Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Viongozi wa serikali ya awamu ya tano wamekuwa wakidai kuwa wanamsubiri Tundu Lissu na dereva wake wapone ili wakamilishe uchunguzi wa tukio lile ambalo Tundu Lissu alishambukiwa na risasi zaidi ya 30 pale mjini Dodoma, hapo tarehe 7/09/2017 kwa lengo la kumwua
Sababu kuu inayotolewa na Jeshi la Polisi nchini ni madai kuwa eti kwa kuwa hawajampata Tundu Lissu na dereva wake kwa hiyo uchunguzi umeshindikana kukamilishwa!
Hata hivyo katika mahojiano ya hivi karibuni kwa vyombo vya habari vya kimataifa pamoja na kuongea na watanzania waishio ughaibuni, Tundu Lissu na dereva wake wametoa Maelezo ya ushahidi ambao endapo Jeshi la Polisi utauifanyia kazi wanaweza wakawapata "watu wale wasiojulikana"/waliofanya shambulio lile kwa nia ya kumwua Tundu Lissu
Tundu Lissu na dereva wake wametoa ushahidi wao kama ifuatavyo:-
1. Kwa kawaida huwa panakuwepo ulinzi wa Massa 24/7 wa askari wenye silaha pale kwenye geti la kuingilia kwenye makazi yao. Lakini cha kushangaza siku ya tukio lile hapakuwepo na ulinzi wowote. Kwa hiyo Tundu Lissu na dereva wake wanawataka Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi ni nani aliamuru kusiwepo ulinzi siku hiyo??
2. Palikuwepo CCTV camera kwenye majengo hayo ya viongozi wa ngazi za juu wa Taifa hili, lakini camera hizo za CCTV zilinyofolewea na kupelekwa mahali kusikojulilama, kwa hiyo wameliomba Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi ni nani aliyehusika na kuzinyofoa camera hizo??
3. Tundu Lissu amedai kuwa kuna Mkuu wa Mkoa mmoja ambaye alionekana mkoani Dodoma, siku hiyo ya tukio hilo mjini Dodoma. Wakati ambapo siku hiyo hiyo kulikuwa na tukio la kukabidhi ripoti ya makinikia, kwa Mheshimiwa Rais, tukio ambalo siyo kawaida kwa Mkuu huyo wa Mkoa kukosekana kuhudhuria tukio hilo, kwa hiyo ingekuwa vyema Mkuu huyo wa Mkoa akahojiwa alikuwepo Dodoma kwa shughuli gani kwa kuwa kuna kitu kinachoitwa "suspicious characters" kwa lugha ya kisheria, ambazo inabidi zifanyiwe uchunguzi
Polisi huwa wanaomba ushrikiano kutoka kwa raia wema ili watoe ushahidi wa matuio kama hayo yanapotokea, kwa hiyo Tundu Lissu na dereva wake wameshatoa ushirikiamo kwa tukio zima hilo, kwa hiyo ni kazi ya Jeshi la Polisi kumalizia kazi ya kuwabaini wahalifu hao
Kama Polisi wasipofanyia uchunguzi wa ushahidi huo na wanaendelea kusisitiza tu wanamtaka Tundu Lissu na dereva wake warejee nyumbani ili wake watoe ushahidi wao, ndipo hapo tunapijiuliza iwapo Tundu Lissu na dereva wake wameshatoa ushahidi wao ni kwanini Jeshi la Polisi liendelee kisisitiza kuwa ni lazima Tundu Lissu na dereva wake warejee nchini ili watoe "physically" ushahidi huo, je dhamira yao ni nini??
Je wanajilaumiu kwa kutoweza "ku-accomplish" jukumu hilo zito la "kutoa" uhai wa Mheshimiwa Tundu Lissu kwa hiyo kumtaka arejee nyumbani ili wajje wakamilishe zoezi lile "lililofeli" mwaka 2017 kwa second chance??
Kama Jeshi la Polisi litakanusha kuwa hilo siyo lengo lao basi wakubali wachunguzi wa nje waje nchini kulichiunguza kwa undani tukio hilo ili kila kitu kiwekwe hadharani!
Kwa kukataa wachunguzi kutoka nchi za nje waje kuchunguza tukio lile, ambalo ni zaidi ya mwaka mmoja unusu hawajamkamata hata mtuhimiwa mmoja kumuhoji ni "indirectly" wanakiri kuwa ni "wao" ndiyo waliohusika na shambulio lile!
Sababu kuu inayotolewa na Jeshi la Polisi nchini ni madai kuwa eti kwa kuwa hawajampata Tundu Lissu na dereva wake kwa hiyo uchunguzi umeshindikana kukamilishwa!
Hata hivyo katika mahojiano ya hivi karibuni kwa vyombo vya habari vya kimataifa pamoja na kuongea na watanzania waishio ughaibuni, Tundu Lissu na dereva wake wametoa Maelezo ya ushahidi ambao endapo Jeshi la Polisi utauifanyia kazi wanaweza wakawapata "watu wale wasiojulikana"/waliofanya shambulio lile kwa nia ya kumwua Tundu Lissu
Tundu Lissu na dereva wake wametoa ushahidi wao kama ifuatavyo:-
1. Kwa kawaida huwa panakuwepo ulinzi wa Massa 24/7 wa askari wenye silaha pale kwenye geti la kuingilia kwenye makazi yao. Lakini cha kushangaza siku ya tukio lile hapakuwepo na ulinzi wowote. Kwa hiyo Tundu Lissu na dereva wake wanawataka Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi ni nani aliamuru kusiwepo ulinzi siku hiyo??
2. Palikuwepo CCTV camera kwenye majengo hayo ya viongozi wa ngazi za juu wa Taifa hili, lakini camera hizo za CCTV zilinyofolewea na kupelekwa mahali kusikojulilama, kwa hiyo wameliomba Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi ni nani aliyehusika na kuzinyofoa camera hizo??
3. Tundu Lissu amedai kuwa kuna Mkuu wa Mkoa mmoja ambaye alionekana mkoani Dodoma, siku hiyo ya tukio hilo mjini Dodoma. Wakati ambapo siku hiyo hiyo kulikuwa na tukio la kukabidhi ripoti ya makinikia, kwa Mheshimiwa Rais, tukio ambalo siyo kawaida kwa Mkuu huyo wa Mkoa kukosekana kuhudhuria tukio hilo, kwa hiyo ingekuwa vyema Mkuu huyo wa Mkoa akahojiwa alikuwepo Dodoma kwa shughuli gani kwa kuwa kuna kitu kinachoitwa "suspicious characters" kwa lugha ya kisheria, ambazo inabidi zifanyiwe uchunguzi
Polisi huwa wanaomba ushrikiano kutoka kwa raia wema ili watoe ushahidi wa matuio kama hayo yanapotokea, kwa hiyo Tundu Lissu na dereva wake wameshatoa ushirikiamo kwa tukio zima hilo, kwa hiyo ni kazi ya Jeshi la Polisi kumalizia kazi ya kuwabaini wahalifu hao
Kama Polisi wasipofanyia uchunguzi wa ushahidi huo na wanaendelea kusisitiza tu wanamtaka Tundu Lissu na dereva wake warejee nyumbani ili wake watoe ushahidi wao, ndipo hapo tunapijiuliza iwapo Tundu Lissu na dereva wake wameshatoa ushahidi wao ni kwanini Jeshi la Polisi liendelee kisisitiza kuwa ni lazima Tundu Lissu na dereva wake warejee nchini ili watoe "physically" ushahidi huo, je dhamira yao ni nini??
Je wanajilaumiu kwa kutoweza "ku-accomplish" jukumu hilo zito la "kutoa" uhai wa Mheshimiwa Tundu Lissu kwa hiyo kumtaka arejee nyumbani ili wajje wakamilishe zoezi lile "lililofeli" mwaka 2017 kwa second chance??
Kama Jeshi la Polisi litakanusha kuwa hilo siyo lengo lao basi wakubali wachunguzi wa nje waje nchini kulichiunguza kwa undani tukio hilo ili kila kitu kiwekwe hadharani!
Kwa kukataa wachunguzi kutoka nchi za nje waje kuchunguza tukio lile, ambalo ni zaidi ya mwaka mmoja unusu hawajamkamata hata mtuhimiwa mmoja kumuhoji ni "indirectly" wanakiri kuwa ni "wao" ndiyo waliohusika na shambulio lile!