Ushauri BASATA wasanii wetu kazi zao ni za kimataifa sio Tanzania pekee

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,601
8,741
Ushauri wangu kwa Basata ni huu kazi za wasanii sio za Tanzania pekee na hamuwezi kukaa vikao bila kuelewa hilo. Usanii ni biashara ambayo serikali inanufaika kwa ubunifu sasa cha ajabu ni watu kuwa katikati na kutaka kuwaeleza wabunifu etu wabuni vipi!. Dhana ya hiki chama ni kusaidia kusiwepo na ubaguzi wa dini, jinsia, ukabila na kukokuwa na matusi. Mambo mengine kama wabunifu wanaimba kwa mafumbo ya kimapenzi au kisiasa waachwe wafanye kazi.

Lakini kikubwa ni kwamba kazi yao sio ya Tanzania pekee na hatuwezi kuwabana kiasi kwamba wasanii wetu washidwe kushindana na wenzao maana wenzao hawana sheria za watu eti kusoma mashairi yao kabla hayajatoka!. Hebu jiulizeni hizi rap za bongo flava na taarabu tofauti yake ni nini wote wanaweka mafumbo kwenye sanaa hizi.

Ukiangalia vizuri muziki wa Nigeria, US, South Africa na Congo hauna BASATA hivyo mkibana wasanii wetu kila siku tutakuwa watu wa kusikiliza miziki ya wenzetu. Tusishangae kwanini wasanii wetu wanaimba kwa lugha za kiingereza siku hizi sababu moja wapo wapo zaidi huru kusema lolote bila kufungiwa au kupigwa faini za kijinga lakini ukiangalia vizuri kama ni matusi kwenye kiingereza ni mara 100 ya kiswahili. Hivyo mnafanya wasanii wetu waanze kukimbia kutumia kiswahili kwenye nyimbo za budget kubwa.

Michael Jackson kwenye nyimbo yake BAD mstari wa kwanza anasema "Your Butt Is Mine" sasa je hii ina maana gani? mbona nyimbo haijafungiwa?

 
Hatuna aja ya kuwenda kwa kasi hivo, tamaduni zetu zinakataza na itakuwa hivo. Mpaka leo movie za kihindi wanashindwa kuonyesha watu wakikiss sisi tunataka tukimbilie wapi? "

Alternative wasanii waje na version mbili za kazi zao moja local nyingine international kama mzalendo sitavumilia kuona wasanii wanapanda mbegu za kifirauni kwa watoto wetu.
 
Hatuna aja ya kuwenda kwa kasi hivo, tamaduni zetu zinakataza na itakuwa hivo. Mpaka leo movie za kihindi wanashindwa kuonyesha watu wakikiss sisi tunataka tukimbilie wapi? "

Alternative wasanii waje na version mbili za kazi zao moja local nyingine international kama mzalendo sitavumilia kuona wasanii wanapanda mbegu za kifirauni kwa watoto wetu.

Sent from my 601SO using JamiiForums mobile app
Wasanii wa bongo wanazidi kuingiza habari za matusi kila kukicha.
Diamond nyimbo zake matusi matusi tu
 
"Your butt is mine" kwa Kiingereza cha Kimarekani ni tofauti sana na tafsiri ya Kiingereza straight.

Katika Kiingereza cha Marekani hapo maana yake ni kama "Utanitambua" au "Ama zako ama zangu" au "nitakupiga".

Lakini ukiweka tafsiri ya moja kwa moja kinachosomeka ni "Matako yako ni mali yangu".

Nafikiri mzizi wa "Your butt is mine" ni "I will kick your butt" maana yake nitakupiga.

Sasa hapo unaweza kuona ugumu wa lugha ya usanii.

Mtu anasema utanitambua, nitakupiga, anatafsiriwa kwamba anataka kumiliki matako ya mtu!

Hapo BASATA lazima wangekuja juu.
 
"Your butt is mine" kwa Kiingereza cha Kimarekani ni tofauti sana na tafsiri ya Kiingereza straight.

Katika Kiingereza cha Marekani hapo maana yake ni kama "Utanitambua" au "Ama zako ama zangu" au "nitakupiga".

Lakini ukiweka tafsiri ya moja kwa moja kinachosomeka ni "Matako yako ni mali yangu".

Nafikiri mzizi wa "Your butt is mine" ni "I will kick your butt" maana yake nitakupiga.

Sasa hapo unaweza kuona ugumu wa lugha ya usanii.

Mtu anasema utanitambua, nitakupiga, anatafsiriwa kwamba anataka kumiliki matako ya mtu!

Hapo BASATA lazima wangekuja juu.

Lakini kikubwa umenipata kuwa mafumbo ni sehemu ya ustanii na hivyo wasanii wawe huru.

unajua Price alikataa kuwa kwenye video hii kwasababu ya hiyo “your butt is mine”!
 
Lakini kikubwa umenipata kuwa mafumbo ni sehemu ya ustanii na hivyo wasanii wawe huru.

unajua Price alikataa kuwa kwenye video hii kwasababu ya hiyo “your butt is mine”!
Tanzania is topsy-turvy.

Ukisoma kitabu cha Andy Chande alielezea walikuwa censors wa sinema tangu miaka ya sitini, the job was a joke.

The same thing still goes on today.
 
Bahati mbaya hawatazuia nyimbo za matusi ila watakazia zile zenye nia ya kukosa tabia za baadhi ya watu ambao kwao wanaona wana manufaa
 
Back
Top Bottom