Ushauri: Jinsi ya kujieleza kwenye Interview (nafasi za uuguzi)

apologize

JF-Expert Member
Jul 22, 2015
710
568
Habarini wakuu!

Kuna mdogo wangu hapa amemaliza chuo cha uuguzi (nursing) mwaka jana, ngazi ya Cheti na kupata GPA 4.5 na alikuwa anategemea kupata ajira mwaka huu (ambazo serikali hutoa kwa kuwapangia vituo vya kazi)

Alijaribu kutuma maombi sehemu mbalimbali katika hospitali binafsi na za serikali.

Sasa leo kapigiwa simu kutoka hospitali moja kubwa sana hapa Tanzania ipo Dar es Salaam kuwa ijumaa anahitajika kwenye usahili (interview)

Naamini humu kuna watu wanaujuzi Sana na haya maswala ya interview kutoka kwenye hiyo kada ya afya au hata wanaotoka kada nyingine wanaweza kutusaidia ni vitu gani muhimu ambavyo huwa Vinaulizwa mara kwa mara au ni maswali gani muhimu ambayo hutokea katika interview kutokana na uzoefu wenu

NB:
Kwa sasa hivi anafanya kazi (temporary na hana mkataba wowote pale) katika zahanati moja hapa jijini

Nawasilisha
 
Ataulizwa kama alivyo somea pia nursing n kama customer care ivyo ajue matumizi ya lugha vizuri
 
Back
Top Bottom