Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
Watanzania na watu wengine wenye mapenzi mema na nchi yetu wameguswa na mpango wa M4C (Movement for Change) uliozinduliwa na CHADEMA usiku wa tarehe 22 Machi 2012; na baadhi yao wameanza kuchangia kwa njia ya M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
Nimegundua kuwa pesa inapofika ujumbe unatumwa kwenye simu ya mtumaji kutoka kwa mtandao ulioutumia kuwa CHADEMA Arusha imepokea mchango wako. Kasoro niliyoigundua ni kuwa CHADEMA Arusha hawatumi ujumbe wowote kwa aliyewachangia ama kumshukuru au kuthibitisha kuwa nao pesa imepokelewa katika akaunti yao. Vilevile, simu zinazotumika hazipokelewi na yeyote unapojaribu kupiga ili kuhakiki.
Ushauri:
1. CHADEMA Arusha tengeneza ujumbe "default" wa kuwashukuru wanaowachangia.
2. Wajue walipo na watumie risiti zao kama itakuwa rahisi kufanya hivyo.
Swali: M4C ni kwa ajili ya Arusha tu au utafanya kazi nchi nzima?
Kwa pamoja tunaweza.
Nimegundua kuwa pesa inapofika ujumbe unatumwa kwenye simu ya mtumaji kutoka kwa mtandao ulioutumia kuwa CHADEMA Arusha imepokea mchango wako. Kasoro niliyoigundua ni kuwa CHADEMA Arusha hawatumi ujumbe wowote kwa aliyewachangia ama kumshukuru au kuthibitisha kuwa nao pesa imepokelewa katika akaunti yao. Vilevile, simu zinazotumika hazipokelewi na yeyote unapojaribu kupiga ili kuhakiki.
Ushauri:
1. CHADEMA Arusha tengeneza ujumbe "default" wa kuwashukuru wanaowachangia.
2. Wajue walipo na watumie risiti zao kama itakuwa rahisi kufanya hivyo.
Swali: M4C ni kwa ajili ya Arusha tu au utafanya kazi nchi nzima?
Kwa pamoja tunaweza.