Ushauri: Ama Rais wa Tanzania aende DRC Congo au Rais wa DRC Congo aje Tanzania kupeana mikakati ya uongozi na biashara.

365

JF-Expert Member
Nov 28, 2014
1,377
1,453
Rais wa sasa wa DRC Congo, Felix Tshisekedi anatokea kabila kubwa la wafanyabiashara,Kabila la wakasai,asilimia kubwa ya mizigo ya wakongo wanaoingiza mizigo kupitia bandari ya Dar es salaam ni wakasai wanaoishi Lubumbashi,Katanga na Kasai.

Kwakweli kuwapoteza wafanyabiashara hawa ni hasara kubwa kwa Tanzania,

Rais wa Tanzania itafaa saana kama angeweza kwenda congo kuwashawishi wacongo na rais wao waendelee kupitishia mizigo yao hapa Tanzania,

Au Rais wa Tanzania amwalike rais wa DRC Congo Tanzania,ili aje azungumze nia yake ya kuendelea kufanya biashara na Tanzania.

Katika makosa ambayo sisi kama Tanzania hatutakiwi kufanya ni kupuuza soko la kongo kwa huduma na bidhaa zetu,congo ni soko kubwa la kila kitu kwa ukanda huu wa maziwa makuu,DRC Congo kila kitu hakitoshi isipokua mziki tu.

Sisi watanzania ambao hatuna namba za simu za Rais inabidi tutoe ushauri kupitia majukwaa kama haya,mheshimiwa rais zingatia sana hili suala,ni muhimu sana kwa maendeleo yetu wote.

Maendeleo hayana chama wala dini.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umetoa hoja nzuri mno ,ni hoja inayohitaji kufanyiwa kazi kitaalaamu sio kisiasa,nimebahatika mno kutembelea sana hizi nchi za ukanda huu na sio siri kuwa taratibu tunapoteza biashara kubwa kutoka DRC KWA WASHINDANI WETU HASA NAMIBIA,SA NA MSUMBIJI,inauma mno kuona sisi ambao tupo karibu mno na DRC hatunufaiki na nchi hii,na nchi hii(DRC) NDIO FUTURE ya AFRIKA,tukiikamata nchi hii na kiufanya ipitishie bidhaa zake hapa kwetu even for 70%mabadiliko makubwa ya kimaendeleo tutayapata,ni aibu kuona mizigo yake mingi inaelekezwa kwenye bandari ya DURBAN,wakati ya kwetu ambayo ipo karibu mno na wao tumelala usingizi,ni vema kwanza our no 1 afagie kwanza nchi yetu na tujipange vema,barabara yetu ya Dar to Tunduma ni lazima irekebishwe na iwe na sifa ya kuwa ni Highway(for now ni Main rd )na tuwashawishi ndugu zetu wazambia na wao warekebishe ya kwao ,maana kutoka pale Nakonde hadi Mpika hakuna barabara ni njia za kupita vifaru tu;na to make things more bad to us Zambia wametengeneza na kuboresha barabara yao ya kutoka Livingstone hadi few kms to Lusaka(its a first class road)na wanaitengeneza ya Lusaka to Ndola na ukipita kwa sasa pale kapiri mposhi pamebadilika kabisa.na matokeo ya haya DRC WANAELEKEZA BIASHARA ZAO KUSINI SIO KWETU HUKU,na tuelewe kwa kila malori 10 ya SA YANAYOVUKA MPAKA 6 KATI YAO YANAKWENDA DRC THR ZAMBIA!!!,hopeful mtoa hoja hii our no 1 atapata muda wa kuusoma.
 
Ushauri mzuri sana kwa wakati muafaka.Hata hao ATCL waache kurundika midege hapo airport wafikirie Lumbumbashi.Bahati nzuri nimeishi jimbo la Katanga na hasa pale Lubumbashi. Bidhaa zao nyingi mahotelini,madukani,nk ni Made in Tanzania.Ukifika mpakani pale Kasumbalesa kwenye msururu wa KM 3-5 wa malori,~90% ya trucks zina registration numbers za Tanzania yakitokea Daresalaam.Huwezi kujua,Rais mpya anaweza kuja na mawazo mapya bora "tujipendekeze"
 
Mkuu umetoa hoja nzuri mno ,ni hoja inayohitaji kufanyiwa kazi kitaalaamu sio kisiasa,nimebahatika mno kutembelea sana hizi nchi za ukanda huu na sio siri kuwa taratibu tunapoteza biashara kubwa kutoka DRC KWA WASHINDANI WETU HASA NAMIBIA,SA NA MSUMBIJI,inauma mno kuona sisi ambao tupo karibu mno na DRC hatunufaiki na nchi hii,na nchi hii(DRC) NDIO FUTURE ya AFRIKA,tukiikamata nchi hii na kiufanya ipitishie bidhaa zake hapa kwetu even for 70%mabadiliko makubwa ya kimaendeleo tutayapata,ni aibu kuona mizigo yake mingi inaelekezwa kwenye bandari ya DURBAN,wakati ya kwetu ambayo ipo karibu mno na wao tumelala usingizi,ni vema kwanza our no 1 afagie kwanza nchi yetu na tujipange vema,barabara yetu ya Dar to Tunduma ni lazima irekebishwe na iwe na sifa ya kuwa ni Highway(for now ni Main rd )na tuwashawishi ndugu zetu wazambia na wao warekebishe ya kwao ,maana kutoka pale Nakonde hadi Mpika hakuna barabara ni njia za kupita vifaru tu;na to make things more bad to us Zambia wametengeneza na kuboresha barabara yao ya kutoka Livingstone hadi few kms to Lusaka(its a first class road)na wanaitengeneza ya Lusaka to Ndola na ukipita kwa sasa pale kapiri mposhi pamebadilika kabisa.na matokeo ya haya DRC WANAELEKEZA BIASHARA ZAO KUSINI SIO KWETU HUKU,na tuelewe kwa kila malori 10 ya SA YANAYOVUKA MPAKA 6 KATI YAO YANAKWENDA DRC THR ZAMBIA!!!,hopeful mtoa hoja hii our no 1 atapata muda wa kuusoma.
Uko sahihi kabisa,bahati nzuri umeongea kitu halisi,wacongo kwa sasa idadi yao wakaribia milion 200,yaani ukichukua kenya,uganda,tanzania,burundi na rwanda kwa pamoja bado hawafikishi idadi ya watu wa congo,

Zambia imelishika vizuri soko la congo la mahindi,kwa siku zambia inauza tani nyingi za mahindi (ukiwa kasumbalesa border post utaona hili).

Tanzania tuko karibu sana na Drc congo kwa upande kusini (Tunduma-kapiri mposhi-copper belt-kasumbalesa-lubumbashi)

Lakini pia tuko karibu sana kwa upande magharibi (Kigoma-Goma).

Msumbiji,Zimbabwe,south africa,kenya, ziko mbali lakini wacongo wanapitisha mizigo huko.
Kwanini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
True kiongozi diplomasia ikizorota na uchumi wetu utazorota vilevile nashashauri hata maneno kama haya angeambiwa mkuu wetu akikataa ushauri aambiwe kama umbeya tuu.
 
Ushauri mzuri sana kwa wakati muafaka.Hata hao ATCL waache kurudindika midege hapo airport wafikirie Lumbumbashi.Bahati nzuri nimeishi jimbo la Katanga na hasa pale Lubumbashi. Bidhaa zao nyingi mahotelini,madukani,nk ni Made in Tanzania.Ukifika mpakani pale Kasumbalesa kwenye msururu wa KM 3-5 wa malori,~90% ya trucks zina registration numbers za Tanzania yakitokea Daresalaam.Huwezi kujua,Rais mpya anaweza kuja na mawazo mapya bora "tujipendekeze"
Sawa sawa,congo ni mhimu sana kwa biashara ya Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenda jana tu Kenya na yeye aanzishe safari ghafla ya kwenda kuonana nae nchi kweli inaendeshwa hivyo?

Taratibu tuache diplomasia ifanye kazi yake serikali inajua tofauti tunavyofikilia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu umetoa hoja nzuri mno ,ni hoja inayohitaji kufanyiwa kazi kitaalaamu sio kisiasa,nimebahatika mno kutembelea sana hizi nchi za ukanda huu na sio siri kuwa taratibu tunapoteza biashara kubwa kutoka DRC KWA WASHINDANI WETU HASA NAMIBIA,SA NA MSUMBIJI,inauma mno kuona sisi ambao tupo karibu mno na DRC hatunufaiki na nchi hii,na nchi hii(DRC) NDIO FUTURE ya AFRIKA,tukiikamata nchi hii na kiufanya ipitishie bidhaa zake hapa kwetu even for 70%mabadiliko makubwa ya kimaendeleo tutayapata,ni aibu kuona mizigo yake mingi inaelekezwa kwenye bandari ya DURBAN,wakati ya kwetu ambayo ipo karibu mno na wao tumelala usingizi,ni vema kwanza our no 1 afagie kwanza nchi yetu na tujipange vema,barabara yetu ya Dar to Tunduma ni lazima irekebishwe na iwe na sifa ya kuwa ni Highway(for now ni Main rd )na tuwashawishi ndugu zetu wazambia na wao warekebishe ya kwao ,maana kutoka pale Nakonde hadi Mpika hakuna barabara ni njia za kupita vifaru tu;na to make things more bad to us Zambia wametengeneza na kuboresha barabara yao ya kutoka Livingstone hadi few kms to Lusaka(its a first class road)na wanaitengeneza ya Lusaka to Ndola na ukipita kwa sasa pale kapiri mposhi pamebadilika kabisa.na matokeo ya haya DRC WANAELEKEZA BIASHARA ZAO KUSINI SIO KWETU HUKU,na tuelewe kwa kila malori 10 ya SA YANAYOVUKA MPAKA 6 KATI YAO YANAKWENDA DRC THR ZAMBIA!!!,hopeful mtoa hoja hii our no 1 atapata muda wa kuusoma.
Facts mkuu.

Ila ni mapema mno kusema serikali imezembea au imepuuzia kwa ujio wa Tshisekedi pale Kenya kana kwamba serikali imepoteza fursa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngoja rais amalize kukutana na waziri wa kilimo wa Zimbabwe ndiyo aende drc. Labda anachukua uzoefu jinsi kilimo cha Zimbabwe kilivyopiga hatua ili na sisi tufuate mbinu zao
 
Back
Top Bottom