Sasa kama ulikuwa hujifahamu ulivyo, hii ndio description halisi ya wewe ulivyo .... !Kuna vilaza waliobarikiwa kuwa vilaza na wakaupokea ukilaza kwa moyo mkunjufu na vigeregere wanaangalia zile picha, still photos za tukio lilivuoyokea na wanafanya hitimisho kuwa Juliana ndo hakuwa sahihi.
Hapa sijaelewa! Huu ni ufafanuzi wa kilichotokea au ni ujumbe kwa Chadema kuwa wewe sio wa mchezo mchezo na wakishasoma wakukome au mimi ndio sijui kusoma???Wanajamvi,
Kwa muda sasa nimekuwa kimya sana kuchangia na kushiriki mijadala mbalimbali inayoendelea kwenye jamvi letu hii ni kutokana na majukumu yanayonikabili ikiwemo kazi pamoja na shule.
Nalazimika kurudi tena jukwaani kutolea ufafanuzi wa kile kilichotokea jana katika viwanja vya bunge kwani nimepokea simu nyingi na ujumbe mbalimbali, na kwa maelezo yao nimegundua kuwa upo upotoshaji mkubwa wa kilichotokea na kinachoendelea. Katika hali kama hiyo busara yangu ikaniongoza kuja kulitolea ufafanuzi.
Mtakumbuka kuwa siku ya jumatatu ya tarehe 5 June, 2017 Bunge liliazimia kumsimamisha Mbunge Halima Mdee kwa kipindi cha Mwaka mmoja, na azimio hili lilitokana kwa kiasi kikubwa na hoja yangu ya kutaka Mhe Halima aongezewe adhabu ambayo mara ya kwanza ilikuwa ni ndogo na isiyofanana na aina ya makosa aliyoyafanya. Kitendo hicho kiliwaghadhibisha wabunge na viongozi wa CHADEMA, hivyo wakakutana mjini Dodoma na kupanga mikakati ya kunidhuru.
Kama kawaida nikapata taarifa hizo mapema sana hata kabla ya kikao chao hakijaisha nami nikachukua hatua ya kwenda kuripoti katika vyombo vinavyohusika na Ulinzi na Usalama wa raia kuwa upo mkakati wa aina hiyo, hatua hiyo iliwafanya washindwe kufanikisha mkakati wao. Hivyo tangu hapo wakawa wanafikiria mbinu nyingine za kutaka kunishughulikia.
Kilichotokea jana ni matokea ya kufeli kwa mipango yao ya kidhalimu dhidi yangu, jana walidhihirisha wazi wazi kilichomo ndani ya vifua vyao juu yangu. Jana, nimeshambuliwa, kwa mara nyingine tena nimetukanwa na kudhalilishwa tena ndani ya viwanja vya bunge.
Nimesikitishwa na vijana waliotumwa kuja kunishambulia, hawakuja kwa bahati mbaya bali ni sehemu ya maelekezo waliyopewa, nao kama kawaida bila kufikiria athari ya maelekezo hayo wakaamua kuyatekeleza na kuja kunishambulia na kunidhalilisha, tena wengi ni wabunge Vijana ambao mimi siku zote nimekuwa nikiwaheshimu na kuwafanya wenzangu, nikiamini kuwa Viongozi Vijana tuna mzigo mzito mabegani mwetu wa kuongoza kizazi cha leo na kesho, na ili tufike mbali hatuna budi tutembee na kizazi chetu na tushirikiane baina yetu. Inasikitisha kuona Vijana kwa mara nyingine tena wanakubali kutumwa kumshughulikia kijana mwenzao. Taarifa kuwa nimeshambuliwa na watu wazima hazina ukweli wowote, ni vijana waliotumwa.
Naomba niwakumbushe jambo moja, miaka 5 iliyopita nikiwa na umri wa miaka 25 tu nilikuwa na UJASIRI wa kupambana na aliyewatuma jana, i dare to stand against ur so praised DEMIGOD, and i made my way out victoriously.
Naandika historia yangu kwa mkono wangu, U should always be alarmed and alerted mkitumwa kushughulika na mimi, i have never been soft in my life, go easy on urself. Wapo wanaoitengeneza historia, kuna wanaoiandika na wapo wanaoitazama historia ikitengenezwa na kuandikwa.,mmeamua kuendelea kubaki watazamaji.
Ingefaa zaidi kushughulika na Chama chenu kuliko kushughulika na JULIANA, i am just UNBREAKABLE.
Akagombee jimbo ndipo tuone how she is "UNBREAKABLE"!! ANADANGANYWA na WANAOMDANGANYA na HAJUI KUWA ANATUMIKA KWA MASLAHI YA WENGINE"UNBREAKABLE" kumbe bado hujaijua dunia!
Papuchi tu baba! Hamna kigezo kingineEti muwakilishi wa vijana Songwe mjengoni,walitumia vigezo gani kukuweka hapo?
Baby wa Mwigulu,kamtuma Mwigulu vilevile atatoa ushahidi wake hadi mbinguniMbunge wa hovyo kabisa huyu
Endelea kuwaosha wenye nacho miguu