Ushauri: Bomoa bomoa ifanyike nchi nzima

Rebeca 83

JF-Expert Member
Jun 4, 2016
14,840
31,583
yes,hatutaki vizazi vyetu vijavyo wapitie bomoa bomoa,

sio kurudia rudia na bomoa bomoa zenu,

fanyeni once and for all,

na nyie mnaojenga mafly over ,jengeni kwa uimara hatutaki maafa,

Na pia mzingatie miundo mbinu,kuwa mji kama Dar,inakua daily,sio baada ya miaka 20 tunakosa hata pa kupumua,wala kupita,

zingazitieni expansion joint,:D:D:D:D:D:D:D:D:D:D

Mbona kwa wenzetu,hakuna kuvunjika kwa daraja,mabarabara yamejengwa tangu Enzi za mkoloni???:confused::confused::confused::confused::confused::confused:,
 
Mdada unatakiwa ujue lengo la serekali ya ccm nikuwatesa wanainchi.


Kuna watu wanajenga sasa hivi wala ata hawakatazwi na umeme wanapewa na maji wanafungiwa kodi ya jengo na ya ardhi wanalipa baada ya miaka 17 utashangaa wanabomolewa.


Tunasafari ndefu.
 
Mdada unatakiwa ujue lengo la serekali ya ccm nikuwatesa wanainchi.


Kuna watu wanajenga sasa hivi wala ata hawakatazwi na umeme wanapewa na maji wanafungiwa kodi ya jengo na ya ardhi wanalipa baada ya miaka 17 utashangaa wanabomolewa.


Tunasafari ndefu.
Usiku mwema mkuu
 
Acha mipango miji iwepo. Hatuna haja ya kuishi kama tupo mapangoni porini.
Vilevile watunga sheria wetu ndio wanaoleta bomoabomoa. Bomoabomoa ipo kisheria na sheria zimetungwa na wabunge tunaowachagua wenyewe. So kama hutaki mipango miji na bomoabomoa itakubidi uwe mbunge ukapinge sheria za mipango miji na miradi mingine inayolazimu kuwepo bomoabomoa, au chagua mbunge unayeamini ataweza kuzuia hiki.

Mleta mada acha uvivu wa kufikiri
 
Acha mipango miji iwepo. Hatuna haja ya kuishi kama tupo mapangoni porini.
Vilevile watunga sheria wetu ndio wanaoleta bomoabomoa. Bomoabomoa ipo kisheria na sheria zimetungwa na wabunge tunaowachagua wenyewe. So kama hutaki mipango miji na bomoabomoa itakubidi uwe mbunge ukapinge sheria za mipango miji na miradi mingine inayolazimu kuwepo bomoabomoa, au chagua mbunge unayeamini ataweza kuzuia hiki.

Mleta mada acha uvivu wa kufikiri

mmnh hivi wewe umenielewa kweli????:rolleyes::rolleyes::rolleyes:
 
Alianza raisi akaja mkuu wa mkoa sasa hivi hadi raia wenzangu hamtaki nibaki Dar, haya mi nawaachia jiji lenu la kubomoleana nyumba.
 
Acha mipango miji iwepo. Hatuna haja ya kuishi kama tupo mapangoni porini.
Vilevile watunga sheria wetu ndio wanaoleta bomoabomoa. Bomoabomoa ipo kisheria na sheria zimetungwa na wabunge tunaowachagua wenyewe. So kama hutaki mipango miji na bomoabomoa itakubidi uwe mbunge ukapinge sheria za mipango miji na miradi mingine inayolazimu kuwepo bomoabomoa, au chagua mbunge unayeamini ataweza kuzuia hiki.

Mleta mada acha uvivu wa kufikiri
Acha uongo.

Aliyesema Mwanza wasivunjiwe lilikua bunge lile?

Aliyetaka Jangwani pavunjwe lilikua bunge lile?
 
Acha uongo.

Aliyesema Mwanza wasivunjiwe lilikua bunge lile?

Aliyetaka Jangwani pavunjwe lilikua bunge lile?
Hakika wewe hujui kitu.
Suala la mwanza lilikuwa ni suala la mipaka. Taasisi ile ya serikali iliambiwa wazi kuwa kabla ya kubomolea wananchi inabidi ikae nao kwanza kujadili mipaka halisi. Tena wapo walioambia waanze kubomoa majengo yao wenyewe kabla hawajabomolewa kwa mujibu wa sheria, nao ni wale waliojenga karibu na uwanja wa ndege, na barabara iendayo huko.
Jangwani na maeneo mengine yanayostahili kuvunjwa, na yaliyavunjwa kweli, ni kwa mujibu wa sheria zilizotungwa na bunge. Au ulitaka spika wa bunge atoe tamko kuwa wavunjiwe ndio ujue ni bunge?
Wengine utawalaumu bure tu, wale ni watekelezaji wa sheria za bunge tu.
 
Hakika wewe hujui kitu.
Suala la mwanza lilikuwa ni suala la mipaka. Taasisi ile ya serikali iliambiwa wazi kuwa kabla ya kubomolea wananchi inabidi ikae nao kwanza kujadili mipaka halisi. Tena wapo walioambia waanze kubomoa majengo yao wenyewe kabla hawajabomolewa kwa mujibu wa sheria, nao ni wale waliojenga karibu na uwanja wa ndege, na barabara iendayo huko.
Jangwani na maeneo mengine yanayostahili kuvunjwa, na yaliyavunjwa kweli, ni kwa mujibu wa sheria zilizotungwa na bunge. Au ulitaka spika wa bunge atoe tamko kuwa wavunjiwe ndio ujue ni bunge?
Wengine utawalaumu bure tu, wale ni watekelezaji wa sheria za bunge tu.

Mkuu, sheria imetaka Jangwani pavunjwe, watu wameenda mahakamani kufungua kesi, kesi inaendelea uvunjaji ukaendelea.

Kwahiyo kisheria Jangwani pakatakiwa kuvunjwa, Mwanza tukaambiwa pasivunjwe ingawa iko ndani ya sheria hizi hizi.

Wewe upo hapa unaleta stori za bunge limesema bunge limesema.

Spika wa bunge atoe tamko la kuvunja yeye kama nani? Mtunga sheria na sera anazipeleka kwa executive body then stays on the corner hopping check and balance iwepo ili alichowakabidhi kifanyiwe kazi.

Check and balance is compromised.
 
Mdada unatakiwa ujue lengo la serekali ya ccm nikuwatesa wanainchi.


Kuna watu wanajenga sasa hivi wala ata hawakatazwi na umeme wanapewa na maji wanafungiwa kodi ya jengo na ya ardhi wanalipa baada ya miaka 17 utashangaa wanabomolewa.


Tunasafari ndefu.
Na anapaswa kuelewa kuwa kubomoa ni suluhisho la mwisho saana kwa mtu aliyeshindwa kutumia njia mbadala kabisa. Ubomoaji huu unawaacha wahanga wengi wakiwa fukara na chuki mioyoni. Hivyo basi, sheria za ujenzi zielimishwe kwa wananchi. Ufanyikapo ujenzi wasimamizi wa hizo sheria wafanye kazi zao kwa haki kuepusha hasara mbeleni.
Siyo mara zote ubomoaji ndiyo uwe dawa. Suluhisho mbadala litafutwe na siyo komoakomoa.
 
Acha mipango miji iwepo. Hatuna haja ya kuishi kama tupo mapangoni porini.
Vilevile watunga sheria wetu ndio wanaoleta bomoabomoa. Bomoabomoa ipo kisheria na sheria zimetungwa na wabunge tunaowachagua wenyewe. So kama hutaki mipango miji na bomoabomoa itakubidi uwe mbunge ukapinge sheria za mipango miji na miradi mingine inayolazimu kuwepo bomoabomoa, au chagua mbunge unayeamini ataweza kuzuia hiki.

Mleta mada acha uvivu wa kufikiri
Aisee! Hivi huwa zinatungwa sheria za bomoabomoa au sheria za mipango miji? Kwamba hutungwa sheria ili kubomoa nyumba? Fafanua
 
Mimi kuna kitu najiuliza sipati jibu. Hivi hawa maafisa mipango miji huwa wanafanya kazi gani? Kila siku wako maofisini na mishahara wanalipwa. Tena huenda minono. Sasa inakuwaje kuwe na bomoabomoa kama wanapanga miji?

Jiji kama dar ina maana hakuna master plan inayoelekeza nini kijengwe wapi? Hizi bomoabomoa zinahusika either na uzembe wa watu flani ambao hawakifanya kazi zao au rushwa au labda mipango yetu ya miji ni ya miezi sita sita.

Inastaajabisha mji unaokua kama Iringa majengo marefu yanasimamishwa katikati ya mji na wakati barabara ni nyembamba sana. Hakuna hata parking. Halafu baadae tunaambiwa hayo majengo yanayoota kama uyoga yavunjwe kupisha upanuzi wa barabara. Kama manyumbu hivi. Inaudhi na inatia gasara sana.

Naunga mkono hoja mkuu. Bomoabomoa ifanyike nchi nzima, once and for all na ofisi ya mipango miji ifikiriwe upya.
 
Back
Top Bottom