Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 213
Mimi sio mkazi wa eneo la Chuo kikuu cha Dar es salaam , lakini naishi pembeni mwa eneo hilo na muda mwingi sana nakuwa ndani ya eneo la UDSM kwa ajili ya shuguli zangu nyingi zinazonilazimu mimi kuwa katika eneo lile .
Kwa siku za karibuni kumetokea matukio zaidi ya 3 ambayo kwa kweli yanatishia usalama sio wa UDSM pekee bali hata ya majirani wa maeneo yale kama mimi binafsi .
Siku ya jumamosi mchana kama kawaida yangu nilielekea chuoni mchana , lakini kule njiani nilikutana na dimbwi la damu na kibanio cha nywele cha mwanamke , mbele kidogo nikaona chupa ya pombe imepasuka nikajua kuna jambo limetokea .
Ikabidi niende kituo cha polisi kuulizia kulikoni kama wana taarifa zozote za tukio lile , kutuo cha polisi hawajua hata kama kitu kama kile kimetokea ndani ya chuo kikuu tena karibu na kituo cha polisi si unajua polisi walivyo wakaidi ? wakaniomba nisiendelee kuuliza chochote kile .
..
Zamani kidogo niliwahi kupita usiku eneo hilo nikakutana na vijana wakanipa shilingi 500 wakaniambia niende kupanda dala dala nisipite kule kwa sababu kuna shuguli inaendelea ilikuwa zamani sana nilikuwa bado mdogo mdogo kumbe walikuwa wanafanya hivi ?
Basi nikaanza kuulizia ulizia mambo huku mlimani usalama ukoje , nikaambiwa sasa imekuwa ni dili sana vibaka kibao ndani ya chuo na maeneo jirani na hakuna yeyote anayejali kuhusu suala hili kwanza nani atapambana nao wale askari wanaopita pita wote wazee wazee watapambanaje na wahalifu wanaokuja na kuondoka ?
Wiki mbili zilizopita kuna kijana alikuwa anapita toka hall 5 kwenda hall 7 kupitia njia ya kanisani , alikuwa amebeba mkoba wake , alishangaa anaitwa anti alipogeuka tu kisu kikali kikakata mkoba wake na yule kijana akakimbia na ule mkoba ilikuwa saa 5 asubuhi yule dada alipiga kelele weee kila mtu akamshangaa utafikiri wanaangalia ze comedi .
Huyu dada alichunwa na kile kisu kilivyokuwa kikali , katika mkono wake kwahiyo akaendelea kukaa tu vile vile afanye nini mali yake ameshakwenda tena kinguvu ?
..
Sasa taarifa nilizosikia hivi karibuni ni kwamba vijana wa maeneo ya msewe ambayo mimi ni mwenyeji kidogo huko wamepanga kuweka mtego ili waweze kuwakamata watu hawa na kuwauwa kabisa na hili ni jambo la hatari sana kwa wananchi kuamua kuchukua hatua mkononi wanafanya hivi kwa sababu imani yao kwa walinda usalama wa eneo hilo wameshindwa kufanya kazi hiyo ya kuwapa wananchi usalama na uhuru wao sasa sijui itakuwaje ngoja tuone .
Watamchukuwa msichana mrembo wampe simu nzuri ya gharama na kumvalisha mambo mengine halafu awe na mazoea ya kupita pita maeneo yale waone nani atamsogelea au kwenda kujaribu kumpora ndio wafanye kazi yao hao wananchi wenye hasira .
Kwa siku za karibuni kumetokea matukio zaidi ya 3 ambayo kwa kweli yanatishia usalama sio wa UDSM pekee bali hata ya majirani wa maeneo yale kama mimi binafsi .
Siku ya jumamosi mchana kama kawaida yangu nilielekea chuoni mchana , lakini kule njiani nilikutana na dimbwi la damu na kibanio cha nywele cha mwanamke , mbele kidogo nikaona chupa ya pombe imepasuka nikajua kuna jambo limetokea .
Ikabidi niende kituo cha polisi kuulizia kulikoni kama wana taarifa zozote za tukio lile , kutuo cha polisi hawajua hata kama kitu kama kile kimetokea ndani ya chuo kikuu tena karibu na kituo cha polisi si unajua polisi walivyo wakaidi ? wakaniomba nisiendelee kuuliza chochote kile .
..
Zamani kidogo niliwahi kupita usiku eneo hilo nikakutana na vijana wakanipa shilingi 500 wakaniambia niende kupanda dala dala nisipite kule kwa sababu kuna shuguli inaendelea ilikuwa zamani sana nilikuwa bado mdogo mdogo kumbe walikuwa wanafanya hivi ?
Basi nikaanza kuulizia ulizia mambo huku mlimani usalama ukoje , nikaambiwa sasa imekuwa ni dili sana vibaka kibao ndani ya chuo na maeneo jirani na hakuna yeyote anayejali kuhusu suala hili kwanza nani atapambana nao wale askari wanaopita pita wote wazee wazee watapambanaje na wahalifu wanaokuja na kuondoka ?
Wiki mbili zilizopita kuna kijana alikuwa anapita toka hall 5 kwenda hall 7 kupitia njia ya kanisani , alikuwa amebeba mkoba wake , alishangaa anaitwa anti alipogeuka tu kisu kikali kikakata mkoba wake na yule kijana akakimbia na ule mkoba ilikuwa saa 5 asubuhi yule dada alipiga kelele weee kila mtu akamshangaa utafikiri wanaangalia ze comedi .
Huyu dada alichunwa na kile kisu kilivyokuwa kikali , katika mkono wake kwahiyo akaendelea kukaa tu vile vile afanye nini mali yake ameshakwenda tena kinguvu ?
..
Sasa taarifa nilizosikia hivi karibuni ni kwamba vijana wa maeneo ya msewe ambayo mimi ni mwenyeji kidogo huko wamepanga kuweka mtego ili waweze kuwakamata watu hawa na kuwauwa kabisa na hili ni jambo la hatari sana kwa wananchi kuamua kuchukua hatua mkononi wanafanya hivi kwa sababu imani yao kwa walinda usalama wa eneo hilo wameshindwa kufanya kazi hiyo ya kuwapa wananchi usalama na uhuru wao sasa sijui itakuwaje ngoja tuone .
Watamchukuwa msichana mrembo wampe simu nzuri ya gharama na kumvalisha mambo mengine halafu awe na mazoea ya kupita pita maeneo yale waone nani atamsogelea au kwenda kujaribu kumpora ndio wafanye kazi yao hao wananchi wenye hasira .