Wadau mimi binafsi na ninaamini wakazi wengi wa jiji la Dar wanakerwa na vitendo vya kihalifu ambavyo vimekuwa kwa kasi kubwa. Watu wanakabwa na kunyang'anywa magari kama vile wizi wa simu; watu wanaumizwa na kuuawa kila siku; watu wanaibiwa kibabe hasa kwenye mataa ya ubungo kwa kung'olewa site mirrors kwenye magari yao bila msaada wa polisi; na miezi kadhaa watu walikuwa wanakabwa sana kwenye daraja la salender karibu kabisa na kituo cha polisi. Watu wanaogopa hata kwenda kwenye shughuli za kijamii wakihofia kukabwa au kuvamiwa magetini mwao wanaporudi.
Majambazi wana confidence ya ajabu, wanashika silaha na kuwaua wananchi bila kusikia lolote toka kwa kina Kova, Lukuvi na viongozi wengine. Waziri wa Mambo ya Ndani amekuwa kama picha tu, kwani hatumsikii hata kidogo hadi nasahau kama kuna hiyo wizara hapa nchini. Jeshi nalo linaongoza kwa kushirikiana na majambazi, watu wanavamiwa usiku, polisi wanapigiwa lakini response inajitokeza baada ya masaa mawili kwa kigezo cha kupotea njia.
Tunakwenda wapi jamani; watu tunaishi kama tuko kwenye nchi yenye vita..!! Wasiwasi tele, ukitembea barabarani huna amani, ukifika nyumbani kwako huna amani, utafikiri hatuna serikali. Kama kuna mdau anafahamiana na kina Kova na Mwema, awaambie wafanye kazi ya ziada kwani wimbi la ujambazi limezidi sasa.
Kuna mdau kaniarifu kuwa leo asubuhi kwenye Power Breakfast kuwa kuna familia imevamiwa na baba wa familia hiyo ameuawa kinyama na majambazi. Tumesikia mengi yakiwemo ya kina Prof. Mwaikusa. Sidhani kama kuna u-seriousness kwenye usalama wa raia.
Hali inatisha...!! Naomba kuwasilisha hoja wadau.
Majambazi wana confidence ya ajabu, wanashika silaha na kuwaua wananchi bila kusikia lolote toka kwa kina Kova, Lukuvi na viongozi wengine. Waziri wa Mambo ya Ndani amekuwa kama picha tu, kwani hatumsikii hata kidogo hadi nasahau kama kuna hiyo wizara hapa nchini. Jeshi nalo linaongoza kwa kushirikiana na majambazi, watu wanavamiwa usiku, polisi wanapigiwa lakini response inajitokeza baada ya masaa mawili kwa kigezo cha kupotea njia.
Tunakwenda wapi jamani; watu tunaishi kama tuko kwenye nchi yenye vita..!! Wasiwasi tele, ukitembea barabarani huna amani, ukifika nyumbani kwako huna amani, utafikiri hatuna serikali. Kama kuna mdau anafahamiana na kina Kova na Mwema, awaambie wafanye kazi ya ziada kwani wimbi la ujambazi limezidi sasa.
Kuna mdau kaniarifu kuwa leo asubuhi kwenye Power Breakfast kuwa kuna familia imevamiwa na baba wa familia hiyo ameuawa kinyama na majambazi. Tumesikia mengi yakiwemo ya kina Prof. Mwaikusa. Sidhani kama kuna u-seriousness kwenye usalama wa raia.
Hali inatisha...!! Naomba kuwasilisha hoja wadau.