KAMA Rais anawaagiza returning officers wa Tume ya Uchaguzi NEC (maDED) kuwa asisikie DED anamtangaza mpinzani kashinda kwa vile anamlipa mshahara, anampa ulinzi na gari juu.
KAMA viongozi wa CCM wakiwemo wabunge wanawaagiza wafuasi wa CCM kuwafuata wapinzani kuwapiga na kuwakata mapanga huku wakisema polisi ni yao na mahakama ni yao tena mbele ya polisi bila kuchukuliwa hatua zozote.
KAMA polisi anatumika kumpiga na kumbruta nje ya chumba cha kuhesabia kura wakala wa Chadema ili abaki wakala wa CCM pekee.
Na KAMA matokeo yanatangazwa kwa kutumia hesabu zao wanazozipanga wenyewe pamoja na dosari zote kuripotiwa bado NEC inabariki.
Kuna haja gani ya kusumbua wanachama na mashabiki wenu kufanya kampeni huku mkijua hata mshinde hamtatangazwa washindi?
Kuna chaguzi ndogo zinakuja za Wabunge majimbo ya Longido, Singida Magharibi na Songea Mjini, najua kabla kutakuwa na mikutano kati yenu na NEC, wapinzani (CHADEMA) waje na RESOLUTION moja ya kuwakataa maDED kuwa returning officers huku mkijenga hoja yenu kutokana na kauli ya rais.
IWAPO NEC itakataa ushauri huo, kuliko kupeleka watu wakavunjwe miguu na polisi, wakadhalilishwe pengine kuuawa. Mimi nashauri huku nikijua kabisa faida na hasara za kususia uchaguzi, tumejifunza kwa CUF ya Maalimu Seif na juzi tumejifunza kwa NASA ya Raila Odinga, bora mjitoe kwenye uchaguzi huu, ili muanze mikakati mipya ya kujifunza mbinu mbalimbali za kukabiliana na matukio hayo mapema kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2019.
Mengi yatasemwa, ila najua watu watawaelewa kuwa mmeepusha maafa kama yaliyotokea kwenye uchaguzi uliopita wa Madiwani, na vile vile mtakuwa mmepeleka 'clear message' kwa watawala na mataifa kuwa kinachofanyika Tanzania sio uchaguzi bali ni mfumo wa kudanganya watu na mataifa yadhani kuwa wako madarakani kihalali na wamechaguliwa na wananchi.
KAMA viongozi wa CCM wakiwemo wabunge wanawaagiza wafuasi wa CCM kuwafuata wapinzani kuwapiga na kuwakata mapanga huku wakisema polisi ni yao na mahakama ni yao tena mbele ya polisi bila kuchukuliwa hatua zozote.
KAMA polisi anatumika kumpiga na kumbruta nje ya chumba cha kuhesabia kura wakala wa Chadema ili abaki wakala wa CCM pekee.
Na KAMA matokeo yanatangazwa kwa kutumia hesabu zao wanazozipanga wenyewe pamoja na dosari zote kuripotiwa bado NEC inabariki.
Kuna haja gani ya kusumbua wanachama na mashabiki wenu kufanya kampeni huku mkijua hata mshinde hamtatangazwa washindi?
Kuna chaguzi ndogo zinakuja za Wabunge majimbo ya Longido, Singida Magharibi na Songea Mjini, najua kabla kutakuwa na mikutano kati yenu na NEC, wapinzani (CHADEMA) waje na RESOLUTION moja ya kuwakataa maDED kuwa returning officers huku mkijenga hoja yenu kutokana na kauli ya rais.
IWAPO NEC itakataa ushauri huo, kuliko kupeleka watu wakavunjwe miguu na polisi, wakadhalilishwe pengine kuuawa. Mimi nashauri huku nikijua kabisa faida na hasara za kususia uchaguzi, tumejifunza kwa CUF ya Maalimu Seif na juzi tumejifunza kwa NASA ya Raila Odinga, bora mjitoe kwenye uchaguzi huu, ili muanze mikakati mipya ya kujifunza mbinu mbalimbali za kukabiliana na matukio hayo mapema kabla ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2019.
Mengi yatasemwa, ila najua watu watawaelewa kuwa mmeepusha maafa kama yaliyotokea kwenye uchaguzi uliopita wa Madiwani, na vile vile mtakuwa mmepeleka 'clear message' kwa watawala na mataifa kuwa kinachofanyika Tanzania sio uchaguzi bali ni mfumo wa kudanganya watu na mataifa yadhani kuwa wako madarakani kihalali na wamechaguliwa na wananchi.