Mundana
Member
- Jun 8, 2015
- 84
- 114
Habari Za Mchana,
Poleni na majukumu na mihangiko ya Kila Siku na Kwa wale watakaofanya Usahili kesho niwatakie Usahili Mwema.
Sasa nirudi Kwenye topic, hili suala nimekua nikiliangalia Sana kwenye Usahili ukienda lugha inayotumika kuwasahili ni kiingereza. Hivi wanavyofanya hawatendi haki kabisa Yan unakuta MTU Ile kazi anaiweza vizuri na anaimudu akipewa kuifanya sasa kwenye suala la kujieleza au kujitetea Kwa lugha ya kiingereza inakuwa mtihani lakini anajua yupo vizuri, Sasa walau Utumishi basi wangekuwa wanaruhusu lugha zote mbili zitumike kiingereza na Kiswahili hasa kwenye usahili wa ana kwa ana na wa vitendo.
Kufanya hivyo kutawasaidia Wale watu ambao wanasifa na wanakizi vigezo vya hiyo Kazi na wao wapate nafasi. Haki inatakiwa kotekote kuleta usawa, hasa ukizingatia lugha ya Kiswahili ndo lugha yetu ya Taifa, kwanini wasiipe kipaumbele.
Kuna siku miaka ya nyuma nilienda kwenye Usahili sehemu Fulani Hivi, tulikuwa ni wengi Sana, tukapunguzwa Sana katika hatua zile za awali yan written na practical sasa ikabaki hatua ya mwisho ya oral nilikuwa na Dada mmoja hivi tunasubiri kuingia kwenye oral ya mwisho, Yule Dada mpaka nilimuonea huruma na machozi yanamtoka nikamfuata kujaribu kumuuliza nini kilichokuwa kina mliza, akaniambia kuwa Amalia kwasababu Yeye kujieleza Kwa lugha ya kiingereza hajui kabisa anajua Tu Ile ngeli ya kwenye makaratasi na sio kusimama mbele za Watu ukajenga hoja na wakuelewe vizuri kwake yeye ni mtihani, hivyo anaona kabisa hiyo Nafasi ameshaikosa tayari, uzoefu wa KAZI anao mzuri Tu lakini hapo kwenye lugha ndo palimshinda kabisaa hawezi hata kidogo.
Nikajaribu kumpa Moyo asikate Tamaa ajaribu Bahati yake, ikafika zamu yake kuingia, Yan Hata dakika moja haikuisha akawa Ametoka
Ile kazi hakufanikiwa kuipata hatua ya mwisho ndo ilimfelisha.
Utumishi wajaribu kuangalia Hilo suala walau basi wabalance lugha zote mbili zitumike kiingereza na Kiswahili ili kuwapa nafasi wengine waweze kupata Kazi. Mbona kwenye matangazo Yao ya Kazi wanatuandikia Kwa Kiswahili hasa Yale ya kuitwa kwenye Usahili au kuitwa Kazini.
Nawasilisha.
Poleni na majukumu na mihangiko ya Kila Siku na Kwa wale watakaofanya Usahili kesho niwatakie Usahili Mwema.
Sasa nirudi Kwenye topic, hili suala nimekua nikiliangalia Sana kwenye Usahili ukienda lugha inayotumika kuwasahili ni kiingereza. Hivi wanavyofanya hawatendi haki kabisa Yan unakuta MTU Ile kazi anaiweza vizuri na anaimudu akipewa kuifanya sasa kwenye suala la kujieleza au kujitetea Kwa lugha ya kiingereza inakuwa mtihani lakini anajua yupo vizuri, Sasa walau Utumishi basi wangekuwa wanaruhusu lugha zote mbili zitumike kiingereza na Kiswahili hasa kwenye usahili wa ana kwa ana na wa vitendo.
Kufanya hivyo kutawasaidia Wale watu ambao wanasifa na wanakizi vigezo vya hiyo Kazi na wao wapate nafasi. Haki inatakiwa kotekote kuleta usawa, hasa ukizingatia lugha ya Kiswahili ndo lugha yetu ya Taifa, kwanini wasiipe kipaumbele.
Kuna siku miaka ya nyuma nilienda kwenye Usahili sehemu Fulani Hivi, tulikuwa ni wengi Sana, tukapunguzwa Sana katika hatua zile za awali yan written na practical sasa ikabaki hatua ya mwisho ya oral nilikuwa na Dada mmoja hivi tunasubiri kuingia kwenye oral ya mwisho, Yule Dada mpaka nilimuonea huruma na machozi yanamtoka nikamfuata kujaribu kumuuliza nini kilichokuwa kina mliza, akaniambia kuwa Amalia kwasababu Yeye kujieleza Kwa lugha ya kiingereza hajui kabisa anajua Tu Ile ngeli ya kwenye makaratasi na sio kusimama mbele za Watu ukajenga hoja na wakuelewe vizuri kwake yeye ni mtihani, hivyo anaona kabisa hiyo Nafasi ameshaikosa tayari, uzoefu wa KAZI anao mzuri Tu lakini hapo kwenye lugha ndo palimshinda kabisaa hawezi hata kidogo.
Nikajaribu kumpa Moyo asikate Tamaa ajaribu Bahati yake, ikafika zamu yake kuingia, Yan Hata dakika moja haikuisha akawa Ametoka
Ile kazi hakufanikiwa kuipata hatua ya mwisho ndo ilimfelisha.
Utumishi wajaribu kuangalia Hilo suala walau basi wabalance lugha zote mbili zitumike kiingereza na Kiswahili ili kuwapa nafasi wengine waweze kupata Kazi. Mbona kwenye matangazo Yao ya Kazi wanatuandikia Kwa Kiswahili hasa Yale ya kuitwa kwenye Usahili au kuitwa Kazini.
Nawasilisha.