Usajili wa Bernard Morrison kurudi Yanga, kuna mvutano mkali unaendelea!

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Jana hata kabla ya Simba kutoa taarifa kuhusu kumsimamisha Bernard Morrison nilieleza kuwa mchezaji huyo amesimamishwa kwa sababu ya utovu wa nidhamu kwa kile kilichodaiwa kuwa alitoroka kambini.

Baadaye Morrison akapost kwenye pages zake kuwa kuna kitu kikubwa kinakuja akiwa ameweka picha ameshika mabegi kama mtu anayesafiri.

Sasa taarifa za ndani ya Simba zinaeleza kuwa klabu hiyo haina mpango wa kuendelea kuwa na mchezaji huyo, hivyo wanachosubiri ni kumalizika kwa mkataba wake ambao umesalia miezi mitano, kisha wamalizane naye kwa kuwa hajaonyesha uwezo walioutarajia.

Mbali na hapo inaelezwa kuwa kuna kigogo wa Klabu ya Yanga yupo tayari kusimamia shoo ili mchezaji huyo arejee Jangwani, jambo ambalo limewagawa baadhi ya viongozi.

Kwa hatua iliyopo ni kuwa Morrison anaweza kufanya mazungumzo na klabu nyingine yoyote kwa kuwa kanuni inamruhusu na ikiwezekana kusaini mkataba wa awali.

Hakuondoka Yanga vizuri, hiyo ni hoja ya baadhi ya viongozi wanaopinga kurejea kwake klabuni hapo wakionekana watakuwa wanamrudisha mtu aliyewakosea heshima, lakini wale wanaounga mkono kurejea kwake wanataka arejee ili wawaumize wapinzani wao wa jadi, Simba.

Hivyo, ni suala la muda kusubiri nini kitatokea, Simba wapo kwenye presha ya matokeo na kiwango bora, je, wataendelea kumfikiria Morrison au watapuuzia na kumuacha akiondoka ikiwezekana kwenda Yanga kirahisi? Muda utazungumza ila suala la Morrison kuondoka Simba hilo halikwepeki kwa sasa.
 
Jana hata kabla ya Simba kutoa taarifa kuhusu kumsimamisha Bernard Morrison nilieleza kuwa mchezaji huyo amesimamishwa kwa sababu ya utovu wa nidhamu kwa kile kilichodaiwa kuwa alitoroka kambini.

Baadaye Morrison akapost kwenye pages zake kuwa kuna kitu kikubwa kinakuja akiwa ameweka picha ameshika mabegi kama mtu anayesafiri.

Sasa taarifa za ndani ya Simba zinaeleza kuwa klabu hiyo haina mpango wa kuendelea kuwa na mchezaji huyo, hivyo wanachosubiri ni kumalizika kwa mkataba wake ambao umesalia miezi mitano, kisha wamalizane naye kwa kuwa hajaonyesha uwezo walioutarajia.

Mbali na hapo inaelezwa kuwa kuna kigogo wa Klabu ya Yanga yupo tayari kusimamia shoo ili mchezaji huyo arejee Jangwani, jambo ambalo limewagawa baadhi ya viongozi.

Kwa hatua iliyopo ni kuwa Morrison anaweza kufanya mazungumzo na klabu nyingine yoyote kwa kuwa kanuni inamruhusu na ikiwezekana kusaini mkataba wa awali.

Hakuondoka Yanga vizuri, hiyo ni hoja ya baadhi ya viongozi wanaopinga kurejea kwake klabuni hapo wakionekana watakuwa wanamrudisha mtu aliyewakosea heshima, lakini wale wanaounga mkono kurejea kwake wanataka arejee ili wawaumize wapinzani wao wa jadi, Simba.

Hivyo, ni suala la muda kusubiri nini kitatokea, Simba wapo kwenye presha ya matokeo na kiwango bora, je, wataendelea kumfikiria Morrison au watapuuzia na kumuacha akiondoka ikiwezekana kwenda Yanga kirahisi? Muda utazungumza ila suala la Morrison kuondoka Simba hilo halikwepeki kwa sasa.
Asirudi Yanga aslani.
 
Jana hata kabla ya Simba kutoa taarifa kuhusu kumsimamisha Bernard Morrison nilieleza kuwa mchezaji huyo amesimamishwa kwa sababu ya utovu wa nidhamu kwa kile kilichodaiwa kuwa alitoroka kambini.

Baadaye Morrison akapost kwenye pages zake kuwa kuna kitu kikubwa kinakuja akiwa ameweka picha ameshika mabegi kama mtu anayesafiri.

Sasa taarifa za ndani ya Simba zinaeleza kuwa klabu hiyo haina mpango wa kuendelea kuwa na mchezaji huyo, hivyo wanachosubiri ni kumalizika kwa mkataba wake ambao umesalia miezi mitano, kisha wamalizane naye kwa kuwa hajaonyesha uwezo walioutarajia.

Mbali na hapo inaelezwa kuwa kuna kigogo wa Klabu ya Yanga yupo tayari kusimamia shoo ili mchezaji huyo arejee Jangwani, jambo ambalo limewagawa baadhi ya viongozi.

Kwa hatua iliyopo ni kuwa Morrison anaweza kufanya mazungumzo na klabu nyingine yoyote kwa kuwa kanuni inamruhusu na ikiwezekana kusaini mkataba wa awali.

Hakuondoka Yanga vizuri, hiyo ni hoja ya baadhi ya viongozi wanaopinga kurejea kwake klabuni hapo wakionekana watakuwa wanamrudisha mtu aliyewakosea heshima, lakini wale wanaounga mkono kurejea kwake wanataka arejee ili wawaumize wapinzani wao wa jadi, Simba.

Hivyo, ni suala la muda kusubiri nini kitatokea, Simba wapo kwenye presha ya matokeo na kiwango bora, je, wataendelea kumfikiria Morrison au watapuuzia na kumuacha akiondoka ikiwezekana kwenda Yanga kirahisi? Muda utazungumza ila suala la Morrison kuondoka Simba hilo halikwepeki kwa sasa.
Jangwani hana nafas, aende prison
 
Muache asepe, morrison ni mchezaji mzuri endapo ataacha uchoyo na kupenda kucheza kwa show off

Huko aendako akijirekebisha hayo mapungufu yake atakuwa ni mchezaji hatari na wakuhofiwa na wapinzani
Ile tabia hatoiacha kamwe, anajiona bonge la superstar na nyie mlivyomjaza upepo akajaa zaidi, ukijumlisha na walishindwa kulala usingizi kisa yeye mpaka kuangaika na CAS ndio kabiisaaaaa akajaaa zaidi na kujiona kumbe kwa hapa Tanzania ni mtu mmoja wakipee sana nagombaniwa kama dhahabu. Mzee akawakera wana Yanga saivi kawakera hadi na nyie wenyewe.

Labda kwanza waangaike na afya yake ya akili nako ni kupoteza muda utafikiri hakuna wachezaji zaidi yake
 
Mi naombea aende kwa watani zetu utoh ili waongeze idadi ya mapoyoyo kwenye klub yao (manara +morison+……)
 
Ivi Yanga Haioni Wachezaji Wengine, Mbn Wachezaji Wamejaa Wengi Kila Kona Ya Afrika Kuanzia Kusini, Kaskazini, Kati, Magharibi Na Mashariki...Af Wanauwezo Mzuri Wa Kucheza Soka Shida Bado Hamjawaona...Yanga Wafanye Msako Kwenye Ligi Za Sehemu MbaliMbali Hapa Afrika Watapata Watu Wataokaweza Kuwamudu Kuwasajili Na Wenye Uwezo Mzuri Kwa Manufaa Ya Timu... Sio Kila Siku Kung'ang'ania Watu Wale Wale Wakati Wachezaji Wazuri Na Wenye Hadhi Ya Kucheza Yanga Ni Wengi...
 
Back
Top Bottom