Usahihi kuhusu BRELA

Pagan Amum

JF-Expert Member
Aug 28, 2015
1,932
4,395
Imani iwe kwenu Wakuu!

Baada ya mdau moja kuleta uzi leo kuhusu BRELA Kwanini Rais Magufuli hataki kutumbua jipu la BRELA? , naomba nisaidie kuweka record sahihi. Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni. Mimi ni mteja wa BRELA wa miaka mingi, ukweli ni kwamba BRELA ile ya enzi zile siyo hii ya sasa. BRELA ya sasa wanajitahidi sana kwenda na wakati hususani siku za karibuni

Kwa sasa huduma ya kusajili jina la biashara hutolewa kwa njia ya mtandao kwa Tsh. 20,000 tu, popote ulipo Tanzania, awali ilikuwa inakulazimu kusafiri kwenda Dar es Salaam kusajili jina la biashara

Pia, kupata taarifa za makampuni hususani, majina ya wanahisa, wakurugenzi, ofisi za kampuni na mtaji wa kampuni huduma hizo sasa inapatikana kwa njia ya mtandao

Vile vile ukitaka kusajili kampuni awali ilikulazimu kuandika barua na kupeleka kwenye ofisi za BRELA (DSM) kuomba jina hilo unalotaka kusajili kuhakikiwa kama hakuna kampuni nyingine iliyosajiliwa kwa jina hilo hilo, sasa hivi huduma hiyo inatolewa kwa njia ya mtandao na ni bure, ila ukiwa unapenda jina hilo litunzwe kwa muda wa siku 60 itakulazimu kulipa nafkiri Tsh. 50,000 tu. Na hii ni kwa mujibu wa sheria za makampuni

Pia, malipo ya huduma zote za usajili sikuhizi hulipwa kwa njia ya mtandao; Mpesa, Tigopesa, Fahari huduma, Simbanking, Mobile banking, matawi yote ya CRDB, matawi yote ya NMB Tanzania nzima.

Mwisho, naomba niwasihi wana Jukwaa hili na wananchi wote, kwa kuepuka upotoshaji kama ulivyoletwa humu JF kwa makusudi yake binafsi, ni vyema tujenge tabia ya kupata taarifa zaidi za usajili wa makampuni kwa kuwatembelea ofisini kwao moja kwa moja ama kwa njia ya mtandao www.brela.go.tz (Hapo utapata kila kitu, na sio ule upotoshwaji uliofanya na member mwenzetu wa JF)..

Asanteni!
 
Naungana na wewe Mkuu. brela ya sasa inaendana na speed ya Magufuli. Juzi juzi walikuja huku kanda ya ziwa majamaa wako fresh sana. Ndani ya dakika 10 nilipata cheti na sasa nina kampuni yangu.

Kuna vijana pale wanapiga kazi sana sana.
 
Mtoa mada kwa heshima naomba nitofautiane na wewe. BRELA bado sana tena sana na inalekea hata Brela wenyewe haelewi ni wapi wana mapungufu. Kwa mfano unasema kuwa siku hizi huduma za usajili zinapatikana kupitia kwenye mtandao wao. Lakini sielewi ni kwanini inachukua zaidi ya saa 12 kufanya usajili kwa kutumia mtandao. Jaribu kufanya usajili Singapore, ndani ya dakika kumi umemaliza mchezo, Brela ni utani mtupu.

Kama Brela wanakubaliana na hoja yako kuwa wanatoa huduma nzuri basi tuna tatizo kubwa zaidi. Tuko kwenye dunia ya ushindani, nchi nyingine wanafanya mageuzi makubwa kwenye taasis kama ya Brela ili kuweka mazingira rafiki ya biashara. Hapa Tanzania inalekea Brela wamejiwekea viwango vya chini mno. Na ukienda kwenye Ofisi zao - tena makao makuu ni zogo tupu utafiki tuko kwenye industrial revolution era. Inatia aibu kweli.
 
BRELA kuna urasimu sana nilitaka kusajili kampuni nikashindwa hasa wa mikoani mpaka uende makao makuu Dar na bado ukifika huko unazungushwa weeee hata online ndio hakuna kitu website yao hata ku update shida habari toka za mwaka juzi ndio hizo hizo wanahitaji kubadilika sana
 
Katika watu wanaomkwamisha Magufuli kwenye azma yake ya kuifanya Tanzania iwe ya viwanda, wa kwanza ni BRELA....
 
Katika watu wanaomkwamisha Magufuli kwenye azma yake ya kuifanya Tanzania iwe ya viwanda, wa kwanza ni BRELA....

Kama kweli Magufuli anataka kuifanya Tanzania iwe ya viwanda ni lazima afumue BRELA, TDFA, NEMC, SIDO na Tantrade. Bila kuzifumua hizo taasis atapata shida sana.
 
BRELA bado hawajajipanga bado msitetee ujinga tenda mmwambie anaesimamia tovuti yao awe shapu kubadilisha taarifa mara kwa mara kama kazi inawashinda waseme
 
Imani iwe kwenu Wakuu!

Baada ya mdau moja kuleta uzi leo kuhusu BRELA, naomba nisaidie kuweka record sahihi. Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni. Mimi ni mteja wa BRELA wa miaka mingi, ukweli ni kwamba BRELA ile ya enzi zile siyo hii ya sasa. BRELA ya sasa wanajitahidi sana kwenda na wakati hususani siku za karibuni

Kwa sasa huduma ya kusajili jina la biashara hutolewa kwa njia ya mtandao kwa Tsh. 20,000 tu, popote ulipo Tanzania, awali ilikuwa inakulazimu kusafiri kwenda Dar es Salaam kusajili jina la biashara

Pia, kupata taarifa za makampuni hususani, majina ya wanahisa, wakurugenzi, ofisi za kampuni na mtaji wa kampuni huduma hizo sasa inapatikana kwa njia ya mtandao

Vile vile ukitaka kusajili kampuni awali ilikulazimu kuandika barua na kupeleka kwenye ofisi za BRELA (DSM) kuomba jina hilo unalotaka kusajili kuhakikiwa kama hakuna kampuni nyingine iliyosajiliwa kwa jina hilo hilo, sasa hivi huduma hiyo inatolewa kwa njia ya mtandao na ni bure, ila ukiwa unapenda jina hilo litunzwe kwa muda wa siku 60 itakulazimu kulipa nafkiri Tsh. 50,000 tu. Na hii ni kwa mujibu wa sheria za makampuni

Pia, malipo ya huduma zote za usajili sikuhizi hulipwa kwa njia ya mtandao; Mpesa, Tigopesa, Fahari huduma, Simbanking, Mobile banking, matawi yote ya CRDB, matawi yote ya NMB Tanzania nzima.

Mwisho, naomba niwasihi wana Jukwaa hili na wananchi wote, kwa kuepuka upotoshaji kama ulivyoletwa humu JF kwa makusudi yake binafsi, ni vyema tujenge tabia ya kupata taarifa zaidi za usajili wa makampuni kwa kuwatembelea ofisini kwao moja kwa moja ama kwa njia ya mtandao www.brela.go.tz (Hapo utapata kila kitu, na sio ule upotoshwaji uliofanya na member mwenzetu wa JF)..

Asanteni!
chek inbox.nimekutumia text
 
BRELA kuna urasimu sana nilitaka kusajili kampuni nikashindwa hasa wa mikoani mpaka uende makao makuu Dar na bado ukifika huko unazungushwa weeee hata online ndio hakuna kitu website yao hata ku update shida habari toka za mwaka juzi ndio hizo hizo wanahitaji kubadilika sana

Lini umejaribu?. Ebu jaribu hata leo Mkuu. Tusiongelee mate wakati wino upo
 
chek inbox.nimekutumia text
una tabia ya majungu,

anyway,brela wanajitahidi sana,na hii ni taasisi nyeti kwa usalama wa nchi,hawawezi kukurupuka tu na kukusajiria kampuni yako hata kama.ina malengo ya kigaidi na kuuza madawa ya kulevya.

pia si mbaya mtu kusajili kampuni ndani ya siku mbili tatu au maximum wiki moja,una haraka ya nini?unawahi kutapeli au?

la msingi nafikiri imefika wakati wawe na ofisi za kanda,dar,mwanza,arusha
 
Sawa lakini ulitakiwa kuleta mapema haya maelezo hapa Kwa sababu wananchi wengi wanapitia wangeyapata hivyo ingeepusha upotoshaji.........

Jitahidini kuwa munaleta maelezo kabla ya upotoshaji maana ni wajibu wenu kutoa elimu Kwa umma......

Mimi pia sipendi upotoshaji unaofanywa na baadhi ya watu lakini tusiogope kuleta ufafanuzi ,elimu Kwa umma kabla umma aujatupotosha .....

Taasisi zetu kukaa kimya ndio kansa ya mambo yote.

Asante.
una tabia ya majungu,

anyway,brela wanajitahidi sana,na hii ni taasisi nyeti kwa usalama wa nchi,hawawezi kukurupuka tu na kukusajiria kampuni yako hata kama.ina malengo ya kigaidi na kuuza madawa ya kulevya.

pia si mbaya mtu kusajili kampuni ndani ya siku mbili tatu au maximum wiki moja,una haraka ya nini?unawahi kutapeli au?

la msingi nafikiri imefika wakati wawe na ofisi za kanda,dar,mwanza,arusha
 
Mtoa mada kwa heshima naomba nitofautiane na wewe. BRELA bado sana tena sana na inalekea hata Brela wenyewe haelewi ni wapi wana mapungufu. Kwa mfano unasema kuwa siku hizi huduma za usajili zinapatikana kupitia kwenye mtandao wao. Lakini sielewi ni kwanini inachukua zaidi ya saa 12 kufanya usajili kwa kutumia mtandao. Jaribu kufanya usajili Singapore, ndani ya dakika kumi umemaliza mchezo, Brela ni utani mtupu.

Kama Brela wanakubaliana na hoja yako kuwa wanatoa huduma nzuri basi tuna tatizo kubwa zaidi. Tuko kwenye dunia ya ushindani, nchi nyingine wanafanya mageuzi makubwa kwenye taasis kama ya Brela ili kuweka mazingira rafiki ya biashara. Hapa Tanzania inalekea Brela wamejiwekea viwango vya chini mno. Na ukienda kwenye Ofisi zao - tena makao makuu ni zogo tupu utafiki tuko kwenye industrial revolution era. Inatia aibu kweli.

Sidhani kama inachukua masaa 12. Last time ilinichukua masaa 2 Mkuu. Like two weeks ago...

Infact nakubaliana na issue ya IT department yao kuwa inactive
 
BRELA bado hawajajipanga bado msitetee ujinga tenda mmwambie anaesimamia tovuti yao awe shapu kubadilisha taarifa mara kwa mara kama kazi inawashinda waseme
taarifa ipi ilichelewa kubadilishwa?hii nchi ndio maana muingereza alikataa umoja wa mataifa wakamuomba akae nayo kwa muda mpaka.ipate uhuru,uhuru wenyewe tuliupata kwa maneno,ndio maana kila siku maneno,mpaka miaka hamsini ya uhuru tumejaa maneno
 
Sidhani kama inachukua masaa 12. Last time ilinichukua masaa 2 Mkuu. Like two weeks ago...

Infact nakubaliana na issue ya IT department yao kuwa inactive

Nina watu kama watano (mimi nikiwemo) tumeshajaribisha sana kufanya usajili. Hatua ya kwanza lazima ufanye clearance ya jina process ambayo inachukuwa masaa sio chini ya nane, then ndio uanze usajili wenyewe. Kumbuka registration inaanza na clearance ya jina kwanza. Lakini hakuna haja ya kuandikia mate, jaribu leo hii ufanye name search, clearance na usajili wenyewe uone itakukuchua muda gani. Halafu jiridhishe kama hiyo process ni 'friendly' kwa watanzania wa kawaida ambao hata lugha (kiingereza) inayotumika kwenye mtandao ni shida.

Ukiangalia report ya Workd Bank kuhusu 'ease of doing business' Tanzania tuko nyuma sana (tunashika nafasi ya 139). Na hatuwezi kurekebisha hayo kama utendaji wa Brela utandelea kama ulivyo. Waziri wa viwanda sijui anafanya nini?
 
taarifa ipi ilichelewa kubadilishwa?hii nchi ndio maana muingereza alikataa umoja wa mataifa wakamuomba akae nayo kwa muda mpaka.ipate uhuru,uhuru wenyewe tuliupata kwa maneno,ndio maana kila siku maneno,mpaka miaka hamsini ya uhuru tumejaa maneno
Hayo maelezo ya historia ungewafundisha wanafunzi ingependeza kwenye tovuti yenu mnaona ipo sawa kabisa tunavyo apply kupata hiyo fomu ya kusajili jina la kibiashara/kampuni? Halafu mpompo tu hamna ushawishi wowote kwa wateja hata kujitangaza ni kazi
 
To be honest BRELA wamejitahidi sana kubadilika kwa kiwango kikubwa sana tofauti na enzi ya JK

Tatizo kubwa ni mifumo ya IT ndio inaleta shida ila ukikuta imetulia ni ndani ya masaa 24 inakua tayari
Cha umuhimu ambacho watu wengi wanafanya usjilk kuwa mrefu ni kutokuyimiza nyaraka zote zinazotakiwa zikiwa timamu

Ni kweli kwamba mapungufu yapo lakini sio kama mleta mada wa awali alivyojaribu kuamisha watu

Hebu mtu aende kusajili halafu alete ripoti hapa
 
Mie nilishakataga tamaa, maadam mmekuja kufafanua nitajaribu tena kusajili kampuni!Ilikuwea ni lazima utoe rushwa, nikasema to hell!
 
ku search jina la kampuni...why does one have to register kufanya search? its like Google kualzimisha watu wajisajili ndio wataruhusiwa kufanya search

Usajili ni pale unapotaka kufungua kampuni ndio unaweza ku sajili
 
Back
Top Bottom