Ushabiki wa mgogoro wa Iran na Marekani siyo wa kisiasa ni wa kidini

Idd Ninga

JF-Expert Member
Nov 18, 2012
5,136
4,298
Kwa muda sasa wa siku chache mitandao mingi ya kijamii watu wamekua wakitoa maoni yao kuhusu mgogoro unaoendelea katika ya nchi ya Marekani na Iran huku baadhi ya watu wakionekana kuishabikia Marekani kwa kile walichokifanya huku upande wa pili ukionekana kuilUamu Marekani na kuunga mkono Irani kuwa imefanyiwa vitendo visivyo vya halali kwa kiongozi wao wa kijeshi kuuliwa.

Ushabiki mkubwa ulipo hapo siyo wa siasa na sera za kiamerika na kiirani,bali ni misukumo ya dini ambayo inapelekea watu wengi kuwa upande fulani wa mgogoro huo.

Siyo mara ya kwanza kwa Marekani kufanya shambulio kama hilo, miaka ya 1989, jeshi la Marekani lilitungua ndege ya shirika la Irani na kuua abiria wote 290 waliokuwepo ndani ya ndege hiyo.

JE, SABABU NI NINI MAREKANI WAMEFANYA HAYA LEO?
Ukitazama mgogoro huu haujaanza leo, taifa la Marekani limeonekana kwa muda mrefu likinyemelea mataifa ya kiarabu na mwisho kuyatafutia sababu za vita kwa ajili ya maslahi yao binafsi huku wanajeshi wao wengi na maelfu ya raia wakipoteza maisha yao na mwisho wa siku kuziacha nchi za watu zikiwa chakavu na uharibufu mkubwa.
Alichofanya Marekani ni kutafuta sababu ya kuingia na kuivamia Iran kwa sababu zake anazozijua yeye za kwanini ukanda huo wa Arab. Na kwa kuwa lengo lake ni kutaka vita,

JE KISASI KITALIPIZWA?
Kwa kifupi tusitegemee kuona kisasi kikilipizwa ndani ya Marekani, kisasi kitalipizwa nje ya Marekani kwa yeyote yule aliemmarekani kugeuzwa mbuzi wa tambiko ili Mmarekani apate sababu ya kuivamia Iran, atakua radhi atume pandikizi lolote ambalo litakamilisha kazi ya kisasi,atakabidhiwa dola zake za kutosha na kazi itakua imeisha kwa upande wa kwanza,hapo kisasi kitalipwa na Mmarekani mwenyewe,kwa sababu lengo la Marekani nyuma ya ukanda wa waarabu ni kutengeneza vita na siyo amani.

Yaliyotokea katika mataifa ya Afghanistani,Iraq na Libya,yalikuwa ni maandalizi ya kuivamia Irani,kwa sababu,wao waamerika waliamini wakiweza kuzipiga nchi hizo basi itakuwa rahjisi kuingia Irani kwa sababu tayari uwezo wa kupitisha silaha utakuwa mrahisi zaidi na uwezo wa kutengeneza viabaraka mapandikizi utakua wa kiwango cha juu.
Wakati waafrika tunashabikia hili,tusidhani hatupo kwenye shabaha ya taifa hilo,Afrika ipo katika shabaha hiyo,shabaha ambayo itafuata baada ya Irani kuharibiwa,baadae watamalizia na mataifa ya India,Korea na China,Kisha safari ya mwisho ya Marekani kuwa super power itakamilika ndani ya Afrika kwa muda mfupi kabisa kutokana na nguvu ndogo iliyopo ndani ya bara hili.

KISASI KITALIPWA NJE YA MAREKANI, Irani itavamiwa, vita kubwa itapiganwa, dunia itaathirika na mwisho Marekani wataondoka bila ya sababu ya msingi ya kuishambulia Irani, Uingereza itaomba raia wake msamaha kuwa ilikosea kuwa mshiriki wa vita hivyo, umasikini utarudi nchini Irani, soko la bidhaa la kidunia litapanda, hela itakua ndogo, Marekani atakula bata.

TUJIONGEZE.
 
Chonde chonde muingereza, usije ukahusika na hiyo vita mbaka EPL iishe msimu huu, tukimshuhudia liverpool akiondoka na ubingwa kwa zaidi ya alama 100.

YNWA.
 
Kuivamia Iran na kupeleka majeshi ya mguu haiwezekani ila wanachotaka ni mafuta tu ya Iraq na kuiwekea vol wazo Iran
Kama tujuavyo ISIL ndio walivunja historic sites za Iraq zote na yuma yake ilikuwa ni kuiba artefacts zote ambazo ni historia ya nyuma sana hata miaka 3000.

Nani walikuwa nyuma ya wizi huo?

Marekani
Nasema hivi kwa uhakika kwani baada ya miezi michache tu vito hivyo vya thamani vilikuja ulaya na USA na kuuzwa kwenye maduka makubwa kwa bei mbaya. Sasa yaleyale Trump ulimi umeteleza na kusema atashambulia majengo ya kizamani akijua fika kuna vitu vingi vya thamani zaidi ya dhahabu.

Hapo utajua who’s behind it, and definitely not Arabs


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
January 7, 2020

Tanzania nayo yachukua tahadhari


Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania ktk mahojiano na kituo cha televisheni cha Azam TV amekiri kuona taadhari iliyotolewa na Wizara ya Masuala ya Nje ya Marekani kupitia Ubalozi wao uliopo Tanzania. Hivyo jeshi la Polisi linaichukulia taarifa hiyo kwa umakini na kujipanga maana Tanzania ni sehemu ya Jumuiya ya Kimataifa alisema msemaji huyo wa Jeshi la Polisi.
Source: Azam TV
 

Gharama hapo kweli,tutaachwa sana,LONG SURVIVOR
Sijasoma uzi wake wote huyu V.M huwa ana kreki mahala.
Nimesoma hadi katikati lakini neno arabu na ukanda wa arabu limetawala sana.
.
Sasa nimeshindwa kuelewa ukanda wa uajemi toka lini ukawa wakiarabu?
Sasa kama haujasoma hadi mwisho utaelewa ?
Soma kwanza hadi mwisho ukimaliza uniambie nimemaliza,halafu uje kuuliza swali la unachotaka kuuliza.
 
Vita kati ya Marekani na Iran itokee vita ya 3 ya dunia? Hii itakuwa ni ndoto za mchana. Kipindi Iraq anachapwa, Iran alikuwa kimya wala hakuongea na hakuna nchi iliyoingilia
Iran inabidi apotezee, ajifanye kama haoni kilichotokea.

Watu wamewekeza mabilion ya fedha kujiandaa kuivamia Iran halafu ajidai anajua vita? Atapigwa mpaka achakae na hakuna mrusi au mchina atakayeingilia kati.

Mtoa uzi ukipewa visa ya kwenda kuishi Marekani au Iran utaichagua ipi?
Watu hawapigani vita ili kuonesha wanasilaha kali bali kutaka utajiri. Kuna mali nchi fulani, twende tukavamie, tuchukue.
 
Lakini vita ni vita tu haijalishi wewe ukoje unaweza kuwa vizuri na ukachakazwa tu nilijifunza pale somalia yaani majeshi yenye weledi lakini yalisalimu amri.
 
Vita kati ya Marekani na Iran itokee vita ya 3 ya dunia? Hii itakuwa ni ndoto za mchana. Kipindi Iraq anachapwa, Iran alikuwa kimya wala hakuongea na hakuna nchi iliyoingilia
Iran inabidi apotezee, ajifanye kama haoni kilichotokea.

Watu wamewekeza mabilion ya fedha kujiandaa kuivamia Iran halafu ajidai anajua vita? Atapigwa mpaka achakae na hakuna mrusi au mchina atakayeingilia kati.

Mtoa uzi ukipewa visa ya kwenda kuishi Marekani au Iran utaichagua ipi?
Watu hawapigani vita ili kuonesha wanasilaha kali bali kutaka utajiri. Kuna mali nchi fulani, twende tukavamie, tuchukue.
Na unaona ni ufahari kwenda kuvamia na kuiba mali za nchi nyingine?wewe ni mfuasi wa PK

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yanayo endelea ni muendelezo na mkologo wa mkubwa kutaka cha anae muona mdogo. Ubabe huu utaipekea aibu na anguko la Marekani...
 
Hayo wanayofanya hata waarabu walifanya sana kipindi cha biashara ya watumwa Afrika Mashariki.
Nao wao waonje dhuluma waliokuwa wanafanya Tanganyika na Zanzibari.
Najua wewe ni mfuasi wa asiyejua kusoma na kuandika ndiyo maana roho inakuuma.
Haulazimishwi kupigana ila unatengenezewa sababu ili uingie kwenye vita. Kiduku kukaa zake kimya siyo kama mjinga bali aliepusha mengi.
Na unaona ni ufahari kwenda kuvamia na kuiba mali za nchi nyingine?wewe ni mfuasi wa PK

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom