Habarini za wakati huu mabibi na bwana wa JF.......!
Mimi ni kijana wa kwanza kuzaliwa kwa wazazi wangu.
Kwa sasa nina umri wa miaka 27, kama mjuavyo huo ni umri sahihi kabisa wa mimi kuwa na mwenza wa kusaidiana nae kulisongesha gurudumu la maisha...!
Na mzee wangu amekua mastari wa mbele katika kunisisitiza nioe haraka iwezekanavyo....!
Sasa mchumba niliyempata kwa upande wake yuko vizuri kuanzia tabia yake, matendo yake...! Kiukweli ni binti aliyejitunza na kujiheshimu sana, vijana wa kileo tunaita "wife material" na halikadhalika mama yake ni mama anayejishemu na kuheshimu ndoa yake sana....!
Tatizo ni pale nilipomjulisha baba yangu juu ya kutaka kumuoa huyo binti....! Baba mwanzoni alikubali na kumsifia sana yule binti maana anamfahamu,....! Tunaishi jirani tu
Ila mzee hakuishia hapo akafanya uchunguzi akagundua baba yake mkubwa na huyo binti alikua mwizi...! Na aliuwawa kwa ajili ya wizi, kwa mantiki hiyo baba yangu kasema siwezi kumuoa sababu ya baba ake mkubwa kuwahi kuuwawa kwa ajili ya wizi....!
Akiwa na maana ya kwamba hata kizazi changu kinaweza kuwa cha wizi....!
Sasa ndugu zangu hiyo sababu inatosha kweli kumuacha binti wa watu, kwa kuhofia kuja kupata kizazi cha wizi? Hivi wizi huwa nia tabia ya kimalezi au kurithi?
Ushauri wako kwangu ni muhimu sana....! Maana jf kuna ma great thinker wengi
Mimi ni kijana wa kwanza kuzaliwa kwa wazazi wangu.
Kwa sasa nina umri wa miaka 27, kama mjuavyo huo ni umri sahihi kabisa wa mimi kuwa na mwenza wa kusaidiana nae kulisongesha gurudumu la maisha...!
Na mzee wangu amekua mastari wa mbele katika kunisisitiza nioe haraka iwezekanavyo....!
Sasa mchumba niliyempata kwa upande wake yuko vizuri kuanzia tabia yake, matendo yake...! Kiukweli ni binti aliyejitunza na kujiheshimu sana, vijana wa kileo tunaita "wife material" na halikadhalika mama yake ni mama anayejishemu na kuheshimu ndoa yake sana....!
Tatizo ni pale nilipomjulisha baba yangu juu ya kutaka kumuoa huyo binti....! Baba mwanzoni alikubali na kumsifia sana yule binti maana anamfahamu,....! Tunaishi jirani tu
Ila mzee hakuishia hapo akafanya uchunguzi akagundua baba yake mkubwa na huyo binti alikua mwizi...! Na aliuwawa kwa ajili ya wizi, kwa mantiki hiyo baba yangu kasema siwezi kumuoa sababu ya baba ake mkubwa kuwahi kuuwawa kwa ajili ya wizi....!
Akiwa na maana ya kwamba hata kizazi changu kinaweza kuwa cha wizi....!
Sasa ndugu zangu hiyo sababu inatosha kweli kumuacha binti wa watu, kwa kuhofia kuja kupata kizazi cha wizi? Hivi wizi huwa nia tabia ya kimalezi au kurithi?
Ushauri wako kwangu ni muhimu sana....! Maana jf kuna ma great thinker wengi