Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Inasikitisha, inakera, inaudhi na inaboa kweli kweli pale unapoona kwamba tangu mwezi wa pili hadi leo watanzania wenzetu walioathirika kwa mabomu huko gongo la mboto bado wanakaa kwenye mahema. Hawa watu hawakuingia mkataba na JWTZ kwamba ifanyie majaribio ya mabomu yake kwao, ni kiherehere cha serikali ya Kikwete na jeshi lake kuamua kuwashambulia wananchi wasio na hatia, sasa iweje watu hawa waendelee kutaabika kwenye mahema na mvua hizi zinazoendelea Dar? Jamani kama kuna asiyejua namna ambavyo hawa watu wanataabika, ajaribu japo kupita maeneo ya Majohe, kitunda, Moshi bar na maeneo ya jirani ajionee jinsi watanzania wenzetu wanavyotaabika na familia kwa kuishi kwenye mahema ambayo mengi yake yameoza na yanavuja.
Juzi nimepita mahali nikaona mama anavyohangaika na watoto kutokana na maji kuingia ndani ya hema, nikasikia uchungu sana. Huyu mtu alikuwa na nyumba yake na maisha yake leo hii anageuka kuwa mtumwa na ombaomba kwa kuwa tu jeshi lilikosa mahali pa kujaribishia mabomu yake. Sitaona shida kuingia msituni kupambana na hii serikali ya kibazazi iwapo nitatakiwa kufanya hivyo. I have nothing to loose if I die. Sioni faida ya mimi kuendelea kuishi wakati watanzania wengine wakiendelea kulia na kuomboleza kutokana na uhuni wa serikali hii ya kiuaji.
Juzi nimepita mahali nikaona mama anavyohangaika na watoto kutokana na maji kuingia ndani ya hema, nikasikia uchungu sana. Huyu mtu alikuwa na nyumba yake na maisha yake leo hii anageuka kuwa mtumwa na ombaomba kwa kuwa tu jeshi lilikosa mahali pa kujaribishia mabomu yake. Sitaona shida kuingia msituni kupambana na hii serikali ya kibazazi iwapo nitatakiwa kufanya hivyo. I have nothing to loose if I die. Sioni faida ya mimi kuendelea kuishi wakati watanzania wengine wakiendelea kulia na kuomboleza kutokana na uhuni wa serikali hii ya kiuaji.