Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Naona jukwaa hili linazidi kupata umaarufu. Kwa ushauri tu kuna wajasirimali wengi tu wanaokusudia kuanzisha biashara, tatizo baadhi ya bidhaa upatikanaji wake huwa mgumu na pengine gharama na matatizo ya visa huwagharimu zaidi kwa kufikiria kila mmoja ajipange kivyake.
Ushauri wangu ni bora kuwa na mshikamano kwa wafanyabiashara wadogo kadhaa kuwa katika vikundi kwa kufanya ushirikiano wa kuingiza bidhaa kwa pamoja. Tanzania ya leo si kama ya miaka 10 iliyopita, kuna wenye nafasi ya kupenda sehemu nyingi bila vikwazo, hivyo bora katika kundi kuwa na mmoja anayeaminika kuwa importer wa bidhaa. Tatizo hapa si kila mmoja wa kuaminiana, napengine ingefaa kuwa na mikataba inayowalinda wote.
Njia hii ni nzuri kwani hata mwenye mtaji mdogo hata wa 1,000,000 anaweza kupata bidhaa zake na gharama za usafirishaji kwa pamoja huwa nafuu kuliko pengi kujipanga kivyake.
Binafsi na mpango wa kuanza shughuli hii, napenda kupata vijana kadhaa ambao wana malengo kweli ya ujasirimali, ambao mitaji yao huanzia 3,000,000 and up, ambao biashara zao zinatokana na bidhaa za kutoka nje ya Tanzania. Kukusanya nguvu ya vijana kama watano hivi wa biashara ndogo kuna uwezo wa kuanza na container moja na likishafika kila mmoja anachukua chake.
Lakini lazima kuwepo na utaratibu maalumu ambao utafanywa kimkataba. Uwezo wangu wa kuleta bidhaa ni kutoka Europe na USA. Ni pendekezo kwa wadau, kwani tukiunganisha nguvu ndio kufanikiwa kwetu.
Ushauri wangu ni bora kuwa na mshikamano kwa wafanyabiashara wadogo kadhaa kuwa katika vikundi kwa kufanya ushirikiano wa kuingiza bidhaa kwa pamoja. Tanzania ya leo si kama ya miaka 10 iliyopita, kuna wenye nafasi ya kupenda sehemu nyingi bila vikwazo, hivyo bora katika kundi kuwa na mmoja anayeaminika kuwa importer wa bidhaa. Tatizo hapa si kila mmoja wa kuaminiana, napengine ingefaa kuwa na mikataba inayowalinda wote.
Njia hii ni nzuri kwani hata mwenye mtaji mdogo hata wa 1,000,000 anaweza kupata bidhaa zake na gharama za usafirishaji kwa pamoja huwa nafuu kuliko pengi kujipanga kivyake.
Binafsi na mpango wa kuanza shughuli hii, napenda kupata vijana kadhaa ambao wana malengo kweli ya ujasirimali, ambao mitaji yao huanzia 3,000,000 and up, ambao biashara zao zinatokana na bidhaa za kutoka nje ya Tanzania. Kukusanya nguvu ya vijana kama watano hivi wa biashara ndogo kuna uwezo wa kuanza na container moja na likishafika kila mmoja anachukua chake.
Lakini lazima kuwepo na utaratibu maalumu ambao utafanywa kimkataba. Uwezo wangu wa kuleta bidhaa ni kutoka Europe na USA. Ni pendekezo kwa wadau, kwani tukiunganisha nguvu ndio kufanikiwa kwetu.