Usajili wa simcard kwa vidole imekuwa nongwa

Shoctopus

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
3,434
1,985
Nakumbuka niliponunua line ya Airtel mara ya mwisho nilipigwa picha kwa usajili.

Sasa nasikia hii haitoshi, lazima nisajili tena kwa kidole.

Wamesema kutosajili kwa kidole ni kosa (la jinai). Adhabu yake ni faini ya shilingi milioni au kifungo jela miezi sita au vyote!

Ajabu hapa ni kwamba wahusika sio kwamba hawanijui kwa majina yangu, umri na sura au kama hawanijui labda kwa kidole changu tu, sio sura nk! Kwasababu kidole peke yake bila jina, sura, umri kinatosha?

Yaani kwa wahusika kukosa alama ya kidole changu ninastahili kwenda jela?

Hamjasikia mtu amezaliwa bila mikono. Sasa huyo mtamsweka jela kwa kukosa alama ya kidole au simu kwake ni marufuku?

Hivi tumewakoseeni nini hadi kustahili manyanyaso usiku na mchana mwaka mzima?

Tunawezaje kuishi kwa amani na furaha kama mnatutesa kwa kutunyima haki zetu kwakuwa tumeshazeeka, halafu tuishi kwa vitisho kwa kutosajili simu kwa kidole tu?

Sisi ndio tumekula matrilioni ya fedha za nchi au tumegeuka watuhumiwa wa ugaidi?

Kuna watu wanapenda kutuchonganisha na Serikali bila sababu za msingi.

Hakuna mtu mwenye akili timamu atapinga zoezi la kusajili kwa kidole. Ila kila mtu ana sababu zake kutokamilisha usajili, baadhi ya hizo sababu wahusika wanazijua. Hii mambo ya deadline na vitisho ili iweje?

Kila siku watu wananunua simu na huwezi kusema mwisho wa kununua simu ni December 31, baada ya hapo hamtasajili simu kwa vidole?
 
Mkuu unastahili tuzo ya ulalamikaji mpk unatia huruma!!.. ujumbe wako ni dhahiri kwa kukazia tu ni Hivyo vitambulisho vya nida hili zoezi linavyoendeshwa sijui ni ktk namna gani upatikanaji wake tabu hlf mwisho wa hayo alama vidole ati mwezi wa 12!! Yajayo yanafurahisha
 
Pamoja na kuwa na alama za vidole, wanataka pia ukipoteza hiyo line, lazima uende polis upange foleni ulipie loss report
 
Voda kwani si nasikia matangazo yao unaweza kusajili kwa vidole na kitambulisho chochote ila hadi mwezi huu mwishoni na baada ya hapo lazima utumie nida id
 
zoezi hili awali ilikuwa mwisho mwezi mei 2019 kama sijakosea lakini rais JPM akaongeza muda hadi mwezi disemba kwa kigezo kwamba vitambulisho vya utaifa ambavyo ndio pekee vinatumika kusajili line wanavyo watanzania wachache sana.

nashukuru Mungu nimeweza kukamilisha usajili kwa line zangu mbili ninazotumia( voda na tigo).
ni zoezi ambalo halichukui muda mrefu hasa pale voda, namba za kitambulisho cha utaifa na namba ya simu ndio vinahitajika.
tigo kidogo nilikaa sababu network yao ilikuwa chini siku hiyo.

ni vema sote tuende kukamilisha zoezi hilo, na kwa jinsi nilivyoelewa deadline kwa sisi wateja wa muda mrefu.
kwa wateja wapya baada ya deadline hautaweza kutumia line yako bila kusajiliwa kikamilifu baada.

na line ikipotea kwenda polisi ili kujilinda wewe mwenyewe, kisije kikakutwa eneo la criminal case ukahusishwa.
mfano kadi za benki tunaripoti polisi na benki kusudio lake ni kwamba, kuanzia muda ule ambao benki na polisi wana taarifa ukitokea wizi wowote wa pesa kwenye kadi yako ya benki UTALIPWA NA BENKI.
 
Nyie ndio wezi wa mitandao, nenda kasajili line, maana huko tunakokwenda unakuwa hautumii tena namba ya siri kufanya manunuzi, ni unatumia finger print kwenye simu zenye finger print sensor
 
General Akudo,
Nia ya kusajili inaweza kuwa nzuri lakini uendeshaji zoezi umekuwa complicated bila sababu yoyote. Kuna njia rahisi kabisa za kufanikisha hili na bila kuifanya ni kama tutakuwa tunahangaisha watu na kupoteza mali na muda. Bila kuwa na database ya raia na wakazi wa nchi kwa ujumla ni bure. Kwenye database kuwa na data zote za watu eg jina, picha, fingerprints nk. Ni hatari sana kutumia watu mitaani kuchukuwa fingerprints za watu. Madhara yake yatakuja kujitokeza wakati tumeshachelewa.
 
Vitambulisho vyenyewe havipo kwa watu wote.hapo inakuwaje?Halafu wakati tulipokuwa tunasajili walitusambazia mawakala mpaka vijijini.leo kusajili kwa kidole uwafuate ofisini.sijui huyu kikongwe mliemsajilia huko kijijini MNAMSAIDIAJE??
 
Ni vigumu sana sana kwa watu kukuelewa ulichosema. Watu wameshazoea kuonewa na kuchukulia kila huduma ni kwa kuhurumiwa na kwa kuteseka. It turns out hiyo ndiyo furaha ya watoa watoa maagizo na watoa huduma. Gives them a chance to exercise their powers and control. Na wananchi nao bila kunyanyaswa kidogo every now and then inawafanya washituke kuwa kuna kitu si cha kawaida katika maisha yao ya kila kitu. Nao inawapa pia nafasi ya kitu cha kulalamikia na kujisikia unyonge. This is psychological and it has been embedded onto citizens minds since decades ago.
 
Back
Top Bottom