kwa kilo. Unaweza kununua moja kwa moja kutoka kwa wenye mitumbwi yao au kutoka kwa walanguzi ambao wao huzinunua kwa wingi na kuzihifadhi Kwenye mafriza baada ya kuwatoa mautumbo na mabondo.

Hawa walanguzi ndiyo wenye Bei niliyokupa hapo juu. (Ukumbuke Bei hubadilika ) walanguzi hawahawa ukitaka samaki wanakufungia vizuri na kuwapakiza Kwenye mafuso. Fuso zote zinapakulia pale urafiki freti. Ila unalipia usafiri mwenyewe.

Kuhusu kibali mlanguzi huwa anakibali na mwenye fuso anakibali cha usafirishaji. Na ushuru utalipwa na mlanguzi. (Ukitaka namba ya mlanguzi utaniambia).

Bei ya kuuza huku samaki mbichi kilo ni kuanzia elf 8-10.

Of course ukitaka kuwa na frem lazima uwe na leseni nenda halmashauri na tra lazima ikuhusu.

Ukitaka nafuu sambazia mzigo ukiwa home kwako.
UZOEFU KATIKA UVUAJI NA UUZAJI WA SAMAKI

Mimi Nimevua SANGARA ziwa Victoria, Sato tulikuwa tukiwakamata mara chache kwasababu tulikuwa tuna vua maji ya kina kirefu.

Mimi nimewahi kuvua ziwa Victoria kisiwa cha kome na visiwa jirani huko. Biashara ya uvuvi siyo rahisi na siyo ngumu. Urahisi wa biashara hii ikiwa wewe mwenye mtaji utaamua kuishi kambini na wavuvi wako, ukisimamia ukiwa site kabisa, yani anzisha kambi, wavuvi wengi tu, wanakuja wenyewe mnaanza kazi.

Malipo inategemea na wewe mwenyewe, unaweza kuwaliapa pesa, au ukawapa siku zao za uvuvi kama sehemu ya malipo yao. Yaani wanakuvulia Jumatatu mpaka Ijumaa, Jumamosi na Jumapili wanavua lakini nizao au ndio malipo yao, wakipata sawa wakikosa pia wanelewa. Ila gharama za kuwalisha ni zako mwenye kambi, unanunua Unga tu, samaki wanapatikana ziwani kama kitoweo.

Unaweza ukawa unauza samaki wabichi, kwa wamiliki wa viwanda au kuna wachuuzi wa wenye viwanda wanazunguka na mzani wananunua na kupeleka kiwandani, ama unaweza wachana samaki ukawatia chumvi na kuwakausha juani kule wanaitwa Kayabo, soko lao ni Zaire, na Zambia kwa sana.

Unahitaji kuwa na mitumbwi ya kuvulia kadhaa kutokana na mtaji wako na mahitaji yako, unahitaji kuwa na Injini za boti atleast Mbili. Kwasababu unahitaji pia kufanya doria ya nyavu zako, wavuvi ni wezi kama ilivyo kwa sehemu zingine, kama huna speed bot na hufanyi doria, hao hao wavuvi wako wanongea na wenzao wa maeneo mengine wanakuja kukuibia nyavu zote.Lakini wakijua una speed boti na unafanya doria pia umiliki bunduki wataogopa. Nimefanya kazi hizo za usimamizi miaka mingi kidogo imepita lakini huo ni uzoefu nilio upata huko.

Najua uzi huu labda ume expire lakini niliona ni shere labda uhitaji bado upo.

Naomba kuwasilisha.

 
Inalipa sana inategemea unawatoa wapi? Kama ni mtera inakuwa poa sana hata bei yake inalipa kiasi.
 
Inalipa sana inategemea unawatoa wapi? Kama ni mtera inakuwa poa sana hata bei yake inalipa kiasi.

Nashukuru Sana Mkuu
Mimi Nimepanga Kuwatoa Ziwa Nyasa(mbeya)
Sababu Ndiko Niliko
Ila Kama Ulivyosema Mtera,itabidi Niangalie Inakuwaje!
 
Nashukuru Sana Mkuu
Mimi Nimepanga Kuwatoa Ziwa Nyasa(mbeya)
Sababu Ndiko Niliko
Ila Kama Ulivyosema Mtera,itabidi Niangalie Inakuwaje!

Mkuu watu wa Mbeya, Njombe na Ruvuma wako wengi tu DAR na wengine tumeoa huko na tungependa sana kupata samaki toka Ziwa Nyasa. Binafsi sijawahi kuona au sijuwi sehemu yeyote DAR panapouzwa samaki toka ziwa Nyasa kama vile Mbasa, mbelele n.k bila kuwasahau dagaa wake watamu. Nafikiri kwa DAR inaweza kulipa zaidi maana hata access yake ni rahisi kuliko DOM.
 
Mkuu watu wa Mbeya, Njombe na Ruvuma wako wengi tu DAR na wengine tumeoa huko na tungependa sana kupata samaki toka Ziwa Nyasa. Binafsi sijawahi kuona au sijuwi sehemu yeyote DAR panapouzwa samaki toka ziwa Nyasa kama vile Mbasa, mbelele n.k bila kuwasahau dagaa wake watamu. Nafikiri kwa DAR inaweza kulipa zaidi maana hata access yake ni rahisi kuliko DOM.

Mkuu Nimekupata Sana Sikulijua Hilo

Kiukweli Samaki Hawa Ni Wazuri Ila Changamoto Ni Uhifadhi Mpaka Ziweze Kufika DAR
shukran Sana Mkuu

Tafadhari Naomba Mawasiliano Yako

Vilevile Kama Kuna Mtu Anajua Soko La Samaki Hawa Kwa Hapo DAR kama Lipo,nahitaji Mchango Wenu!
 
Mkuu Nimekupata Sana Sikulijua Hilo
Kiukweli Samaki Hawa Ni Wazuri Ila Changamoto Ni Uhifadhi Mpaka Ziweze Kufika DAR
shukran Sana Mkuu
Tafadhari Naomba Mawasiliano Yako

Vilevile Kama Kuna Mtu Anajua Soko La Samaki Hawa Kwa Hapo DAR kama Lipo,nahitaji Mchango Wenu!

Mkuu ushauri wangu ni kuwa unaweza kufika DAR ukajaribu kuzunguka kwenye mabucha/maduka ya kuuza samaki. Ongea nao wewe waweza kuwa supplier wao tu. Kama una mpango wa kufungua duka lako mwenyewe basi inabidi ujuwe sehemu ambayo idadi ya wakazi wa Songea/Mbeya ni kubwa ili uweze kupata wateja kwa haraka.

Wazoefu wa DAR wanaweza kutuambia hapa maana DAR imegawanyika japo si mgawanyo rasmi. Kwamfano ukitaka wachaga wengi utawapata Kimara, Wakurya utawapata Kipunguni na Kitunda, wasukuma utawapata Vingunguti na Kigamboni. Japo najua watu wa Songea unaweza kuwapa kwa wingi Mabibo huenda kuna sehemu nyingine waliko wengi zaidi.

Biashara ikishakuwa unaweza sasa kufungua matawi sehemu zingine. Soko ni kubwa tu na familia yangu tutakuwa wateja wako wa kudumu.
 
Mkuu ushauri wangu ni kuwa unaweza kufika DAR ukajaribu kuzunguka kwenye mabucha/maduka ya kuuza samaki. Ongea nao wewe waweza kuwa supplier wao tu. Kama una mpango wa kufungua duka lako mwenyewe basi inabidi ujuwe sehemu ambayo idadi ya wakazi wa Songea/Mbeya ni kubwa ili uweze kupata wateja kwa haraka.

Wazoefu wa DAR wanaweza kutuambia hapa maana DAR imegawanyika japo si mgawanyo rasmi. Kwamfano ukitaka wachaga wengi utawapata Kimara, Wakurya utawapata Kipunguni na Kitunda, wasukuma utawapata Vingunguti na Kigamboni. Japo najua watu wa Songea unaweza kuwapa kwa wingi Mabibo huenda kuna sehemu nyingine waliko wengi zaidi.

Biashara ikishakuwa unaweza sasa kufungua matawi sehemu zingine. Soko ni kubwa tu na familia yangu tutakuwa wateja wako wa kudumu.

Shukrani sana mkuu kwa kunipa Mori Na Ushauri Makini,nitayafanyia Kazi!

Nafikiria Namna Ya Kuwahifadhi Samaki Mpaka Kufika Kwenye hzo Bucha Kubwa Bila Kupoteza Ubora Wake.

Sababu Barafu Sijazipa % kutokana Na Changamoto Za Usafiri!
 
Wakuu,
Kwa wale wataalam wa biashara ya samaki wabichi naomba mwongozo wenu wa namna ya kuendesha hiyo biashara.
  1. Ni kiasi gani cha mtaji kinahitajika?
  2. Ni wapi ambapo soko ni zuri kwa biashara hizi?
  3. Kuna tofauti yoyote ya biashara hizo za samaki wabichi kutegemeaa na maeneo ya bishara?
  4. Mambo gani ya muhimu nahitajika kuzingatia?
Naombeni maoni na ushauri pia.
Asanteni.
 
Mkuu unalitumia vizuri jamvi, kila la heri mkuu katika mipango yako ya kujitanua kibiashara!
 
Mkuu ungefunguka wanauwa nje ya Nchi wapi? Ulaya au Uganda, Kenya, ninavyo jua wana uzwa Ulaya ni waleSangara na huwa wamekwisha procesisia tiyali, jena wewe una process?
 
Greetings! Shikamoo! Habari zenu wanajamii!
Mimi nipo Bukoba najihusisha na biashara ya samaki. Kwa hivi sasa nahitaji business partner. Samaki wanauzwa nje ya nchi. Details zaidi ni kwa wale wako interested only. Mtaji ni Tshmil 4 kuendelea.

Samaki wa aina gani? Sato au Sangara.
 
Mkuu ungefunguka wanauwa nje ya Nchi wapi? Ulaya au Uganda, Kenya, ninavyo jua wana uzwa Ulaya ni waleSangara na huwa wamekwisha procesisia tiyali, jena wewe una process?

Samaki wa aina gani? Sato au Sangara.

May be kwa sababu amesema waliokuwa interested wamtafute,labda anataka tupige naye story za chemba ndio atafungukia huko.Si mnaona amepost tu kisha akatokomea kizani.Na hii inanitia hofu ikiwa kweli yuko serious kweli.
 
Hizi taarifa Mh!

scam@work!

siku hizi nasikia bukoba kuwa matapeli wengi sana sijui kwa nini? wadau kuwa makini!
 
Greetings! Shikamoo! Habari zenu wanajamii!
Mimi nipo Bukoba najihusisha na biashara ya samaki. Kwa hivi sasa nahitaji business partner. Samaki wanauzwa nje ya nchi. Details zaidi ni kwa wale wako interested only. Mtaji ni Tshmil 4 kuendelea.
Greetings!

Nauza set nzima ya star times decoder, aerial na cable yake ya 20m. Price 80,000. Haina matatizo yeyote. Nipo Dar es salaam. Asante.
wajingawatu upo arusha? Ni PM nina biashara
Tunakodisha machine ya hydraform ya kutengeneza matofali kwa kutumia udongo. Pia tunaye mtaalam wa kuyatengeneza kama utamhitaji.

Ona post za huyo mjasiriamali!
 
Kijana anatafuta mtaji, yawezekana anayo idea nzuri ya biashara ila mtaji ndo unagomba.
 
  • Thanks
Reactions: amu
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom