Ushauri: CCM tafuteni mtu makini wa kupambana na Bilionea Mbowe Hai, huyu mnayemtumia sasa Ole Sabaya ni sawa na kupoteza muda wenu bure

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,221
217,188
Mtu ambaye ni kapuku , mtu ambaye imethibitika kwamba umasikini wake umepelekea hadi kufoji nyaraka za Usalama wa Taifa ili atishe watu na kuwaomba rushwa ya kujikimu , mtu ambaye imethibitishwa mbele ya wakuu wa TRA kwamba anatumia mtutu wa bunduki kuomba rushwa ndogo hadi ya mil 2 za madafu , huyu hawezi kupambana na Tajiri Mbowe hata mkimkabidhi jeshi lote la polisi .

Freeman Mbowe atadhibitiwa kisiasa na mtu mwenye hoja za kisiasa aliyejaa utajiri wa wema na roho ya kibinadamu mwenye ushawishi , Mbowe ni jabali la kisiasa la nchi hii , huyu kauli zake ndio zinazotoa mwelekeo wa nchi , Mbowe ndiye dira ya Taifa , mipango yote ya kudhibiti siasa za nchi hii inapangwa baada ya Mbowe kuzungumza , Jabali kama hili haliwezi kutishwa na kijana mdogo asiye na kitu kama huyu Sabaya , na akiendelea na siasa za kishamba kutoka kwa wanaomtuma atakuja siku moja kukutwa mlangoni kwa Mbowe kapiga goti kuomba msamaha .

Kwa ufupi sana huu ushauri ninaowapa muuzingatie , Majuto ni mjukuu
 

Attachments

  • VIDEO_ Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai ( 750 X 750 ).mp4
    5.1 MB
Ole Sabaya kwenye kikao cha juzi ndani ya chama nasikia aliwaambia wana CCM kuwa jimbo hilo ni lake 2020 sasa sijajua je asili yake ni mchaga mana kwenye jamii ninayotoka mimi kuongozwa na mtu wa kuja hilo halipo
Majimbo hayana ukabila, huyo kijana anajitutumua kipumbavu na hana haki ya kutaka kumdhalilisha kiongozi kama Mbowe, hata sie wana CCM wengine hatuungi mkono yanayofanyika Hai hivi sasa.

Kuhusu ukabila kama ni kigezo cha mtu kuishi ama kugombea sehemu, Hai haikuwa sehemu ya wachaga bali ilikuwa sehemu ya wamasai na kama ni ukabila Ole Sabaya ni Mmasai, wachaga wamekuja kuishi kama walivyohamia mkoa wa Arusha, Tanzania ni ya kila mtu.
 
Ole Sabaya kwenye kikao cha juzi ndani ya chama nasikia aliwaambia wana CCM kuwa jimbo hilo ni lake 2020 sasa sijajua je asili yake ni mchaga mana kwenye jamii ninayotoka mimi kuongozwa na mtu wa kuja hilo halipo
Aisee kama sifa ya kwanza ya mtu anayepaswa kukuongoza wewe ni lazima awe mtu wa kabila lako na anayetokea eneo hilo hilo, basi na watu wa maeneo mengine watakuwa wanafanya makosa makubwa sana.

Maana nyie wachaga kuna maeneo mengi sana nchi hii mmepewa nafasi ya udiwani na ubunge ambayo sio ya kwenu kiasili.

Na endapo kama kila mtu akiamua ku reciprocate kwa hiki unachokisema, basi hii inchi itaingia kwenye utter political chaos na hatimae kuingia kwenye civil war sababu ya kugombania maeneo.

Watu wenye akili kama zako ni cancer kwa Taifa na hamstahili kuishi. Maana uwepo wako ni hatari kwa uwepo wa wengine.
 
Kwani si Pole Pole amewapiga marufuku hawa viongozi wa mikoa na wilaya kutamani na baadae kugombea ubunge?
 
Napenda kuwahakikishia kuwa
Lema.
Msigwa
Mbowe
Mdee
Heche
Esta bulaya
Zito kabwe
Hawa wote 2020 hawatarudi bungeni lkn Sugu atapona atarudi mjengoni hao waliobaki watake wasitake bungeni hawatorudi
MARK MY WORDS
Na Mungu atujaalie uhai tu
 
Napenda kuwahakikishia kuwa
Lema.
Msigwa
Mbowe
Mdee
Heche
Esta bulaya
Zito kabwe
Hawa wote 2020 hawatarudi bungeni lkn Sugu atapona atarudi mjengoni hao waliobaki watake wasitake bungeni hawatorudi
MARK MY WORDS
Na Mungu atujaalie uhai tu
Kwa kura za wananchi watarudi bungeni,ila kama kuna mtu anampango ovu wakudhulumu haki za wananchi wasipite huyo yeye hata fika 2020
 
Majimbo hayana ukabila, huyo kijana anajitutumua kipumbavu na hana haki ya kutaka kumdhalilisha kiongozi kama Mbowe, hata sie wana CCM wengine hatuungi mkono yanayofanyika Hai hivi sasa.

Kuhusu ukabila kama ni kigezo cha mtu kuishi ama kugombea sehemu, Hai haikuwa sehemu ya wachaga bali ilikuwa sehemu ya wamasai na kama ni ukabila Ole Sabaya ni Mmasai, wachaga wamekuja kuishi kama walivyohamia mkoa wa Arusha, Tanzania ni ya kila mtu.
Nyie CCM ni nyie na kina nani? Wapi hapo pamepitishwa azimio la kutokukubaliana nae? Yaani kamisaa wenu hukubaliani nae?
 
Majimbo hayana ukabila, huyo kijana anajitutumua kipumbavu na hana haki ya kutaka kumdhalilisha kiongozi kama Mbowe, hata sie wana CCM wengine hatuungi mkono yanayofanyika Hai hivi sasa.

Kuhusu ukabila kama ni kigezo cha mtu kuishi ama kugombea sehemu, Hai haikuwa sehemu ya wachaga bali ilikuwa sehemu ya wamasai na kama ni ukabila Ole Sabaya ni Mmasai, wachaga wamekuja kuishi kama walivyohamia mkoa wa Arusha, Tanzania ni ya kila mtu.
Sabaya ni popoma na ni janga kwake na kwa wanaomtumia
 
Ushauri wako huu ni mzuri, ila kwa hali ya siasa zetu kwa sasa, kwa CCM hata likisimamishwa jiwe jiwe linapita kwasababu zisipotosha zinatosheshwa!.

Ila pia yuko dogo mmoja makini sana, ndiye anayekwenda kumpumzisha Mwenyekiti wa kudumu.
Huyo ni huyu kijana hapa

P
 
Huyu Ol naamini ni mtu mwenye akili kijiko cha chai. Hata mwenye roho mbaya lakini mwenye akili ya kawaida hawezi kufanya ujinga kama anaoufanya huyu mtu. Namshangaa zaidi aliyemweka hapo.
 
Back
Top Bottom