Ushauri kati ya hizi gari wanajamvi

I J NJOVU

JF-Expert Member
Oct 22, 2015
3,149
10,428
Habari wanajukwaa.

Kutokana na hali ya kiuchumi kuyumba wengi tunashindwa kununua gari za gharama. Husika moja kwa moja kwenye mada nahitaji ka luxury car ya bei ya kawaida.

Nimetumia week na zaidi katika kuchagua gari ninayoitaka ila nikapendezwa na hizi gari apo chini na bei zinafanana kwa kuwa zote mbili ziko around 16mil. ningependa mnipe mwongozo Kaka zangu

BF581334_e697f6.jpg


vs
BF579889_00af54.jpg

Muumba akijalia week ijayo nilipie moja. nipeni mwongozo sijawahi kumiliki luxury car.
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Hiyo ya kwanza ni Brevis kama sija kosea, hiyo kwa mwendo iko vizuri ila kwa mafuta ni utumiaji mkubwa sana.hiyo ya pili ni mardesc compresso yenyewe pia kwa mwendo iko vizuri sana ila upande wa spea ndio iko juu kwakuwa benz ni kama nissan ni magari ambayo huwa hayaendi kwa mfumo wa kuchongesha vipuri,yenyewe yanataka kikiharibika badilisha weka kingine nalo litadumu sana.
 
Hiyo ya kwanza ni Brevis kama sija kosea, hiyo kwa mwendo iko vizuri ila kwa mafuta ni utumiaji mkubwa sana.hiyo ya pili ni mardesc compresso yenyewe pia kwa mwendo iko vizuri sana ila upande wa spea ndio iko juu kwakuwa benz ni kama nissan ni magari ambayo huwa hayaendi kwa mfumo wa kuchongesha vipuri,yenyewe yanataka kikiharibika badilisha weka kingine nalo litadumu sana.

Hiyo sio brevis ni Crown ingawa sifa zinafanana kati ya crown na brevis
 
Benz sijawahi tumia ivyo siijui kiundani. Ila ingekuwa ni mimi ningechukua benz dhidi ya crown, maana speed benz ni 220km/hr while crown ni 180km/hr, CC benz ni 1800 inaweza kuwa economy maana ni 4cylinder ila crown ni cc 2400 ambayo ni 6cylinder. Stability zinaweza kufanana maana yote n mazito ila benz ni confortable zaidi kuliko toyota
 
Hiyo ya kwanza ni Brevis kama sija kosea, hiyo kwa mwendo iko vizuri ila kwa mafuta ni utumiaji mkubwa sana.hiyo ya pili ni mardesc compresso yenyewe pia kwa mwendo iko vizuri sana ila upande wa spea ndio iko juu kwakuwa benz ni kama nissan ni magari ambayo huwa hayaendi kwa mfumo wa kuchongesha vipuri,yenyewe yanataka kikiharibika badilisha weka kingine nalo litadumu sana.
Ya kwanza me naona ni toyota crown
 
Unafananisha mlima na kichuguu?

Benz = Value for money.

Japo jiandae na bandari..
 
Chukua Compressor hiyo achana na huo uchafu wa Toyota.

Kama wewe sio lofa, yaani una ukwasi wa kuhudumia gari go for Benz. Hutajutia uamuzi wako. Lakini I insist uwe na uwezo wa kulihudumia sio unalipeleka kwenye magarage ya miembeni. Lipeleke kwa mafundi wa magari ya Ujerumani.
Kama una uwezo mzuri kifedha, go for S-Class, Hili ndio gari nampa salute Benz
 
Mm nakushauri uchukue ya kwanza ambayo ni toyota Crown Athlete.

Kwa sababu hizi, nikirejea kwenye thread yko, unadai kwamba hiyo ndio gari yako ya kwanza ya luxury.

Siku zote ukitaka uvipende vitu vizuri basi sharti udumu navyo na pia visikuchoshe na wala ww mwenyewe usivichoshe.

Pili Toyota ni rafiki wa mazingira yetu ya kiafrica, nikiwa na Maana kwmb, kwa upande wa spare zake ni reliable, service yake unaweza kuifanya kwa urahisi na pia kwa muundo wa ndani wa athlete ni mzuri Mara mia ya Benz.

Shida ya benz ni kwmb vifaa vyke kwanza ni mama mkwe, Service yke sio lelemama, ukimpata fundi wa kiaina unaweza ukajikuta umeingia loss kubwa
 
Kama wewe sio lofa, yaani una ukwasi wa kuhudumia gari go for Benz. Hutajutia uamuzi wako. Lakini I insist uwe na uwezo wa kulihudumia sio unalipeleka kwenye magarage ya miembeni. Lipeleke kwa mafundi wa magari ya Ujerumani.
Kama una uwezo mzuri kifedha, go for S-Class, Hili ndio gari nampa salute Benz
Upo Sahihi mkuu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom