Daimler
JF-Expert Member
- Sep 11, 2018
- 556
- 973
Wana wa Mungu walilala na mabinti wa wanadamu.
Kulingana na Biblia, wanadamu walipoongezeka duniani, Wana wa Mungu waliona mabinti wazuri na kuwachukua kuwafanya wake zao na kuzaa nao watoto. Huo uzao ulikuwa wa watu hodari na giant. Walikuwa wanakula vyakula vingi pamoja na mahitaji mengine (kama ngono) ambapo wanadamu walishindwa kuhimili kuwahudumia kwa ubora na hivyo kusababisha mateso makubwa kwa wanadamu.
Kutokana na wanadamu kushindwa kuhimili mahitaji ya majitu hayo, walikuwa wakiwakimbia na kujificha kwa hofu ya kuuawa. Majitu hayo yalianza kupambana yenyewe kwa yenyewe na hivyo kuleta machafuko kwa wanadamu duniani.
Ubabe wa Giants ulipelekea vifo vya wanadamu wengi.
Mungu aliposikia kilio cha wanadamu, kutokana na maovu yaliyokuwa yakitendeka, akaamua kuwafutilia mbali hao wanadamu wote kupitia Gharika. Hivyo, alimteua Nuhu na familia yake kujiponya kupitia Safina, ambapo aliweza kukusanya pair ya wanyama wote duniani na ndege ili kuepuka gharika.
Kulingana na Biblia:
- Walikuwepo Wanefili (uzao wa Anunnaki) waliokuwa Giants kabla Wana wa Mungu (Watchers) hawajaja duniani. Hivyo, Wana wa Mungu walipokuja duniani, waliwakuta tayari Waanunnaki.
- Wana wa Mungu (Watchers) walikuja duniani baada ya kuwaona mabinti wazuri wa wanadamu huku duniani. Hivyo wakazaa nao watoto ambao walikuwa hodari na giants (kama walivyokuwa Wanefili/Waanunnaki). Swali: Mbona hao watchers hawakuwa wamewahi kuja duniani kabla? Je, madai ya Wataalamu kuwa, Anunnaki ndio walimfundisha mwanadamu namna ya kujiremba, yanaweza kuwa, yalipelekea mabinti kuanza kupendeza na hivyo kuvutia Wana wa Mungu?
- Kwenye gharika, Aliens waliokufa ni Giants wa uzao wa Wana wa Mungu (Watchers) lakini Wanefili/Waanunnaki hawakufa na gharika. Ndiyo maana Mussa alipotuma wapelelezi kwenda Canaan, waliripoti kukuta hao Wanefili. How?
- Katika Kitabu cha Watchers, Enoch alichukuliwa na Malaika na kupelekwa Mbingu ya Tano, ambako huko alijionea kundi kubwa la Askari walioitwa Grigori waliofanana na binadamu. Walikuwa na maumbo makubwa zaidi kuliko Giants wa duniani.
Kama Wanefili ndio hao hao waliozaliwa na Wana wa Mungu, basi hii inaonyesha wazi kuwa, gharika haikuwahi kutokea ya kuua wanadamu wote, ndiyo maana Wanefili walisalimika.
Pamoja na Wanefili (Nephilim), neno la Kiebrania "Rephaim" linajumuisha aina zote za makundi ya majitu (Giants) ya Canaan. Akina Goliath na wengineo wote walikuwa ni mabaki ya aina mbalimbali za Waanunnaki.