Usalama Barabarani - Morogoro, Je hili nalo linamtaka Lugola kutolea Tamko!?

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,814
33,178
Ndugu wanajamvi:

Katika pitapita yangu na mwenyeji wangu leo usiku huko mji kasoro bahari nimekutana na hali ambayo kikosi cha usalama barabarani hawatakiwi kusubiri tamko la Rais au Waziri ili kuongeza usalama kwa abiria wanaotumia barabara wakati wa usiku.

Daladala zinafanya safari usiku zikiwa na abiria lakini hazina taa, na zingine zina taa moja mbele, kiasi kwamba unapopishana nazo utadhani ni pikipiki, na zilizo nyingi hazina kabisa indicators wala taa za kuashiria gari linasimama,

Kwa jinsi nilivyoona, tatizo hili ni rahisi sana kulifuatilia ama kwa kufanya ukaguzi wakati mabasi husika yakiwa katika stand ya kupakilia abiria au kwa kuitisha ukaguzi kama ilivyo wakati wa kutoa stika za wiki ya usalama barabarani.

Nawasilisha
 

Attachments

  • IMG-20180924-WA0002.jpg
    IMG-20180924-WA0002.jpg
    9.6 KB · Views: 38
  • VID-20180924-WA0001.mp4
    1.3 MB · Views: 28
Ndugu wanajamvi:

Katika pitapita yangu na mwenyeji wangu leo usiku huko mji kasoro bahari nimekutana na hali ambayo kikosi cha usalama barabarani hawatakiwi kusubiri tamko la Rais au Waziri ili kuongeza usalama kwa abiria wanaotumia barabara wakati wa usiku.

Daladala zinafanya safari usiku zikiwa na abiria lakini hazina taa, na zingine zina taa moja mbele, kiasi kwamba unapopishana nazo utadhani ni pikipiki, na zilizo nyingi hazina kabisa indicators wala taa za kuashiria gari linasimama,

Kwa jinsi nilivyoona, tatizo hili ni rahisi sana kulifuatilia ama kwa kufanya ukaguzi wakati mabasi husika yakiwa katika stand ya kupakilia abiria au kwa kuitisha ukaguzi kama ilivyo wakati wa kutoa stika za wiki ya usalama barabarani.

Nawasilisha
Kinga ni bora kuliko tiba
 
Tatizo siyo askali tatizo ni viongozi wa siasa askali wakikagua magari taa wanasiasa wanasema askali wanakagua garii taa mchana za nini sasa askali apo anakosa gani
 
Madereva watamaliza watanzania

Upo sahihi lakini abiria wengi wa Tanzania nao wana matatizo mno, na kwa kiwango kikubwa ndiyo chanzo cha ajali nyingi...hawajui haki zao, dereva anakimbiza gari wao ni kimya hawamtahadharisha dereva na mmoja akifanyas hivyo wengine wanakuwa upandewa dereva...abiria wanajazana kwenye mabasi utadhani magunia...ifike wakati abiria waliozidi kwenyemabasi na ambao wamesimama nao wapigwe faqini ya sh. laki tatu...kwenye mabasi ya mwendo kasi ndiyo shida yanajaza kama mizigo ya dagaa.....
 
Upo sahihi lakini abiria wengi wa Tanzania nao wana matatizo mno, na kwa kiwango kikubwa ndiyo chanzo cha ajali nyingi...hawajui haki zao, dereva anakimbiza gari wao ni kimya hawamtahadharisha dereva na mmoja akifanyas hivyo wengine wanakuwa upandewa dereva...abiria wanajazana kwenye mabasi utadhani magunia...ifike wakati abiria waliozidi kwenyemabasi na ambao wamesimama nao wapigwe faqini ya sh. laki tatu...kwenye mabasi ya mwendo kasi ndiyo shida yanajaza kama mizigo ya dagaa.....


Nadhani kazi ya kutoa elimu kwa umma ilipaswa kufanywa na mamlaka inayosimamia masuala ya usafir,i kama sijakose SUMATRA ndiyo wanahusika sana, binafsi ningependekeza wangekuwa na recorded programs za kutoa elimu kwa wasafiri, badala ya kusikiliza na kutazama bongo movies na miziki ya nusu uchi, waweke cds zenye mafuzo ya haki za msafiri ili madereva wajue kuwa abiria nao wanajua haki zao, lakini kwa hali ilivyo wakati mwingi wanawasahaulisha kwa kuwawekea hizo videos
 
Tatizo siyo askali tatizo ni viongozi wa siasa askali wakikagua magari taa wanasiasa wanasema askali wanakagua garii taa mchana za nini sasa askali apo anakosa gani

Kweli hapo shida tupu, ni kama kusema kwanini gari liwe na wind screen kama mtu anaendesha gari siku ambazo hakuna upepo au mvua
 
Mjomba nch yetu wanasiasa ndo wana alibu kila kitu ndugu yangu wanajifanya waho ndo askali wao ndo mahakim yan daaaaaaa
 
Nadhani kazi ya kutoa elimu kwa umma ilipaswa kufanywa na mamlaka inayosimamia masuala ya usafir,i kama sijakose SUMATRA ndiyo wanahusika sana, binafsi ningependekeza wangekuwa na recorded programs za kutoa elimu kwa wasafiri, badala ya kusikiliza na kutazama bongo movies na miziki ya nusu uchi, waweke cds zenye mafuzo ya haki za msafiri ili madereva wajue kuwa abiria nao wanajua haki zao, lakini kwa hali ilivyo wakati mwingi wanawasahaulisha kwa kuwawekea hizo videos

Miongoni mwa makosa makubwa ya serikali ni kuisahau hii sekta ya usafirishaji au uchukuzi ambapo eti kinachoitwa ni 'private sector' ndiyo inaendesha sekta hii ya uchukuzi na hasa kwa abiria...Nasema ni kosa kubwa kwa kuwa sekta hii imeachwa kwa wahuni na ambao ndio wanaoiendesha...wahuni hawa ni wavuta unga, wapiga debe, mateja vituoni na kadhalika...yaani sekta inaendeshwa na mateja, wavuta bangi katika vituo vyote vya mabasi nchini...ukipanda public transport ndipo utauona ukweli huu...utawaona na kuwasikia wapiga debe wakibwatuka 'ngoja apande huyo'...makonda ndiyo hivyo kwenye mabasi utawasikia haya mliosimama misitari miwili miwili , wewe mama pale geukia kule na kadhalika...hawajali hata maumbile ya watu, wanawapanga watu kwenye daladala kama magunia...yaani makonda na madereva wa dalaladala ni wahuni, nguo zao chafu, hawana heshima wala nidhamu kwa abiria...wanawakaripia abiria utadhani abiria hawalipi nauli...viongozi wa serikali hawalioni hili kwa kuwa wengi wao wanatembelea magari ya kifahari, lakini thousands and thousands of people ndio wanaotumia public transport yaani daladala mijini...serikali kimya haifanyi kitu...vituoni magari au daladala ziko nyingi lakini vituo vimetekwa na wahuni, wavuta bangi ambao ndio wanao-control magari yaondoke au yasiondoke...yaani daladala zinaondoka kwa zamu kwa amri ya wapiga debe kwa ujira wa sh. 500 hadi 1,000 kwa kila gari...wanacreate scarcity ya daladala wakati ambapo daladala ni nyingi.serikali ipo na hailioni hili...ukifika kituo cha Mbezi ndipo utashuhudia uchuro na nguvu ya wapiga debe...vituo vya buguruni ni hivyo hivyo...Yaani ni ajabu na kweli...mabasi ya mwendo kasi ilionekana pengine ni suluhisho lakini kimsingi ndiyo hovyo kabisa kwa kujaza abiria kuliko hata daladala...ulaya yapo mwendo kasi lakini hayajazi kama haya ya kwetu....ipo siku itatokea balaa kubwa.sana kwenye mwendo kasi ..hakuna usalama kabisa...gaidi akiingia kwenye mwendo kasi na kufanya yake nidpo serikali pengine itakaposhituka...
 
Nimejiuliza ule usimamishaji wa magari mchana huwa wanakagua nini kama siyo haya mambo ya uwepo wa taa, nchi za wenzetu, mtu hadiriki kuendesha chombo chenye ualakini kwasababu anajua kwanza anaji endanger mwenyewe
Hizo daladala bubu hazitembei mchana mkuu ni usiku kwa usiku tu
 
Hizo daladala bubu hazitembei mchana mkuu ni usiku kwa usiku tu


Nani mwenye wajibu wa kulisimamia hilo, maana maafa hayachagui aina ya daladala, imagine semi trailer imetungua toka huko ghafla inaikuta hiyo daladala ghafla barabrani, kitakachotokea ni kuigonga
 
Miongoni mwa makosa makubwa ya serikali ni kuishau hii sekta ya usafirishaji au uchukuzi ambapo eti kinachoitwa ni 'private sector' ndiyo inaendesha sekta hii ya uchukuzi na hasa kwa abiria...Nasema nin kosa kubwa kwankuwa sekta hii imeachwa kwa wahuni na ambao ndio wanaoiendesha...wahuni hawa ni wavuta unga, wapiga debe, mateja vituoni na kadhalika...yaani sekta inaendeshwa na mateja, wavuta bangikatika vituo vyote vya mabasi nchini...ukipanda public transport ndipo utauona ukweli huu...utawaona na kuwasikia wapiga debe wakibwatuka ngoja apande huyo...makonda ndiyo hivyo kwenye mabasi utawsikia haya mliosimama misitari miwili miwili , wewe mama pale geukia kule! na kadhalika...hawajali hata maumbile ya watu, wanawapanga watu kwenye dalala kama magunia...yaani makonda na madereva wa dalaladala ni wahuni, nguo zao chafu, hawana heshima wala nidhamu kwa abiria...wanawakaripia abiria utadhani abiria hawalipi nauli...viongozi wa serikali hawalioni hili kwa kuwa wengi wao wanatembelea magari ya kifahari, lakini thousands and thousands of people ndio wanaotumiapublic transport yaani daladala mijini...serikali kimya haifanyi kitu...vituoni magari au daladala ziko nyingi lakini vituo vimetekwa na wahuni, wavuta bangi ambao ndio wanao-control magari yaondoke au yasiondoke...yaani daladala zinaondoka kwa zamu kwa amri ya wapiga debe kwa ujira wa sh. 500 hadi 1,000 kwa kila gari...wanacreate scarcity ya daladala wakati ambapo daladala ni nyingi.serikali ipo na hailioni hili...ukifika kituo cha Mbezi ndipo utashuhudia uchuro na nguvu ya wapiga debe...vituo vya buguruni ni hivyo hivyo...Yaani ni ajabu na kweli...mabasi ya mwendo kasi ilionekana pengine ni sulihisho lakini kimsingi ndiyo hovyo kabisa kwa kujaza abiria kuliko hata daladala...ulaya yapo mwendo kasi lakini hayajazi kama haya ya kwetu....ipo siku itatokea balaa kubwa.sana kwenye mwendo kasi ..hakuna usalama kabisa...gaidi akiingia kwenye mwendo kasi na kufanya yake nidpo serikali pengine itakaposhituka...


Mkuu umechambua kwa kina kabisa na ni ukweli mtupu, naafikiana nawe 100%, kinachotugharimu ni hao wenye kusimamia sheria ndiyo haohao wenye daladala na ndiyo hao walktakiwa kuzuia madawa ya kulevya lakini wamestarehe na ndiyo haohao wanao waweka mateja kazini
 
Ukifuatilia kwa karibu unaweza kuona wamiliki wa magari hayo ni askari wenye jukumu la ukaguzi au ndugu au jamaa zao wa karibu
Hujakosea ndivyo ilivyo na huwa hazikaguliwi,unaweza ukalimwa faini wewe mwenye weipa kipisi nyuma,lakini daladala haina taa za nyuma wanaiangali na kumpungia mkono konda
 
Hujakosea ndivyo ilivyo na huwa hazikaguliwi,unaweza ukalimwa faini wewe mwenye weipa kipisi nyuma,lakini daladala haina taa za nyuma wanaiangali na kumpungia mkono konda


Bado tuna safari ndefu mkuu, mhubiri mmoja amezungumzia mfumo wa kuformat kabisa ubongo na kuufanyia full new software installation kuondoa mentality zinazotusumbua na kutucheleweshea maendeleo
 
Kama nimemuelewa vizuri mtoa mada,anasena kuna magari mabovu yanafanya kazi ya kusafirisha abiria na mizigo wakati was usiku katika barabara ya dar/Moro.
Hili tatizo lipo hadi hapa mjini wakati ea usiku yanajitokeza magari mabovu wakati wa usiku hadi alfajiri yanapisitisha shughuli zake kusubili usiku mwingine.
Hapa swali LA msingi ni kuwa trafiki wanapaswa kufanya Nazi masaa 24 kama wezao ?
Mini kinasababisha trafiki kufanya kazi mpaka saa mbili usiku,kishaa kuacha barabara zikirawaliwa na magari mabovu,?
Kwa nini wasipeane shift kama was vituoni?
 
Wanasubiri ajali/maafa,then rambirambi,per diem,ubani,nk.. Namwomba Mungu aepushe
 
Back
Top Bottom