Bi dentamol
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 987
- 1,912
Changamoto za ndoa, dada yupo na stress za kufa mtu.
Iko hivi, kuna hawa wanandoa wameoana wana miaka karibia 2 sasa ya ndoa yao baba mwalimu wa secondary na mama mwalimu wa primary.
Dada anadai alipoolewa walikaa baadae mwanaume akamwambia ili wae huru kufanya maendeleo ya familia yao inabidi wawajengee wazazi wake mwanaume kwanza maana walipokua wanaishi mazingira hayakua mazuri, dada kweli kapima kaona ni sawa.
Mwaka Jana kweli wakajenga nyumba kufika October jamaa akamwambia ujenzi tumemaliza inabidi tulime kijijini kwa wazazi wake ili wazazi wasitusumbue chakula.
Dada kakubali mishahara yao ikatumika katika kilimo anavyodai kipindi wanafanya hayo yote ndani hakuna kununua kitu zaidi ya chakula na kulipa kodi na vitu vidogo vidogo.
Mwaka huu baada ya kumaliza kilimo dada kamwambia mwanaume sasa tuanze na sisi kujenga tununue kiwanja mwanaume kakubali.
Akaenda kwao kusalimia alivyorudi akamwambia baba yaake kamwambia nyumba moja haitoshi watu ni wengi wanabanana na hata wenyewe wakienda kusalimia watakosa pa kulala inabidi wajenge tena nyingine kubwa.
Dada akaomba basi kabla ya ujenzi angalau wanunue kiwanja chao mwanaume akamwambia asiwe na haraka watanunua viwanja hata 10 atulie kwanza.
Dada kakubali lakini kinachomuuma yeye anapigana angalau ujenzi wa kwa wakwe uishe na yeye aanze wake, mara jamaa anapigiwa simu anatakiwa ampeleke mdogo wake shule ambae alikataa ila sasa kaona umuhimu.
Jamaa katoa gharama zote kama laki 7 hivi hapo ujenzi unasimama,
mishahara ikitoka wanaendelea tena na ujenzi pole pole wakikaa kidogo kaka yake hua anaumwa, sasa watoto wake wapo shule wamekwama kaambiwa awalipie ada inabidi ujenzi usimame tena. Sasa dada anachanganyikwa anafanya kazi haoni maendeleo, anaomba ushauri afanyeje?
Kumbuka huyo ni mume wake wa ndoa tena ya RC.
Karibuni
Iko hivi, kuna hawa wanandoa wameoana wana miaka karibia 2 sasa ya ndoa yao baba mwalimu wa secondary na mama mwalimu wa primary.
Dada anadai alipoolewa walikaa baadae mwanaume akamwambia ili wae huru kufanya maendeleo ya familia yao inabidi wawajengee wazazi wake mwanaume kwanza maana walipokua wanaishi mazingira hayakua mazuri, dada kweli kapima kaona ni sawa.
Mwaka Jana kweli wakajenga nyumba kufika October jamaa akamwambia ujenzi tumemaliza inabidi tulime kijijini kwa wazazi wake ili wazazi wasitusumbue chakula.
Dada kakubali mishahara yao ikatumika katika kilimo anavyodai kipindi wanafanya hayo yote ndani hakuna kununua kitu zaidi ya chakula na kulipa kodi na vitu vidogo vidogo.
Mwaka huu baada ya kumaliza kilimo dada kamwambia mwanaume sasa tuanze na sisi kujenga tununue kiwanja mwanaume kakubali.
Akaenda kwao kusalimia alivyorudi akamwambia baba yaake kamwambia nyumba moja haitoshi watu ni wengi wanabanana na hata wenyewe wakienda kusalimia watakosa pa kulala inabidi wajenge tena nyingine kubwa.
Dada akaomba basi kabla ya ujenzi angalau wanunue kiwanja chao mwanaume akamwambia asiwe na haraka watanunua viwanja hata 10 atulie kwanza.
Dada kakubali lakini kinachomuuma yeye anapigana angalau ujenzi wa kwa wakwe uishe na yeye aanze wake, mara jamaa anapigiwa simu anatakiwa ampeleke mdogo wake shule ambae alikataa ila sasa kaona umuhimu.
Jamaa katoa gharama zote kama laki 7 hivi hapo ujenzi unasimama,
mishahara ikitoka wanaendelea tena na ujenzi pole pole wakikaa kidogo kaka yake hua anaumwa, sasa watoto wake wapo shule wamekwama kaambiwa awalipie ada inabidi ujenzi usimame tena. Sasa dada anachanganyikwa anafanya kazi haoni maendeleo, anaomba ushauri afanyeje?
Kumbuka huyo ni mume wake wa ndoa tena ya RC.
Karibuni