Mk54
JF-Expert Member
- Dec 29, 2016
- 1,997
- 3,933
Pamoja na kutolewa kwenye michuano ya Club Bingwa Africa, wa TZ wote tunapaswa kuipongeza The Msimbazi Reds katika jitahada za dhati walizoonesha kwenye michuano hiyo. Aidha, Pongezi za dhati ziende kwa Muhammad Dewji kwa kuleta mabadiliko yenye tija kwa kipindi kifupi sana alichochukua timu.
Kitu pekee ambacho wa TZ tumeshindwa kuelewa ni kwamba Mpira ni KAZI, kama kazi nyingine. Mziki ni KAZI kama kazi nyingine.
Kama mnakumbuka vizuri Kocha wa Tout Puisant alisema pale Taifa ya kwamba,
“Sisi kwetu mpira ni kazi, hapana mchezo mchezo na tumekuja kuifundisha SSC nidhamu ya mpira”
1. Mchezaji Medie Kagere analipwa Mil 15 kwa mwezi, na tayari Js Soura ya Al jazairi( Algérie ) wameshaonesha matamanio ya kumchukua.
2. Immanuel Okwi analipwa kati ya 12mil au 13 mil kwa mwezi. Imagine that. It’s a lot of money my friend kwa TZ!
Tayari wachezaji kama 4 kutoka SSC aliwemo Manula wameshatamaniwa na Klabu mbali mbali ikiwemo AS Vita, Les Armés!
Mchezaji Jean Marc Makusu Mundele wa As Vita ambaye ameuzwa Morocco atakuwa analipwa Mil 80 kwa mwezi, As Vita walikuwa wakimlipa Mil 30 kwa mwezi.
SSC walikuwa wanamnyemelea huyu jamaa lakini mambo ya msingi aliyauliza yeye mwenyewe kwa kujadili na Kocha wake
1. Je The Msimbazi Reds wataweza kunilipa zaidi ya Mil 30 kwa mwezi plus na pesa ya kuvunja mkataba ambayo ilikuwa inakaribia kufika 1 bil?
2. Kama namba 1 ni Yes, je naenda kucheza na nani huko ? Alitaka kujua plan ya Simba ya kuchukua baadhi ya wachezaji wenye Level kama yake ambao watakuwa kwenye Klabu.
Mchezaji kama Chama, Medie, Niyonzima hawa ni wachezaji wazuri sana, lakini je wachezeshwa na nani? Wanachezashwa na Level ya Bocco, hivyo nawao inabidi washushe kiwango chao ili waendane na Bocco na hii ndiyo changamoto kubwa hasa zikija International games.
Mo aliweka bayana kuwa katika usajili ujao, kutakuwa na a lot of changes ikiwa ni pamoja na kuwaaacha baadhi ya wachezaji kwenye usajili mpya.
Hivyo,
1. Usajili wa SSC uangalie Requirements( Mahitaji) ya timu. Kama timu inahitaji kucheza nusu fainali ya Club Bingwa Africa, isajili wachezaji ambao watakuwa na uwezo wa kuifikisha timu huko. Wachezaji ambao wanachukulia mpira kama KAZI, sio kina Mkude wanaoenda kulewa lewa mapombe, mazoezini hawatokei. Hawa ni Makapi. Ban Them!
2. Kuepuka Madalali, Mo anatakiwa kusimamia usajili yeye mwenyewe kwa kushirikiana na kamati maalumu. Game alizocheza mchezaji na uwezo wake akiwa uwanjani, na nidhamu pia. Sio kumuokota mtu huko Ivory Coast halafu majaribio yake ni kupiga danadana, ni Ukichaa, wacheni hiyo kitu.
3. Kuacha usajili wa kukomoana kati ya SSC na Vyura, kwa wachezaji wa ndani, Mchezaji asajiliwe kutokana na uwezo wake, mpira ni business, it’s time now to be serious.
4. Defence na Midfield ni changamoto kwa SSC, honestly. Kwa yakini kwa mwaka huu, Tout Puisant Mazembe hawana kikosi kizuri na trust me, hawatofika mbali, hawatoweza kuchukua kombe mwaka huu.
Wametufungwa kwa ubovu wa defence na midfield. Na kama robo fainali ingekuwa kati Mazembe Vs As Vita, kuna asilimia zaidi ya 60 kuwa Mazembe angetoka.
Usajili wa Simba uangalie sana hili eneo ikiwa ni pamoja Na kuwaweka wachezaji wenye level zinazokaribiana wakishirikiana na hawa wa nyumbani level za kina Bocco.
5. Kama kuna mtu aliangalia gemu ya Al ahly na Mamelodi, waarabu walifikia hatua wanataka kurusha ngumi. Kila wakifika kwenye defence za mamelodi, hakupitiki.it was very tough game, wachezaji wa mamelodi wamekaa Muda mrefu na wamezoeana.
Simba iangalie uwezekano wa kuwasajili wachezaji kwa mikataba mirefu ili wachezaji wakae pamoja kwa muda na kuleta tija kwenye kikosi.
6. Training.
Wachezaji wa SSC wanakosa spirit kwenye game za ugenini. Kuwe na training ambayo itatoa mafunzo ya nidhamu, kuheshimu kazi, Spirit ya ku fight kwenye game, kujiamini na jinsi gani ya ku behave kimataifa. Hii ni kitu muhimu sana kwa sababu wachezaji wetu wengi hawana EXPOSURE na MENTAL STRENGH.
Thank You!
———————————
Jumatatu 15, Aprili 2019.
Kitu pekee ambacho wa TZ tumeshindwa kuelewa ni kwamba Mpira ni KAZI, kama kazi nyingine. Mziki ni KAZI kama kazi nyingine.
Kama mnakumbuka vizuri Kocha wa Tout Puisant alisema pale Taifa ya kwamba,
“Sisi kwetu mpira ni kazi, hapana mchezo mchezo na tumekuja kuifundisha SSC nidhamu ya mpira”
1. Mchezaji Medie Kagere analipwa Mil 15 kwa mwezi, na tayari Js Soura ya Al jazairi( Algérie ) wameshaonesha matamanio ya kumchukua.
2. Immanuel Okwi analipwa kati ya 12mil au 13 mil kwa mwezi. Imagine that. It’s a lot of money my friend kwa TZ!
Tayari wachezaji kama 4 kutoka SSC aliwemo Manula wameshatamaniwa na Klabu mbali mbali ikiwemo AS Vita, Les Armés!
Mchezaji Jean Marc Makusu Mundele wa As Vita ambaye ameuzwa Morocco atakuwa analipwa Mil 80 kwa mwezi, As Vita walikuwa wakimlipa Mil 30 kwa mwezi.
SSC walikuwa wanamnyemelea huyu jamaa lakini mambo ya msingi aliyauliza yeye mwenyewe kwa kujadili na Kocha wake
1. Je The Msimbazi Reds wataweza kunilipa zaidi ya Mil 30 kwa mwezi plus na pesa ya kuvunja mkataba ambayo ilikuwa inakaribia kufika 1 bil?
2. Kama namba 1 ni Yes, je naenda kucheza na nani huko ? Alitaka kujua plan ya Simba ya kuchukua baadhi ya wachezaji wenye Level kama yake ambao watakuwa kwenye Klabu.
Mchezaji kama Chama, Medie, Niyonzima hawa ni wachezaji wazuri sana, lakini je wachezeshwa na nani? Wanachezashwa na Level ya Bocco, hivyo nawao inabidi washushe kiwango chao ili waendane na Bocco na hii ndiyo changamoto kubwa hasa zikija International games.
Mo aliweka bayana kuwa katika usajili ujao, kutakuwa na a lot of changes ikiwa ni pamoja na kuwaaacha baadhi ya wachezaji kwenye usajili mpya.
Hivyo,
1. Usajili wa SSC uangalie Requirements( Mahitaji) ya timu. Kama timu inahitaji kucheza nusu fainali ya Club Bingwa Africa, isajili wachezaji ambao watakuwa na uwezo wa kuifikisha timu huko. Wachezaji ambao wanachukulia mpira kama KAZI, sio kina Mkude wanaoenda kulewa lewa mapombe, mazoezini hawatokei. Hawa ni Makapi. Ban Them!
2. Kuepuka Madalali, Mo anatakiwa kusimamia usajili yeye mwenyewe kwa kushirikiana na kamati maalumu. Game alizocheza mchezaji na uwezo wake akiwa uwanjani, na nidhamu pia. Sio kumuokota mtu huko Ivory Coast halafu majaribio yake ni kupiga danadana, ni Ukichaa, wacheni hiyo kitu.
3. Kuacha usajili wa kukomoana kati ya SSC na Vyura, kwa wachezaji wa ndani, Mchezaji asajiliwe kutokana na uwezo wake, mpira ni business, it’s time now to be serious.
4. Defence na Midfield ni changamoto kwa SSC, honestly. Kwa yakini kwa mwaka huu, Tout Puisant Mazembe hawana kikosi kizuri na trust me, hawatofika mbali, hawatoweza kuchukua kombe mwaka huu.
Wametufungwa kwa ubovu wa defence na midfield. Na kama robo fainali ingekuwa kati Mazembe Vs As Vita, kuna asilimia zaidi ya 60 kuwa Mazembe angetoka.
Usajili wa Simba uangalie sana hili eneo ikiwa ni pamoja Na kuwaweka wachezaji wenye level zinazokaribiana wakishirikiana na hawa wa nyumbani level za kina Bocco.
5. Kama kuna mtu aliangalia gemu ya Al ahly na Mamelodi, waarabu walifikia hatua wanataka kurusha ngumi. Kila wakifika kwenye defence za mamelodi, hakupitiki.it was very tough game, wachezaji wa mamelodi wamekaa Muda mrefu na wamezoeana.
Simba iangalie uwezekano wa kuwasajili wachezaji kwa mikataba mirefu ili wachezaji wakae pamoja kwa muda na kuleta tija kwenye kikosi.
6. Training.
Wachezaji wa SSC wanakosa spirit kwenye game za ugenini. Kuwe na training ambayo itatoa mafunzo ya nidhamu, kuheshimu kazi, Spirit ya ku fight kwenye game, kujiamini na jinsi gani ya ku behave kimataifa. Hii ni kitu muhimu sana kwa sababu wachezaji wetu wengi hawana EXPOSURE na MENTAL STRENGH.
Thank You!
———————————
Jumatatu 15, Aprili 2019.