Ushauri: Biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia Noah (Dar au Pwani)

lizy lizy

Member
Aug 29, 2019
31
18
Wasalaam ndugu zangu.

Kijana mwenzenu nimejichanga nina kiasi kama cha mil. 16, nimefikiria nimeona ninunue Noah ili nifanye biashara ya kubeba abiria walau nami nijiajiri maana nimechoka purukushani za kuajiriwa.

Hivyo basi nilikua naomba mwongozo kuhusu maeneo ambayo biashara hii inafanya kazi kwa DSM au Pwani maana hadi sasa sijajua ni maeneo gani hasa watu hutumia Noah kama usafiri.

Natanguliza shukrani.
 
Wasalaam ndugu zangu.

Kijana mwenzenu nimejichanga nina kiasi kama cha mil. 16, nimefikiria nimeona ninunue Noah ili nifanye biashara ya kubeba abiria walau nami nijiajiri maana nimechoka purukushani za kuajiriwa.

Hivyo basi nilikua naomba mwongozo kuhusu maeneo ambayo biashara hii inafanya kazi kwa DSM au Pwani maana hadi sasa sijajua ni maeneo gani hasa watu hutumia Noah kama usafiri.

Natanguliza shukrani.
Vikindu kuna route zaidi ya nne
 
Wasalaam ndugu zangu.

Kijana mwenzenu nimejichanga nina kiasi kama cha mil. 16, nimefikiria nimeona ninunue Noah ili nifanye biashara ya kubeba abiria walau nami nijiajiri maana nimechoka purukushani za kuajiriwa.

Hivyo basi nilikua naomba mwongozo kuhusu maeneo ambayo biashara hii inafanya kazi kwa DSM au Pwani maana hadi sasa sijajua ni maeneo gani hasa watu hutumia Noah kama usafiri.

Natanguliza shukrani.
Una uzoefu na biashara ya usafiri? Una ujuzi wa kiufundi kuhusu gari? Nina mashaka huenda usifanikiwe kwani jinsi unavyouliza tu inaonyesha wewe ni mweupe pee kwenye biashara ya usafiri. Sikukatishi tamaa ndugu yangu ila nakupa angalizo tu.

Nasema hivi kwa sababu thread yako ni kama vile daktari amefungua thread anaulizia apasue sehemu gani ya kichwa kwani anataka kumfanyia surgery ya kichwa mgonjwa! Kuna biashara nyingine bila kujua abc zake ukiingia na mtaji mbuzi wako utalia haraka sana.

Nakushauri kama wewe ni dereva basi tafuta kazi ya kuendesha Noah mtu inayobeba abiria au gari yoyote ya abiria. Kama kupata kazi ni ngumu basi hata fanye u-daywaka wa gari lolote la abiria kwa kumkatia dereva wake kitu kidogo.
 
Una uzoefu na biashara ya usafiri? Una ujuzi wa kiufundi kuhusu gari? Nina mashaka huenda usifanikiwe kwani jinsi unavyouliza tu inaonyesha wewe ni mweupe pee kwenye biashara ya usafiri. Sikukatishi tamaa ndugu yangu ila nakupa angalizo tu.

Nasema hivi kwa sababu thread yako ni kama vile daktari amefungua thread anaulizia apasue sehemu gani ya kichwa kwani anataka kumfanyia surgery ya kichwa mgonjwa! Kuna biashara nyingine bila kujua abc zake ukiingia na mtaji mbuzi wako utalia haraka sana.

Nakushauri kama wewe ni dereva basi tafuta kazi ya kuendesha Noah mtu inayobeba abiria au gari yoyote ya abiria. Kama kupata kazi ni ngumu basi hata fanye u-daywaka wa gari lolote la abiria kwa kumkatia dereva wake kitu kidogo.
shukrani ndugu kwa mawazo, ila naomba unisaidie kwa kile nilichouliza hayo mengine niachie mimi
 
Back
Top Bottom