Biashara ya Michezo ya Video (Video Games): Jifunze Uendeshaji, Changamoto na Faida Zake

Wenye fundo za roho wako hata ulaya. Muhimu angalia wanakubania wapi halafu uhakikishe unawakabia hapo hapo.
 
Video games zinafaida kwa akili, kwani nchi zilizoendelea mpaka wagonjwa wanashauriwa kuzicheza kwa ajili ya ubongo kuweza ku-charge zaidi kwa kufikiria kwa haraka, kufanya co-ordination kwenye mikono na pia kupunguza stress na depression, na sio kwa watoto tu. mimi nimekuwa nikifanya hii biashara kwa muda sasa, na nimekuwa nikifuatilia wanafunzi ambao wanakuja kucheza, matokeo yao shule vipi?

Wengi wao ni wenye kufaulu mitihani, na kama alikuwa anafeli matokeo ya mbele yanakuwa mazuri baada ya kucheza. Hatuwezi kuzuia maendeleo ya kidunia na technologia, na watoto wa siku hizi hawana michezo mingi nje kama zamani.

Ni kitu kigeni na mara nyingi kipya kinaonekana sio kizuri haswa kwa wasio fahamu. Upande wa tabia ya utoro na wizi, nasema, mtoto umleavyo ndio akuavyo. Matajiri wengi tu, wamewanunulia watoto wao hizi game kucheza nyumbani na wako vizuri tu kielimu, ni sisi walala hao ndio tunapigana wetu wasijue kitu, technologia hizi zipo, na zitaendelea kuboreshwa. mengine baadaye, hayo tu kwa sasa.
 
Gomba siwezi, ni heri nifanye biashara ya halali, mtaji wa million moja unaweza ukakamatwa siku hiyo hiyo, sitaki presha.
 
Hamia Mwanza. Nadhani kwa biashara kama hiyo inalipa zaidi ya Arusha.
 
Wivu na umaskini ni kama baridi kali na barafu vinaenda pamoja. Jibu si kukimbia bali kukaa mbali na wenye green mara nyingi huwa ni watu karibu sana na wewe.
 
Mie nikifuatilia sana malezo yako hapo juu inaonekana wewe ndio una matatizo nani muoga wa maisha. Huwezi kuwapangia mafundi Garage kwa Play station yako wewe, na huwezi kuchukiwa na wapangi wooote bila kuwa na matatizo.

Na inaonekana wewe ni mlalamikaji sana kuliko kupambana na changamoto hizo za majukum ya kazi yako. Hakuna sehem rahisi, we nenda hata wapi hali ni kama hiyo na zaidi ya hiyo.

Wapangaji unawachukia na kusema wanakuchukia,mafundi gereji nao unasema wanakubania,sasa inamaana wote hao ni wabaya ila wewe peke yako ndio mzuri.

Na mie nakushauri ni bora ukae huko huko,ukija jiji la Dar ndio huwezi kabisaaa,maana Dar watu hakuna kulalamika hovyo, huku ni kupambana tu linavyokuja ndio unaendanalo,unalala leo kesho hujui itakuwaje watu wanakomaa na siku zinakwenda.

Una kodi mlango leo kesho nyumba inauzwa,unalipa kodi leo kesho inapanda, ila watu wanakomaa,sasa wewe kesi ndogo hizo unapiga mikelelee.

Sasa kama ilikuwa biashara hiyo inalipa kwanini usinunue meter yako binafsi ya umeme wa biashara.Tatizo ni kwamba watu wengi wakifanikiwa kwenye biashara wao ni starehe na kuhonga tuu,sasa ikianza kwenda hovyo ndio kutafuta nani mchawi.

Wakati inalipa ilitakiwa uwe na akili ya kuanzisha kitu kingine zaidi ya kutegemea hiyo biashara,we huwezi kuomba ushauri wa kuhama mkoa ili ukaanzishe biashara hiyo mkoa mwingine eti kisa kuna watu wanasema nini sijui nini.

Ungekuwa ni jinsia ya kike ningesema sawa,ila wewe mwanaume unaogopa na kukimbia changamoto za kitoto namna hiyo.

Uliza humu watu wanavyokumbana na changamoto za biashara, kichwa kitakuuma, hiyo yako ni issue ya kitoto sana.
Jipange maisha sio lelemama wala kulalamika, kama ulitumia fursa vibaya mwisho wake huwa ni malalamiko kama haya.
 
Sikuelewi, Zanzibar Spices, labda hauelewi vizuri mada yangu. Biashara nimefanya siku nyingi sawa, nilipo aanza eneo lilikuwa hakuna biashara, lakini pole pole kumechangamka na sasa maduka ya spare yamefurika, sina shida na mwenye kutafuta riziki, lakini isiwe unakuja mlangoni kwangu na kufanya biashara yako kwa kunifungia mlango wangu na magari mabovu au kutukanana, watoto wanaocheza ndani wanasikia, sio tabia njema kuwafundisha lugha chafu.

Wapangaji nao wana wivu, nawajua mimi ninaiishi nao, kwani mtu unatumia friji mbili, heater ya maji pasi na kadhalika vya umeme kila siku aning'anienie mimi nilipe sawa naye na nina washa tv na game (sawa na dvd player), ikifika zamu yao kununua luku wanachelewesha haswa watoto wakiwa wengi, na mengine mengi tu unasema eti nalalamika, sawa, ni maoni yako.

Kuhusu kununua mita ya luku nilifuatilia lakini kwa majukumu niliokuwa nayo na faida ya biashara ni bora kutumia mita hiyo hiyo. Mimi nimeomba maoni kuona kama je itakuwa bora kuja dar? Maana huku watu sio wengi kama dar na uzuri wa dar kila mtu na issue zake, arusha watu wanatabia ya kuharibiana sana ni wachache sana watakusaidia kimaendeleo.

Hapa hamna jambo la kitoto, kama wewe unayaweza sawa, lakini wengine ni msaada wa kimawazo tunatafuta.
 
Huitaji kuja Dar, asili ya biashara yako ni popote penye watoto. Toa hiyo picha kwamba arusha hapalipi na ukabiliane na matatizo yako.

Nakishauri tafuta goli lingine hukohuko Arusha, ambalo halina usumbufu kama unaoupata sasa.asili ya biashara yako inalipa, usikate tamaa.

Quiters never win and winners never quit.
 
Tatizo sio Arusha, tatizo ni mahalh ilipo biashara yako, kwani Arusha yote kuna changamoto hizo hizo?

Katika wachangiaji wote, Mkuu umetoa wazo zuri la kutafuta location nyingine ya biashara yake badala ya kuhama Mkoa, kwa kutumia vigezo ambazo alivitumia mwanzoni vya kuanzisha biashara kwenye eneo husika atumie pia kutafuta eneo jingine.
 
Kweli mahali nilipo mabadiliko naona wakati wake umefika, kwa arusha kuna maeneo mengine, lakini kutokana kupanda bei za tanesco, arusha hailipi sana, kwa sasa ninalipisha 500 kwa nusu saa, compare na Dar, ambapo kuna sehemu nyingi tu, wanalipisha 500 kwa mechi moja ya mpira ambayo ni ya dakika 10 au 16 hivi kama sikosei.

Mahesabu haya ndio naona inalipa zaidi Dar, Arusha maisha ni gharama sana na watu ni wachache wenye uwezo wa kuwapa watoto pesa. Nashukuru kwa maoni yote, je kwani Dar si kuna sehemu zenye wakazi wengi zaidi, ni sehemu zipi na kodi ya kupanga je inakuwaje, naomba muendelee kunipa ushauri na maoni, hapa JF nimepakubali.

Pia niko tayari kuingia patnership na mtu wa Dar ambaye ana interest na hii michezo na aliyekuwa na location available, games na tv ninazo za kutosha.
 
Video games zinafaida kwa akili, kwani nchi zilizoendelea mpaka wagonjwa wanashauriwa kuzicheza kwa ajili ya ubongo kuweza ku-charge zaidi kwa kufikiria kwa haraka, kufanya co-ordination kwenye mikono na pia kupunguza stress na depression, na sio kwa watoto tu. mimi nimekuwa nikifanya hii biashara kwa muda sasa, na nimekuwa nikifuatilia wanafunzi ambao wanakuja kucheza, matokeo yao shule vipi?

Wengi wao ni wenye kufaulu mitihani, na kama alikuwa anafeli matokeo ya mbele yanakuwa mazuri baada ya kucheza. Hatuwezi kuzuia maendeleo ya kidunia na technologia, na watoto wa siku hizi hawana michezo mingi nje kama zamani.

Ni kitu kigeni na mara nyingi kipya kinaonekana sio kizuri haswa kwa wasio fahamu. Upande wa tabia ya utoro na wizi, nasema, mtoto umleavyo ndio akuavyo. Matajiri wengi tu, wamewanunulia watoto wao hizi game kucheza nyumbani na wako vizuri tu kielimu, ni sisi walala hao ndio tunapigana wetu wasijue kitu, technologia hizi zipo, na zitaendelea kuboreshwa. mengine baadaye, hayo tu kwa sasa.

Umejibu vizuri mkuu kwa mtu yeyote mwenye akili timamu kukuelewa.
 
Kweli mahali nilipo mabadiliko naona wakati wake umefika, kwa arusha kuna maeneo mengine, lakini kutokana kupanda bei za tanesco, arusha hailipi sana, kwa sasa ninalipisha 500 kwa nusu saa, compare na dar, ambapo kuna sehemu nyingi tu, wanalipisha 500 kwa mechi moja ya mpira ambayo ni ya dakika 10 au 16 hivi kama sikosei. Mahesabu haya ndio naona inalipa zaidi dar, arusha maisha ni gharama sana na watu ni wachache wenye uwezo wa kuwapa watoto pesa.

ashukuru kwa maoni yote, je kwani dar si kuna sehemu zenye wakazi wengi zaidi, ni sehemu zipi na kodi ya kupanga je inakuwaje, naomba muendelee kunipa ushauri na maoni, hapa JF nimepakubali.

Pia niko tayari kuingia patnership na mtu wa dar ambaye ana interest na hii michezo na aliyekuwa na location available, games na tv ninazo za kutosha.

Vipi kama utapata kifaa ambacho kitakusaidia ku connect vifaa vyako vyote bila kuhusisha matumizi ya umeme wa TANESCO ili kuendeleza biashara yako Arusha! Au umeamua kubadili location?

Hata ukihamia Dar, kama bado utahitaji ili kuepukana na usumbufu wa TANESCO twaweza kuwasiliana mkuu ili biashara yako isonge mbele bila manung'uniko.

To every problem there is a solution, if there is no solution,then there is no problem.
 
Kama kuna kifaa, nijuze, maana ndio maendeleo. Natumai kifaa chenyewe sio generator, hebu nieleweshe nifanyaje?
 
Kama kuna kifaa, nijuze, maana ndio maendeleo. Natumai kifaa chenyewe sio generator, hebu nieleweshe nifanyaje?

Unaweza kutumia kifaa kinaitwa Power inverter. Unatumia battery ya gari 12vDC au 24vDC na kinatoa umeme wa 240vAC kama unaotumika majumbani.

Inategemea vitu ulivyonavyo vinatumia Watts ngapi,unaweza kuangalia matumizi ya Watts kwa kila kitu unachotaka kutumia,jumla ya watts utakazopata ndizo zitakusaidia kujua unahitaji kununua chenye watts ngapi.
Vinapishana bei kulingana na uwezo wa watts.

Mkuu ukipata hiki Utasahau kama huwa kuna shirika la TANESCO.

Kama utakuwa tayari nijulishe tufanye biashara. Unaweza connect all domestic appliances. Kazi yako itakuwa kucharge tu battery yako na kuendeleza biashara.

Ukishafanikisha mambo yako in future unaweza ukaamua kuhamia kwenye Solar ukafunga kazi kabisa na kuwasambazia hata majirani zako kwa reasonable cost.

Nitafute kwa email frajosmal@yahoo.com
 
Usikimbie changamoto pambana nazo, alafu uko Dar kunakokupa matumaini pia kuna changamoto zake biashara iyo inalipa uswazi tandale au manzese uko ila kuwa makini na iyo partnership otherwise unaweza kuibiwa kila kitu kama vipi komaa uko uko matatizo hayakimbiwi.
 
Nimeangalia, kwa ujumla vifaa vyote, yaani game consoles na tv zinatumia jumla ya 1831 watts. Je, inakuwaje kwenye hicho kifaa na ni inverter yenye ukubwa gani itafaa?
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom