OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,189
- 103,708
Achana na mastori ya Yanga kujipa moyo kwamba Gendarmerie ni kibonde. Unaweza kuona trend ya matokeo yao kule kwao ukapata picha.
Ushindi mkubwa wa Simba haumaanishi hii timu ni KIBONDE bali ni uwezo mkubwa wa Simba ambao mpaka serikali kupitia Waziri Mwakyembe wamekiri.
Simba ni timu itakayotisha mbaya kwenye CAF Confederation na tayari imeshaanza kuogopwa. Ukitizama matokeo ya jana, ni Simba ni kati ya VIGOGO WANNE tu barani Africa waliopata ushindi wa kuanzia goli nne ikiwepo APR, El Masry, Petro Atletiko na Simba yenyewe
Jopo la coach na wachezaji msije kujidanyanga kwamba Genda ni timu ndogo kibonde. Tunataka tuendelee na speed ile ile katika local na international games. Sisi ndio timu pekee tegemeo kuiwakilisha Tanzania kimataifa. Simba ni timu tegemeo