Usalama wa Taifa: Mpo likizo?

Status
Not open for further replies.

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
Looks like it sasa kabla hamjaanza kumshambulia R.O tuanze kwa kuangalia hao wazungu walikuwa ni akina nani na je walipewa security clearance na nani? Na kwa nini walikuwa wanaopiga picha wakati wananchi wa kawaida hata kulima maboga jirani na kambi za jeshi hawaruhusiwi

Je hii failure ni ya watu wa ARMY INTELLIGENCE au watu wa USLAMA WA TAIFA? Je uslama wa Taifa wako likizo? na kwa nini SALVA AJIBU maswali yasiyo mhusu? MBONA KUMEKUWA NA MEDIA BLACKOUT kwenye hili?

Kazi kwenu


========================

HELIKOPTA YA JESHI NA UTALII

  • Likizo ya rais na usalama wa taifa

SITAKI Rais Jakaya Kikwete aende likizo wakati kuna "suala kubwa linaloshusu usalama wa nchi."

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyememu aliviambia vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Ijumaa kuwa rais yuko likizo, lakini aweza kufanya kazi iwapo kuna suala kubwa linalohusu usalama wa nchi.

Ukweli ni kwamba rais asingekwenda likizo, kwani suala linalohusu usalama wa nchi lipo mezani kwake. Ni lile linalohusu usalama wa mipaka ya nchi na wananchi wake.


Ni suala la kuingia katika ghala la silaha za Jeshi la Wananchi (JWTZ), kuchukua helikopta ya jeshi na kuruka hadi Arusha, huku waliokuwemo, tena watu kutoka nchi za nje – Uingereza, Canada, Marekani na Australia, wakipiga picha.

Tutake tusitake, hili ni suala la usalama wa nchi. Linahusu usalama wa wananchi na mali zao. Linahusu maisha ya nchi na viumbe wake.


Katika safu hii wiki iliyopita, nililalamikia ukimya wa serikali kuhusu tukio hilo. Niliuliza maswali 42. Nilidhani wahusika wataelewa. Watakuwa wepesi wa kujibu. Wataona wanawajibika kutoa majibu. Wataonyesha uadilifu.

Leo hii, wiki tatu tangu kupatikana kwa taarifa za helikopta ya jeshi kutumiwa na watalii kupiga picha, hakuna taarifa yoyote ya serikali – kutoka kwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Juma Kapuya au Amiri Jeshi Mkuu, Jakaya Mrisho Kikwete.

Katika hali hii, sharti watu wenye uchungu na nchi hii; wale wanaojali usalama wa nchi na watu wake, waendelee kuuliza. Hii ni kutokana na uzito wa suala lenyewe; ni kubwa na "linahusu usalama wa nchi."

Ingawa wanaoiuzia silaha Tanzania wanajua kuna aina gani, kiasi gani, kutoka wapi, kwa bei ipi, zinaweza kutumiwa vipi na zina uwezo gani; kuna mambo kadhaa hawajui. Kwa mfano, hawajui lini silaha hizo zinahitajika kufanyiwa kazi.


Lakini hatua ya watu kutoka nchi za nje, kukodi, au kupewa, au kuiba helikopta ya jeshi na kuitumia kwa kazi binafsi, inaonyesha kuwa: Jeshi limeingiliwa. Kuna wanaojua taratibu za kila siku jeshini, matumizi ya zana; zipi zinahitajika sasa, zipi zikodishwe na zipi zikae "stendibai."

Hao ndio wanakwenda ama kuchukua, kukodi au kupewa helikopta za jeshi. Au kuna "Idara ya Masoko" jeshini inayotangaza na kufuatilia wateja wa kutumia hekikopta zake.

Aidha, hatua ya kupata helikopta ya jeshi kwa matumizi binafsi, inaonyesha ama ulinzi ndani ya jeshi umepungua au umelegezwa. Nani kapunguza au kalegeza ulinzi na kwa nini; ndilo swali kubwa hivi leo.

Nani amekataa kuweka suala hili mezani kwa Rais Kikwete, mpaka rais anakwenda likizo bila kulishughulikia? Au, nani amemshauri rais kuwa ni "jambo dogo" kwa hiyo alale na kusahau?

Au tafsiri ya "usalama wa nchi" ndiyo inagomba? Na hili linawezekana. Kuna wanaodhani usalama wa nchi ni usalama wa rais kutopinduliwa, kutopingwa au kutoseng'enywa. Huo ni ufinyu na upofu.

Nani anaweza kumuaga rais, na kumtakia likizo njema, wakati katika jeshi lake kuna biashara inayoweza kuzaa mtafaruku mkubwa wa kuweza kumeza amani nchini au kurudisha nyuma maendeleo madogo ya kidemokrasi yaliyopatikana?


Labda rais awe anajua kuwa kinachoendelea "ni kidogo kisicho na athari mbaya na kubwa;" au anaridhika kuwa kinachofanyika ni sahihi; au hana taarifa kamili juu ya kinachotendeka.

Vyovyote itakavyokuwa, hapo ndipo rais anapaswa kujenga mashaka juu ya chochote kinachotendeka; hasa chochote ambacho wananchi wametilia mashaka; na hasa kile ambacho wachambuzi wameonyesha kinaweza kuleta madhara kiulinzi, kisiasa na kiuchumi.

Ukimya wa serikali unaleta tafsiri nyingi. Kwamba wanaokataa kutoa kauli, wanajua kinachoendelea lakini wanashindwa kutoa majibu ambayo wanajua vema kwamba hayatazima kiu ya wananchi na wapenda nchi.

Kwamba wanaokataa kutoa kauli wanajua nani aliidhinisha matumizi ya helikopta nje ya utaratibu; wanajua kama ndio utaratibu na wanajua nani anachuma kutoka mradi huu ambao bila shaka unaingiza fedhi nyingi.

Na katika hili, tukizungumzia viongozi serikalini ambao wanapaswa kutoa kauli, tuna maana ya kwanza na moja kwa moja, Rais Kikwete, Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri Kapuya, mteule wa rais, Jenerali Mwamunyange na Waziri wa Habari Mohamed Seif Khatib.

Kama wasemaji wanaona suala hili la kuvunja na kuingia kwenye ngome ya jeshi na kuchukua, kuiba au kupewa helikopta ni suala dogo, kwa nini hawatoi majibu yanayolingana na "udogo" huo?

Kama wanaona ni suala kubwa, tena la ulinzi na usalama wa nchi, kwa nini wanakaa kimya na kumwacha rais aende likizo wakati kuna suala kubwa la kumzuia kwenda kulala?

Mkuu wa Mawasiliano ikulu, Salva Rweyemamu, anasema likitokea jambo kubwa la usalama wa nchi, rais anaweza kufanya kazi akiwa likizoni.

Salva, mpelekee rais suala hili. Mfafanulie kwamba, kama ngome ya jeshi imepenywa, na watu kutoka nje wakachukua helikopta ya jeshi kwa raha binafsi, basi yeye na wananchi wake wote, wako uchi!

Mwambie avae na avalishe nchi yake. Lakini muhimu zaidi, mwambie ajibu maswali ya wananchi yaliyowasilishwa kupitia safu hii – wiki iliyopita na leo – ili wajue nafasi yake katika hili na hatua anazochukua.


(Makala hii imeandikwa kwa kuchapishwa katika safu ya SITAKI ya gazeti la Tanzania Daima, Jumapili, 23 Desemba 2007. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)

========================

Huyu mzee alianza na article hii:


========================

JWTZ NA BIASHARA YA KITALII

Na Ndimara Tegambwage

SITAKI serikali ikae kimya kuhusu matumizi ya helikopta ya Jeshi la Wananchi (JWTZ) iliyoanguka mkoani Arusha siku 11 zilizopita. Sitaki!

Maelezo ya awali ni kwamba helikopta ya jeshi ilikuwa imebeba "watalii" kutoka Canada, Marekani, Uingereza na Australia na kwamba ilianguka na kuwaka moto.

Watalii na helikopta ya jeshi? Watalii kutoka nchi za nje, na siyo watalii wa ndani ya nchi, na helikopta ya jeshi? Watalii wasiokuwa na uwezo kifedha wa kukodisha ndege yao mpaka watumie helikopta ya jeshi?

Watalii kutoka nchi tajiri, Canada, Marekani na Uingereza, nchi washirika wakubwa katika maendeleo ya Tanzania kwa kutoa mikopo na misaada, hawana uwezo wa kukodi ndege kutoka kampuni binafsi? Mpaka watumie helikopta ya jeshi?

Eti watalii walikuwa wanapiga picha za Ziwa Natron na mlima Oldonyo wenye volcano hai! Kwamba ziwa na mlima haviwezi kuonekana vizuri kutoka ndege ya kiraia mpaka mpigapicha awe katika ndege ya jeshi?

Katika hili kwa nini serikali inakaa kimya? Inataka habari hii ife? Inataka wananchi waendelee kujiuliza maswali mengi bila kupata majibu sahihi? Au inataka baadaye, itoke na kauli kwamba mambo ya jeshi hayajadiliwi katika vyombo vya habari?

Hakika, hapa serikali isisubiri kuumbuliwa. Ni jana, Jumamosi, baadhi ya waandishi wa habari walikabidhiwa tuzo za uandishi wa uchunguzi nchini. Ukweli ni kwamba bado wanatambaa, lakini tuzo hizo ni motisha kubwa katika kuandika habari za uchokonozi.

Leo hii, hakuna habari nono kama hii. Rubani wa helikopta ni nani? Helikopta ilianzia wapi safari ya kwenda Natron na Oldonyo. Ilipita wapi na "watalii" walikuwa wakifanya nini kabla ya kukaribia maeneo waliyokuwa wakitaka kupiga picha?


Je, kuna kitengo cha utalii katika JW? Kama kipo, kina ndege na helikopta ngapi? Vifaa vyake vingine kwa shughuli hii ni vipi? Je, utalii ni moja ya miradi ya jeshi ya kuzalisha fedha za matumizi ya nyongeza? Je, jeshi linapungukiwa fedha kiasi cha kuanzisha miradi ya "kubangaiza?"

Je, helikopta iliyobeba watalii iliidhinishwa na nani kufanya kazi hiyo? Ilitoka ngome ipi ya jeshi? Kwa nini iliamuliwa kuwa hiyo ndiyo ilikuwa inafaa? Rubani wa helikopta ya jeshi alijuaje maeneo ya kupita ili watalii wapate picha nzuri waliozotaka?

Kuna maswali mengi. Wanaoitwa watalii walitoka wapi kabla ya kuingia Tanzania? Nani anaweza kuthibitisha kweli kwamba ni watalii? Viwanja vya ndege na, au mipaka ya nchi ina rekodi gani juu ya kuingia nchini kwa watalii hao?

Tayari helikopta imeanguka na kuungua. Watalii wamepona! Nani amethibitisha uraia wa watalii? Balozi za nchi watokako watalii hao, zilizoko Dar es Salaam, zinasemaje juu ya raia wake, kama kweli wanatoka huko?

Balozi ambazo nchi zao huning'iniza serikali za nchi nyingi zikizitaka kuwa adilifu, zinasema nini juu ya raia wake kutumia helikopta ya jeshi la ulinzi kwa raha na mafao ya binafsi?

Kuna uhusiano gani kati ya watalii wa Canada, Marekani, Australia na Uingereza kwa upande mmoja, na balozi na nchi watokako, kwa upande mwingine? Je, inawezekana "watalii" wametumwa kutoa mtihani wa uimara au ulegevu wa jeshi?


Nani alichora mpango wa watalii kutumia helikopta ya jeshi? Huyo lazima awe mtu muhimu katika mahusiano ya jeshi. Kwamba ndege ndogo za kibiashara zinagombea maegesho kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere, ni motisha gani watalii walipata kutumia ndege ya jeshi?

Hapa ni muhimu kujua iwapo rubani alikuwa askari wa JW au raia anayejua kuvurumisha kikata hewa hicho Je, rubani wa helikopta alikodishwa kwa kiasi gani au alikuwa wa kujitolea?

Je, helikopta ya jeshi ilichukuliwa kwa mkataba upi? Kuna malipo yoyote yaliyotolewa au ahadi ya kulipa? Kiasi gani cha malipo – fedha taslimu au asante kwa njia mbalimbali? Lini malipo hayo yatatolewa au yalitolewa?


Lakini muhimu pia ni kujua nani hasa anafaidika na malipo hayo – aliyeidhinisha matumizi ya helikopta, rubani na aliyemtuma, baadhi ya maofisa wakuu jeshini, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa au ikulu? Nani anapokea "mshiko?"

Muhimu pia ni kwamba Amiri Jeshi ni rais. Mara hii ni Jakaya Mrisho Kikwete ambaye wakati anaondoka wiki hii kwa ziara ya Marekani aliacha helikopta yake imetumiwa na "watalii" na imeanguka na kuungua.

Amiri Jeshi anasemaje juu ya matumizi ya helikopta "yake?" Helikopta za jeshi, kama zilivyo ndege na magari ya jeshi, ni sehemu ya zana za kazi; waweza kusema, zana za ulinzi wa taifa. Vimeundwa na vinapaswa kutumika na kusimamiwa kwa misingi ya ulizi.

Nafasi ya Amiri Jeshi ni ya kulinda maisha na mali za wananchi ndani ya mipaka ya nchi yao na dhidi ya uchokozi au uvamizi kutoka nje. Kwa maana pana, helikopta ni mali ya wananchi, waliyonunua kwa kodi wanazotozwa na inayopaswa kutumiwa kwa ulinzi wao.

Katika mazingira ambamo serikali imekataa kutoa taarifa juu ya helikopta ya jeshi kutumiwa na watalii kutoka nje kufanya shughuli binafsi, ni uandishi wa wa uchokonozi ambao pekee unaweza kusaidia kuleta nuru juu ya kilichotendeka.

Hadi hapo taarifa zitakapowekwa wazi, acha kila mwananchi awe na mawazo yake: Kwamba sasa jeshi linabangaiza kama machinga; au halina ulinzi kwani kila mmoja aweza kuingia na kujichukulia ndege anavyotaka; au ulinzi wa wananchi sasa mashakani; au wakubwa wameamua kutumia jeshi kufanya biashara ya anga; au amiri jeshi kaenda likizo.

(Makala hii imeandikwa kwa ajli ya safu ya SITAKI, gazeti la Tanzania Daima Jumapili, 16 Desemba 2007. Mwandishi anapatikana kwa simu: 0713 614872; imeili: ndimara@yahoo.com)
 
Lakini kama mtakumbuka right from the begining hizo Helicopter ilisemwa kuwa hazitakuwa zinakaa tu kusubiri kutumiwa na wanajeshi, ilisemwa zitakodidshwa ili kuiletea serikali mapato. Hata hivyo ikumbukwe kuwa maisha ya ndege ni angani na siyo kuiground. Kwenye suala hili tusiinyoshee sana kidole serikali, tujaribu kuangalia busara yake, unless kama kulikuwa na ufisadi ndani yake as usual.
 
Lakini kama mtakumbuka right from the begining hizo Helicopter ilisemwa kuwa hazitakuwa zinakaa tu kusubiri kutumiwa na wanajeshi, ilisemwa zitakodidshwa ili kuiletea serikali mapato. Hata hivyo ikumbukwe kuwa maisha ya ndege ni angani na siyo kuiground. Kwenye suala hili tusiinyoshee sana kidole serikali, tujaribu kuangalia busara yake, unless kama kulikuwa na ufisadi ndani yake as usual.

wanajeshi wetu kazi zao za kulinda nchi zimewashinda hadi wanaingilia kazi za kufanya biashara ya kukodi chopas kwa pesa ya walipa kodi. Nani aliamua iwe hivyo? Je, wamepata faida kiasi gani tangu waanze hii biashara? Hiyo faida nani anachukua Jeshi au kwenye matumbo ya MAFISADI?
 
Dua that is a big question, ni kwanini jeshi lijiingize kwenye biashara? What is the purpose, no doubt ni ufisadi tu ndiyo main motive, lakini mimi sioni rationale ya kuliingiza jeshi kwenye biashara!
 
Bongolander,
Mpaka watu wakafikia hiyo hatua maana yake ni kwamba kuna maswali mengi kuliko majibu. Kwanini JWTZ imepata kigugumizi kusema kwamba hiyo chopper ilikodishwa? Kapuya na Naibu wake hawakutoa majibu ya kueleweka. Kapuya alisema yuko Kaliua, Naibu wake akasema kwamba ameagiza apelekewe comprehensive report kwamba hiyo chopper iliendaje huko, nani alikuwa anaendesha, je ilikaguliwa kabla ya kuruka, na kwanini ilipelekwa huko. Maelezo hayo aliagiza apewe na Chief of Staff. Mpaka leo hii hakuna majibu juu ya hilo swala.

Prof Maghembe na Nyoni walitofautiana katika kutoa kwao majibu na yalikuwa shallow kiasi kwamba kulikuwa na maswali mengi zaidi katika maelezo/majibu yao. Kauli ya Prof. Maghembe iko wazi, kwamba taarifa za hao watu zilikuwepo Ikulu na hivyo inaonekana kulikuwa na blessings za Rais. Je, ndo kusema walikuwa ni wageni wa Rais?

Ikulu walitoa maelezo ambayo yalipingana na Wizara ya Utalii, sasa kwenye mazingira kama hayo unatoa picha gani?

Kama hao wageni walikuwa ni wa wizara ya maliasili na utalii, ilikuwaje wawe na mwenyeji (tour guide ambaye si mwajiriwa wa wizara?). Huyo mwenyeji wao alikuwa ni mtu wa Arumeru na si mfanyakazi wa serikali, hapo unapata picha gani?

Kwanini JWTZ isiseme wazi kwamba hiyo chopper ilikodishwa? Kigugumizi kinatoka wapi? Kinachoonekana wazi ni kwamba hao jamaa walikuwa wanafanya kazi kwa maslahi ya watu fulani lakini wameumbuliwa na ajali hiyo. Bila ya hiyo ajali wala tusingesikia lolote kuhusu hao "watalii" walioletwa kupiga picha. Je, hizo picha zilikuwa zinapelekwa wapi? Eti walikuja kwa ajili ya kutengeneza documentary kwa ajili ya ku-promote utalii Bongo. Documentary gani inatengenezwa kinyemela sina hakika kama Bodi ya Utalii ilikuwa na habari juu ya ugeni wa hao watu, expectation yangu ingekuwa kwamba TTB ndiyo wangekuwa wenyeji wao na wangeweza kutoa tour guides ambao wangewapeleka kwenye sehemu ambazo wao TTB wanajua ni muhimu ziwe kwenye documentary. Tangu lini mtengeneza documentary akajiongoza mwenyewe wakati hajui huko kwenye mbuga za wanyama kuna kipi na kipi zaidi ya kusoma kwenye magazeti ama kuona kwenye news?

Kwa kifupi ni kwamba hapo kuna utata mkubwa sana hasa kwa upande wa wizara ya utalii na pia Ikulu, lazima kuwe na maswali mengi zaidi.
 
Dua that is a big question, ni kwanini jeshi lijiingize kwenye biashara? What is the purpose, no doubt ni ufisadi tu ndiyo main motive, lakini mimi sioni rationale ya kuliingiza jeshi kwenye biashara!

Ukiona Jeshi linatumika kwenye shughuli kama hizi lazima ujue kwamba ni ufisadi wa hali ya juu. Matumizi ya fedha za usalama wa taifa na JWTZ huwa wabunge au mtu yeyote haruhusiwi kuyaingilia eti kwa ajili ya kuhatarisha usalama wa nchi na mipaka yake.

Jeshi limeishatumika kwenye biashara ya dhahabu na likaishia kupata hasara ambayo hatujui ni kiasi gani. Juzi tukaambiwa Jeshi lilikuwa na mgodi wa dhahabu, hatujui ni pesa kiasi gani imeteketea. Kila kukicha tunaambiwa wanabinafsisha ili kuiondoa serikali kwenye shughuli za uzalishaji/biashara ili sekta binafsi ichukue nafasi, hapo hapo unajiuliza hivi Jeshi ni sekta binafsi ama? Tangu lini Jeshi likafanya biashara? Hii sijawahi ona katika nchi yoyote hapa duniani, nadhani JWTZ itakuwa ya kwanza.
 
Serikali yetu imeacha kukodisha ngege zake siku hizi? Haya maswali ya kuhusu hilo chopper aulizwe mkuu wa kikosi cha anga na watu wote waliotoa clearance ya ilo dubwana kuruka..maana jeshi letu nalo limejaza wageni wajerumani,wachina kuna wale wafaransa wa pale airwing sasa tunategemea wakija ndugu zao watashindwa kuwapa chopper kwenda mbugani?
 
Lamsingi ni taarifa ili wananchi sisis tuweze kujua,lakini serikali inapokaa kimya hatuelewi.Inawezekana ilikuwa inafanya jambo hili kwa njia ya heri na ata mtu yeyote angeweza kufanya lakini sisi kama wananchi tupewe taarifa ilikuwa hivi na vile.Kwa muono wangu mimi huo ndio uwajibikaji.
 
Yaleyale!

Hii ni labda ya kufungia mwaka 2007!

Maswali utayoulizwa ukingia Russia au Israleli au USA kwa sasa pamoja na "tailgating" itakayofuata kwa shughuli za walioongelewa hapa kwamba ni watalii, basi ndio mtu utajua maana ya Usalama wa taifa na maslahi yake yaani kwa kiingereza "national interests".

Jeshi na mali zake ni sehemu ya maslahi ya taifa na kuwa kuzingatia hilo kama kumekiukwa taratibu, basi mkuu wa majeshi ameshindwa kazi na ajiuzuru (kama inawezekana!)

Vinginevo, bado hatuwezi kutofautisha usalama wa taifa na maslahi yake na mambo haya ya kipuuzi yaliyotokea.

Na kama kweli kauli hii ni dhahiri, basi jeshi letu linajiharibia sifa yake kwa matukio haya ambayo ndio kipimo cha utendaji wake.
 
Kumekuwa na ziara nyingi sana za JK na EL huko US , Canada na UK .Who knows labda ni washirika wa barrick bado wanaila Nchi yetu ? Usalama wa Taifa upo kupambana na watu kama Zitto na Upinzani kwa ujumla lakini wako tayari kuchukua fedheha na wasiseme kitu . Kumbuka RO na Mwamunyange walivyo rushwa hadi kuwa hapo .Endelea kujiuliza mwananchi .
 
ni kweli huyu mzee he has got a point ku question abt this issue ambayo ni issue nyingine ambayo ina kiini macho flani where by at the end wanaofaidi ni wachache walioko juu nasi wananchi kama kawaida ya mazingaombe mengine twaishia kupiga makofi tukiwa hatujui ni trick gani imefanywa on us!
nashukuru Mungu angalau hii akaikwamisha kwa namna moja au nyingine haya sasa Watanzania tujitahidi kufungua machi na kungangania kuuliza ili tuambiwe ukweli wa trick hiyo na hata zingine nyiiingi kama zile za richmond n.k
 
Kumekuwa na ziara nyingi sana za JK na EL huko US , Canada na UK .Who knows labda ni washirika wa barrick bado wanaila Nchi yetu ? Usalama wa Taifa upo kupambana na watu kama Zitto na Upinzani kwa ujumla lakini wako tayari kuchukua fedheha na wasiseme kitu . Kumbuka RO na Mwamunyange walivyo rushwa hadi kuwa hapo .Endelea kujiuliza mwananchi .


Lunyungu
Umeraise point moja nzuri sana. Unajua nchi nyingine wanatumia inteligency officers kuendeleza nchi. Sio kufanya kazi za kuwalinda viongozi na kuwakandamiza wapinzani au kuwatishia waandishi wa habari. Ukiangalia nchi kama Israel, Mossad haijali kama Katsav amebaka, au Olmert amefanya fyongo kwenye stock market na mambo mengine, wanatoa taarifa kwa PP ambaye anamfikisha kwenye mkono wa sheria. Maslahi ya taifa mbele na maslahi ya chama au mtu binafsi baadaye
Sijui kama kweli idara yetu ya usalama inafanya kazi ya kutumia raslimali zake kuendeleza nchi, au hata at least kuwapa watanzania siri za biashara ili kuinufaisha Tanzania(kama Intel ya wafaransa ilivyosaidia kufanya makampuni ya Ufaransa yapige bao makampuni ya Marekani). It is very sad, kuona kama definition ya usalama wa Taifa bado iko kwenye enzi ya Nyerere wakati kuna issue nyingi mpya zinatokea, na matishio ya zamani yametoweka sasa hivi kuna matishio mapya na tasks mpya ambazo zinahitaji more effective na stronger intel.
Nilidhani Othman baada ya kufanya kazi na watu wa M 16 ataingiza mambo ya kisasa kwenye intel, lakini bado naona kama bado iko kwenye mambo ya miaka ya 60 na sabini.
 
So far developments from our humble government on this matter of our NATIONAL SECURITY is as follows:



RAIS yuko kimya!

WAZIRI MKUU yuko kimya!

MAKAMO WA RAIS yuko kimya!

MEDIA Tanzania wako kimya!

WAPINZANI wako kimya!

WAZIRI WA ULINZI yuko kimya!

RASHID OTHMAN wa uslama wa Taifa na timu yake nao kimya!

IKULU iko kimya !(majibu yao ni lege lege )


MAMBO YA NDANI
iko kimya!

WAZIRI WA UTALII
yuko kimya!

WIZARA YA UTALII iko kimya!


KAMPUNI
husika iko kimya!




na kutokana na hizi catalogue za events ambazo clearly zina threaten our NATIONAL SECURITY mtu unaweza kufikia conclusion ifuatayo:

JK is incompetent katika kila angle hivyo sioni sababu ya kumuamini kwa lolote lile

JK hana interest na NATIONAL SECURITY ya TANZANIA japo ni mwanajeshi

ECHELON nzima ya SERIKALI YA JK eidha imeoza..hapa ni Top/ Bottom au tuseme has been likizo for the last TWO YEARS

WAPINZANI nao ni ma culprits katika hili(hii sishngai kwani ndio kawaida yao)

na zaidi ya yote kuna hatari ya sisi kuelekea kuwa another FAILED STATE kwani serikali yetu ina kila symptoms za FAILED STATE

najua hii post inaweza kuwa provocative LAKINI kama kuna mtu anitakia mema TANZANIA huwezi ukakubali majibu waliyoyatoa IKULU
 
Serikali yafafanua helikopta iliyoanguka Ziwa Natron

Mwandishi Wetu
HabariLeo; Friday,December 28, 2007 @18:03


SERIKALI imetoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya helikopta ya Jeshi iliyoanguka Ziwa Natron mkoani Arusha ikiwa na raia wa kigeni. Taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari ya Tanzania (Maelezo) jana Dar es Salaam ilisema helikopta hiyo ilitolewa na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa ajili ya kampuni ya Travel Channel ya Marekani kwa ajili ya kupiga picha za kuitangaza Tanzania nchi za nje.

"Mapema mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete alifanya ziara nchini Marekani ambako pamoja na mambo mengine, alitoa mwaliko kwa Kampuni ya Travel Channel ya nchini humo ili kuja nchini kupiga picha vivutio vya utalii na uwekezaji kwa ujumla," ilisema taarifa hiyo.

Idara ya Maelezo ilisema kampuni ya Travel Channel, ilifanya utaratibu wa kupata kibali cha kupiga picha na ilipewa kibali namba 00001028, ambacho kilianza Novemba 29, mwaka huu na kinatarajia kwisha leo.

"Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ilitoa helikopta kwa wapiga picha hao ili kuwawezesha kutekeleza kazi hiyo waliyotumwa na Rais kwa lengo la kutangaza vivutio hivyo vilivyopo hapa nchini," ilisema taarifa.

Taarifa hiyo pia ilimnukuu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi, Abel Mwesiumo akisema, "tulitoa helikopta hiyo kwa maslahi ya Taifa," Katika ziara hiyo, kampuni ya Travel Channel iliomba kupiga picha katika maeneo ya Arusha, Dodoma, Ngorongoro, Oldonyo Lengai, Ziwa Natron, Bagamoyo, Dar es Salaam na Zanzibar. Aidha, taarifa hiyo ilisema mratibu wa zoezi hilo ni Dk. Aloyce Nzuki, ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Utalii katika Wizara ya Maliasili na Utalii.
Source: HabariLeo.


SteveD.
 
RAIS yuko kimya!

Yuko Ngoro Ngoro kwa mapumziko ya siku saba, the dataz ni anamalizia kuliweka sawa baraza jipya la mawaziri!
 
Alivyoumia mzee akukweti, mudhihiri, kapuya tulipata update za maendeleo ya tiba zao mara kwa mara na tukafariji familia zao kwa maombi. Mbona wataalamu wetu hatuwapi uzito uleule? Huyu rubani hatujui anaendeleje, rubani aliyebebeshwa mchele wa mbeya hatujui aliishia wapi, Gavana wetu kajuliwa hali na RO kamaville yuko mahabusu!
 
Huo sio ufafanuzi bali ni maelezo ya juu juu ambayo yanaongeza maswali badala ya majibu. Hiyo kampuni ya Travel Channel bila shaka iliingia mkataba na serikali kutengeneza hizo documentaries za kuitangaza Tanzania, sasa huo mkataba unasemaje? Labda kuna kipengele kinachohusu host country kutoa usafiri wa helikopta kwa production crew nzima and the like.

Sasa serikali inapokaa kimya halafu inakuja kujaribu kufunika kizembezembe hivi kunaashiria kuna kitu wananchi wanafichwa, inawezekana kabisa sivyo lakini huu ukimya umejaa utata, wahenga walisema kimya kingi kina mshindo mkuu...

Nimeicheki hii habari:

http://http://www.nydailynews.com/entertainment/tv/2007/12/12/2007-12-12_forrest_sawyer_i_almost_died_in_crash.html
 
Taa nyekundu inamuakia Kikwete,mwenzie Kibaki C***** inabana sasa hivi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom