Isalia213
JF-Expert Member
- Nov 3, 2011
- 1,198
- 431
Siku nyingi zimeshapita tangu kutokea tukio la kusikitisha kule Soweto Arusha, linalohusiana na kurushwa kwa bomu katika mkutano wa hadhara wa Chadema. Lengo langu sio kukumbushia machungu kwa wale waliopata hapana lengo ni kukumbusha ule ushahidi wa mh, Mbowe aliosema anao, naona siku zinasonga lakini hadi hii leo bado tunasubiria ushahidi kutoka kwa mh, Mbowe hatujauona.Tuseme alitania au muda haujafika wa kuutowa kwani tunahamu sana ya kujua ushahidi wa tukio lile. Mh, Mbowe tunaomba sana ushahidi kujua ni nani aliehusika na lile tukio.