Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,643
- 218,099
Hii ndio njia pekee ya kudhibiti na kuondoa kabisa ubaguzi na mauaji ya wageni nchini Africa kusini , kabla ya kuendelea naomba kukiri kwamba mimi binafsi nina masilahi na yanayoendelea S.Afrca maana mimi nina vitega uchumi kwenye nchi ile japo kwa kushirikiana na wazawa .
Viongozi wa nchi ya South Africa wanaotokana na ANC wamelea kwa miaka mingi sana uchafu huu , bado haifahamiki sababu hasa za kulea jambo hili , bali wadau wengi wanaamini kwamba ulezi huu ni mkakati wa kisiasa , ni njia ya kujaribu kutowaudhi waafrica wengi wa nchini humo ili waendelee kushinda chaguzi , ni mkakati wa kishamba sana wenye gharama kubwa sana kwa ndani na nje ya nchi .
Kuna haja kubwa sana kwa wadau wapenda haki kuungana na kuiondoa ANC kwa nguvu ama kwa kura ili kudhibiti wahuni hawa wanaolindwa .
#Say No to Xenophobia