JK akiamua kuweka masrahi ya Taifa mbele inawezekana na Posho anaweza shusha mpaka Tsh.50,000/= na wakawa wanalala Guest za Tsh.7000/=
Kiongozi wa shughuli za serikali Bungeni alikuwa Edward Morengi Sokoine kabla ya kufa katika ajali April 1984 !!!
Wabunge wa kileo wamevimba matumbo, kwa mlango wa basi hawapiti . . .
Wada katika pitapita zangu nimekutana na hiki kitu,hivi hata sasa haiwezekani kufanya hivi kwa masilahi ya masikini wa taifa hili??
Samahani wakuu,
Hivi mwaka 1984 kurudi nyuma, Rais wa Tanzania alikuwa nani vile!
Alikuwa Rais wa Ukweli Mwl. Julius Kambarage Nyerere... Alistaafu kwa hiyari mwaka 1985. Mzee Ruksa akashika kijiti.. Japo JKN alipenda arithiwe na Dr. Salim A. Salim.
Hizo ndiyo enzi za mwalimu bwana......! alibana matumizi ya wakubwa yule mzee bwana hadi akawa anaweza kusomesha wanfunzi vyuo vikuu bure, usafiri wa treni reli ya kati na Tazara ulikuwa timamu matibabu yalikuwa bure..daftari likiisha shuleni lililoisha linacchanwa kidogo unapewa jipya!!!!!
Mwalimu angekuwa ndiyo raisi kwa sasa nchi yetu ingepiga hatua sana maana sasa kuna mahela mengi yanaishia kwenye mikono ya mafisadi.... na walafi wengine wakiwamo wabunge!