Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,907
- 22,053
na Deogratius Temba
KIKAO cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika jana Ikulu jijini Dar es Salaam, kimeikwamisha Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu kujadili utendaji hafifu wa Kampuni ya Reli (TRL) na Shirika la Ndege (ATCL).
Jana asubuhi Waziri wa Miundombinu pamoja na Menejimenti ya TRL na ATCL walitakiwa kufika mbele ya kamati hiyo, iliyokuwa ikiendelea na vikao vyake katika Ofisi Ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa taarifa na msimamo wa serikali juu ya mkataba wa kampuni hizo.
Hatua ya kukwama huko ilitangazwa mbele ya waandishi wa habari jana na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mohamed Misanga baada ya wabunge kukusanyika ukumbini kwa ajili ya kupokea taarifa hizo.
Misanga alisema jana asubuhi kamati ilipanga kukutana na waziri husika na viongozi wengine ili kutoa msimamo wa serikali juu ya mkataba wa kampuni hizo.
Tulipanga leo tupokee taarifa hizo mbili na kujua msimamo wa serikali, lakini nimepokea barua ya waziri iliyoandikwa na msaidizi wake akiiomba kamati ihairishe kikao hiki hadi atakapopata nafasi, alisema Misanga.
Barua hiyo yenye kumbukumbu namba WMI/Gen/2009 kwenda kwa mwenyekiti wa kamati na kusainiwa na msaidizi wa waziri, Alphonce Mwingira, ilisema Waziri Kawambwa atakuwa kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri kilichokuwa kikifanyika Ikulu.
Kamati hiyo iliridhia maombi hayo na kudai kuwa itapokea taarifa hiyo mjini Dodoma wiki ijayo kwenye mkutano wa 17.
KIKAO cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika jana Ikulu jijini Dar es Salaam, kimeikwamisha Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu kujadili utendaji hafifu wa Kampuni ya Reli (TRL) na Shirika la Ndege (ATCL).
Jana asubuhi Waziri wa Miundombinu pamoja na Menejimenti ya TRL na ATCL walitakiwa kufika mbele ya kamati hiyo, iliyokuwa ikiendelea na vikao vyake katika Ofisi Ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa taarifa na msimamo wa serikali juu ya mkataba wa kampuni hizo.
Hatua ya kukwama huko ilitangazwa mbele ya waandishi wa habari jana na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mohamed Misanga baada ya wabunge kukusanyika ukumbini kwa ajili ya kupokea taarifa hizo.
Misanga alisema jana asubuhi kamati ilipanga kukutana na waziri husika na viongozi wengine ili kutoa msimamo wa serikali juu ya mkataba wa kampuni hizo.
Tulipanga leo tupokee taarifa hizo mbili na kujua msimamo wa serikali, lakini nimepokea barua ya waziri iliyoandikwa na msaidizi wake akiiomba kamati ihairishe kikao hiki hadi atakapopata nafasi, alisema Misanga.
Barua hiyo yenye kumbukumbu namba WMI/Gen/2009 kwenda kwa mwenyekiti wa kamati na kusainiwa na msaidizi wa waziri, Alphonce Mwingira, ilisema Waziri Kawambwa atakuwa kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri kilichokuwa kikifanyika Ikulu.
Kamati hiyo iliridhia maombi hayo na kudai kuwa itapokea taarifa hiyo mjini Dodoma wiki ijayo kwenye mkutano wa 17.