Usalama wa mtu anayetoa pesa kwenye hivi vibanda vya huduma ni mdogo sana

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,323
40,172
Usalama wa mtu anayetoa pesa kwenye hivi vibanda vya huduma ni mdogo sana.

Leo bi mkubwa alitembelea kibanda kimoja kwa ajili ya kupata huduma ya kutoa salio,na alifanikiwa kutoa kiasi cha mia nane.

Baada ya kupata huduma wakati anatoka katika eneo hilo kama hatua tano hivi, ghafla akatokea kibaka na kunyakua pochi na kukimbia kusikojulikana.

Mbaya zaidi hajamtambua hata sura kwa sababu alikuwa kama vile ameshikwa na bumbuwazi. Baadaye ndio anakumbuka kupiga kelele wakati hata muhusika hajulikani alipo.Alivyonipa taarifa imeniuma sana...lakini nilichoshukuru hakujeruhiwa.

Sasa najiuliza: Katika hali ya namna hiyo ni wangapi wanakwepa hii 'risk' ya kuibiwa pamoja na kujeruhiwa? Na je hivi vibanda vina ulazima wa kuwa na walinzi ili kuzuia wizi wa namna hii?Au baadhi ya vibanda vinashirikiana na wezi/vibaka?
 
Kwanza pole mkuu, ila hio inatokea sana, wanachukua advantage kwamba wamama au wanawake hawawezi kukimbia, pia umakini unahitajika sana
Kweli mkuu,inaumiza sana kwa sababu inarudisha nyuma badala ya kwenda mbele;wasi wasi wangu ni kuwa,inakuwaje maeneo yaleyale ya huduma kifanyike kitu cha namna hiyo...sio kwamba hawa jamaa wanafahamiana?
 
Yeah, pia inawezekana, mm nilikua naenda kuwatolea mwenyewe, wananipa password zao, hatua ya kwanza kwa sasa muambie bimkubwa aende sehemu nyengine kama ipo karibu, yaani abadilishe
Kweli mkuu,inaumiza sana kwa sababu inarudisha nyuma badala ya kwenda mbele;wasi wasi wangu ni kuwa,inakuwaje maeneo yaleyale ya huduma kifanyike kitu cha namna hiyo...sio kwamba hawa jamaa wanafahamiana?
 
Yeah, pia inawezekana, mm nilikua naenda kuwatolea mwenyewe, wananipa password zao, hatua ya kwanza kwa sasa muambie bimkubwa aende sehemu nyengine kama ipo karibu, yaani abadilishe
Ni kweli mkuu,ingawa akili inakuja baada ya kupoteza
 
Alikuwa kashika pochi, huo wizi upo sana hasa sio kwenye hivyo vibanda2 ila kila sehemu upo. Tena masokoni ndio usiseme
 
Mchongo unakuta wanausuka haohao mawakala sometimes....mm nikiwa natoa pesa nyng Kama hyo huwa natoa kwa vibanda viwili tofauti kabisa....Makato mbele kwa mbele
 
Back
Top Bottom