Pagan Amum
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 1,932
- 4,395
Imani iwe kwenu Wakuu!
Baada ya mdau moja kuleta uzi leo kuhusu BRELA Kwanini Rais Magufuli hataki kutumbua jipu la BRELA? , naomba nisaidie kuweka record sahihi. Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni. Mimi ni mteja wa BRELA wa miaka mingi, ukweli ni kwamba BRELA ile ya enzi zile siyo hii ya sasa. BRELA ya sasa wanajitahidi sana kwenda na wakati hususani siku za karibuni
Kwa sasa huduma ya kusajili jina la biashara hutolewa kwa njia ya mtandao kwa Tsh. 20,000 tu, popote ulipo Tanzania, awali ilikuwa inakulazimu kusafiri kwenda Dar es Salaam kusajili jina la biashara
Pia, kupata taarifa za makampuni hususani, majina ya wanahisa, wakurugenzi, ofisi za kampuni na mtaji wa kampuni huduma hizo sasa inapatikana kwa njia ya mtandao
Vile vile ukitaka kusajili kampuni awali ilikulazimu kuandika barua na kupeleka kwenye ofisi za BRELA (DSM) kuomba jina hilo unalotaka kusajili kuhakikiwa kama hakuna kampuni nyingine iliyosajiliwa kwa jina hilo hilo, sasa hivi huduma hiyo inatolewa kwa njia ya mtandao na ni bure, ila ukiwa unapenda jina hilo litunzwe kwa muda wa siku 60 itakulazimu kulipa nafkiri Tsh. 50,000 tu. Na hii ni kwa mujibu wa sheria za makampuni
Pia, malipo ya huduma zote za usajili sikuhizi hulipwa kwa njia ya mtandao; Mpesa, Tigopesa, Fahari huduma, Simbanking, Mobile banking, matawi yote ya CRDB, matawi yote ya NMB Tanzania nzima.
Mwisho, naomba niwasihi wana Jukwaa hili na wananchi wote, kwa kuepuka upotoshaji kama ulivyoletwa humu JF kwa makusudi yake binafsi, ni vyema tujenge tabia ya kupata taarifa zaidi za usajili wa makampuni kwa kuwatembelea ofisini kwao moja kwa moja ama kwa njia ya mtandao www.brela.go.tz (Hapo utapata kila kitu, na sio ule upotoshwaji uliofanya na member mwenzetu wa JF)..
Asanteni!
Baada ya mdau moja kuleta uzi leo kuhusu BRELA Kwanini Rais Magufuli hataki kutumbua jipu la BRELA? , naomba nisaidie kuweka record sahihi. Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni. Mimi ni mteja wa BRELA wa miaka mingi, ukweli ni kwamba BRELA ile ya enzi zile siyo hii ya sasa. BRELA ya sasa wanajitahidi sana kwenda na wakati hususani siku za karibuni
Kwa sasa huduma ya kusajili jina la biashara hutolewa kwa njia ya mtandao kwa Tsh. 20,000 tu, popote ulipo Tanzania, awali ilikuwa inakulazimu kusafiri kwenda Dar es Salaam kusajili jina la biashara
Pia, kupata taarifa za makampuni hususani, majina ya wanahisa, wakurugenzi, ofisi za kampuni na mtaji wa kampuni huduma hizo sasa inapatikana kwa njia ya mtandao
Vile vile ukitaka kusajili kampuni awali ilikulazimu kuandika barua na kupeleka kwenye ofisi za BRELA (DSM) kuomba jina hilo unalotaka kusajili kuhakikiwa kama hakuna kampuni nyingine iliyosajiliwa kwa jina hilo hilo, sasa hivi huduma hiyo inatolewa kwa njia ya mtandao na ni bure, ila ukiwa unapenda jina hilo litunzwe kwa muda wa siku 60 itakulazimu kulipa nafkiri Tsh. 50,000 tu. Na hii ni kwa mujibu wa sheria za makampuni
Pia, malipo ya huduma zote za usajili sikuhizi hulipwa kwa njia ya mtandao; Mpesa, Tigopesa, Fahari huduma, Simbanking, Mobile banking, matawi yote ya CRDB, matawi yote ya NMB Tanzania nzima.
Mwisho, naomba niwasihi wana Jukwaa hili na wananchi wote, kwa kuepuka upotoshaji kama ulivyoletwa humu JF kwa makusudi yake binafsi, ni vyema tujenge tabia ya kupata taarifa zaidi za usajili wa makampuni kwa kuwatembelea ofisini kwao moja kwa moja ama kwa njia ya mtandao www.brela.go.tz (Hapo utapata kila kitu, na sio ule upotoshwaji uliofanya na member mwenzetu wa JF)..
Asanteni!