Rutunga M
JF-Expert Member
- Mar 16, 2009
- 1,769
- 1,382
Humu katika JF kuna baadhi walikuwa mawakala wa vyama wakati wa mchakato wa kura.nimefanikiwa kuona nakala za matokeo walizopewa mawakala baada ya kuzisaini.Matokeo yalibandikwa pia kwenye vituo(kwa sehemu nyingi)Na wakati wa kujumlisha matokeo ya Rais,Wabunge kutoka kwenye vituo ulifanywa na wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya Wilaya chini ya WAWAKILISHI wa Vyama na wadau wengine na walipewa nakala za matokeo kwa nafasi ya Ubunge na Rais kisha nyingine kutumwa NEC makao makuu.Sasa kuna suala kuwa NEC taifa inabadilisha takwimu tofauti na halisi kutoka majimboni(Inawezekana)Hapa tuwekane sawa kuhusu suala hili la kubadilisha matokeo alyosema Dk Slaa.Kwa kuwa Vyama vina Nakala za matokeo kwa ngazi ya jimbo ,ebu watio mfano mmoja kwa kuskan zile nakala za matokeo ya jimbo fulani ambazo matokeo yake yanatofautiana na matokeo ya NEC kisha waziweke hapa JF .Tusiongelee tu kwamba kule Moshi kituo kimoja kilibadilishwa takwimu bila udhibitisho wa kutoshaInawezekana kabisa Wizi wa kura ulikuwepo na Kipenzi chetu DK Slaa akawa ameibiwa kura LAKINI ushahidi unaotolewa na Dk Slaa,Marando na wana JF haina uzito wa kutosha kuudhibitsha.hapa Twende kwa ushahidi tu