The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Siamini! siamini! siamini!
Ushabiki huu ulipoanza nilidhani kejeli. Baadhi walianza kwa kusema Lowassa bado ana nguvu sana ndani ya CCM nikaamini (nakubaliana na hilo 100%), Wengine wakasema yeye ni mkali kidogo kuliko JK nikakubaliana na hilo na mengine mengi yakaja ya ukweli na ya uongo. Sikudhania itafika siku watokee watu wa kumkweza Lowasa kufikia hatua ya kuanza kampeni za kumtafutia urais mapema kiasi hiki.
Mmoja kaamua kumlinganisha Lowassa na Dr. Slaa akidai mmoja kati ya hawa pekee ndiye angefaa kuongoza nchi yetu (kama itakuwapo bado) ifikapo 2015 Oktoba. Nimeshtuka sana kuiona hali hii ya ushabiki wa ghafla-ghafla kumuunga mkono Lowasa.
Hawa watu wanaotaka Lowassa (ambaye yupo tayari kufanya lolote kupata urais) awe na hadhi sawa na Dr. Slaa (aliyesubiri watu wengine waseme anafaa urais na kumwomba agombee) wanatumia kigezo gani?
Lowassa aliyedai wabunge wamemwandama kwa habari za magazeti ya udaku na kushindwa kuthibitisha hilo leo anafaa vipi kuwa rais wa Tanzania? Kwanini kama tunaipenda nchi yetu kwa dhati tusimtupilie mbali jumla ili akija kiongozi mwingine awe na nidhamu na kujua kuwa watanzania ukiokosea wanakutimua na ajizuie kukosea maksudi?
Je, ni kweli kwamba tumefilisika viongozi wanaofaa na kubakiwa na Lowasa pekee huko kwenye Magamba? Is it possible kwamba tu wajinga kiasi hicho au ni laana ya fedha ili tuamini kuwa wanaompigia debe wanatarajia kupata fadhila zake mzee huyo, asiyecheka na wanyonge kama watendaji katika wilaya na kuwanyenyekea wenye fedha kama Rostam hata kufikia kupindisha sheria maksudi ili watajirike zaidi kwa gharama za wanyonge? Ya Richmond si madogo lakini naamini vyombo vyetu vya dola vingekuwa huru vingegundua madudu mengine zaidi.
Nawatahadharisha watanzania kutofanya kosa la kumfagilia Lowassa, si kwa ajili ya kumwadabisha tu bali kuweka msingi imara kwa waroho kama yeye endapo watajitokeza next time. Viongozi wajao wanatakiwa kujifunza kutokana na adabu tutakazoamua kuwatia kina Mkapa, JK na wapambe wao kwa makosa ya kukusudia waliyofanya ili kujitajirisha.
Tuendelee kumwomba Mwenyezi Mungu atuasaidie kupata viongozi bora na kutuepusha na watu wa "Zamu Yetu" kama Ridhiwan, JK, Lowassa na wengine wengi ambao tutazijua habari zao vema baada ya serikali ya wanamtandao kuondoka madarakani.
Ushabiki huu ulipoanza nilidhani kejeli. Baadhi walianza kwa kusema Lowassa bado ana nguvu sana ndani ya CCM nikaamini (nakubaliana na hilo 100%), Wengine wakasema yeye ni mkali kidogo kuliko JK nikakubaliana na hilo na mengine mengi yakaja ya ukweli na ya uongo. Sikudhania itafika siku watokee watu wa kumkweza Lowasa kufikia hatua ya kuanza kampeni za kumtafutia urais mapema kiasi hiki.
Mmoja kaamua kumlinganisha Lowassa na Dr. Slaa akidai mmoja kati ya hawa pekee ndiye angefaa kuongoza nchi yetu (kama itakuwapo bado) ifikapo 2015 Oktoba. Nimeshtuka sana kuiona hali hii ya ushabiki wa ghafla-ghafla kumuunga mkono Lowasa.
Hawa watu wanaotaka Lowassa (ambaye yupo tayari kufanya lolote kupata urais) awe na hadhi sawa na Dr. Slaa (aliyesubiri watu wengine waseme anafaa urais na kumwomba agombee) wanatumia kigezo gani?
Lowassa aliyedai wabunge wamemwandama kwa habari za magazeti ya udaku na kushindwa kuthibitisha hilo leo anafaa vipi kuwa rais wa Tanzania? Kwanini kama tunaipenda nchi yetu kwa dhati tusimtupilie mbali jumla ili akija kiongozi mwingine awe na nidhamu na kujua kuwa watanzania ukiokosea wanakutimua na ajizuie kukosea maksudi?
Je, ni kweli kwamba tumefilisika viongozi wanaofaa na kubakiwa na Lowasa pekee huko kwenye Magamba? Is it possible kwamba tu wajinga kiasi hicho au ni laana ya fedha ili tuamini kuwa wanaompigia debe wanatarajia kupata fadhila zake mzee huyo, asiyecheka na wanyonge kama watendaji katika wilaya na kuwanyenyekea wenye fedha kama Rostam hata kufikia kupindisha sheria maksudi ili watajirike zaidi kwa gharama za wanyonge? Ya Richmond si madogo lakini naamini vyombo vyetu vya dola vingekuwa huru vingegundua madudu mengine zaidi.
Nawatahadharisha watanzania kutofanya kosa la kumfagilia Lowassa, si kwa ajili ya kumwadabisha tu bali kuweka msingi imara kwa waroho kama yeye endapo watajitokeza next time. Viongozi wajao wanatakiwa kujifunza kutokana na adabu tutakazoamua kuwatia kina Mkapa, JK na wapambe wao kwa makosa ya kukusudia waliyofanya ili kujitajirisha.
Tuendelee kumwomba Mwenyezi Mungu atuasaidie kupata viongozi bora na kutuepusha na watu wa "Zamu Yetu" kama Ridhiwan, JK, Lowassa na wengine wengi ambao tutazijua habari zao vema baada ya serikali ya wanamtandao kuondoka madarakani.