Usafiri Dar - Mtwara, King Yassin Tours hongera

Hao jamaa wanajitahidi kwa huduma , kusini mikoa ya mtwara na Lindi bado kunahitaji ukombozi mkubwa sana kwa biashara ya abiria maana ni kama ndo wanaaanza ,
Abiria kule hana haki zake za msingi , kumbuka hawana hata Miaka 10 ya mabasi mazuri ,kwa sababu njia ilisumbua sana kule ,
Usishangae unapanda Basi halafu konda anakuomba pesa ya begi ulilobeba Kama mzigo mbali na nauli .
Wewe naona hujapanda magari ya Kigoma, Sumbawanga au Mpanda shukruni hata kwa hicho kidoogo wanachotoa. Hizo ruti utaambulia Mende na Kunguni Mkuuu.
 
Wewe naona hujapanda magari ya Kigoma, Sumbawanga au Mpanda shukruni hata kwa hicho kidoogo wanachotoa. Hizo ruti utaambulia Mende na Kunguni Mkuuu.
Kweli sijapanda Basi za huko na hata nikikutana na hizo kero bado nitawasamehe maana huko njia bado ni mbovu sana matajiri hawajainvest vizuri kwenye mabasi.

Njia ya mtwara tayari ni nzuri hutegemei upande mabasi yenye huduma mbovu.
 
Kwa maana hiyo.. mpaka sasa naona kuna haja kuu mbili juu ya usafiri Kusini.

1. Uwekezaji wa hotel ya kisasa kabisa mazingira safi na rafiki kwa abiria wote. Tatizo nawaza tabaka la huko watalua tayari kwa nature ya vipato vyao?
Vipi idadi ya wageni huko? Je, wale wa nje ya mikoa hiyo ni wengi kiasi cha kuvutia uwekezaji huo? Maana muwekezaji asije wekeza mradi mkubwa akaishia kula hasara. Tunatamani hata sisi kama kusafiri kuja huko tupate mazingira safi kabisa ya kula.

2. Bado inaonekana usafi kwa pande hizo haujasimama vyema. Bado inaonekana changamoto mpya juu ya wafanyabiashara wengine waliopo hapo wamebweteka na hawako vizuri kwa huduma. Hivyo ushindani na vyombo imara vinahitajika.

NB: nimewaza chai ya moto na maandazi gari iwe masaa ya mbele halafu ipite lwenye tuta mtikisiko wake na chai ya moto

Mitano tena
Mkoa wa Lindi wenyewe bado hauna basi direct kutoka stand yake kuu, wanategemea mabasi ya mtwara, newala, masasi tunduru nachingwea na songea.

Hata uwe na mishe zako za mjini huwezi kupata Basi la saa kumi na mbili asubuhi kutoka Lindi , itabidi usubirie basi la kwanza kutoka mtwara amabalo linafika Lindi kuanzia saa moja asubuhi.

Abiria bado wachache sana lindi
 
Mkoa wa Lindi wenyewe bado hauna basi direct kutoka stand yake kuu, wanategemea mabasi ya mtwara, newala, masasi tunduru nachingwea na songea .
Hata uwe na mishe zako za mjini huwezi kupata Basi la saa kumi na mbili asubuhi kutoka Lindi , itabidi usubirie basi la kwanza kutoka mtwara amabalo linafika Lindi kuanzia saa moja asubuhi
Abiria bado wachache sana lindi
Lindi Sio mkoa ni kijiji flani tu kilichochangamka.
 
King Yassin bado ni kampuni changa kusini, Inabembeleza wateja waiamini,

Kuna kitu Maning ning, Maning Nice huyu ndiyo mwamba wa kusini, Gari hata iwe na abiria watano muda wa kuondoka ukifika Haina kulemba Pira linawashwa linatembea.

Hasa root ya Mtwara Morogoro. Braza hizi siyo enzi za kusifia chai Bali muda. King Yassin, Bado Bora hata Buti la zungu , Ila Maning Nice Babalao.
Maning nice, nilikata ticket ya kuondoka saa kumi na mbili asubuhi, gari limeondoka saa mbili asubuhi, tena hapo abiria tushaanza kuwapigia makelele.
 
Huduma ya chai kwenye mabasi sio ngeni japo ni complex kidogo. Miaka ya nyuma Basi za grazia venerali, Dar njombe walikuwa wanatoa chai na bites ,
Ivi Grazia iyo kampuni ipo hadi leo ama
 
King Yassin bado ni kampuni changa kusini, Inabembeleza wateja waiamini,

Kuna kitu Maning ning, Maning Nice huyu ndiyo mwamba wa kusini, Gari hata iwe na abiria watano muda wa kuondoka ukifika Haina kulemba Pira linawashwa linatembea.

Hasa root ya Mtwara Morogoro. Braza hizi siyo enzi za kusifia chai Bali muda. King Yassin, Bado Bora hata Buti la zungu , Ila Maning Nice Babalao.
Wapuuzi hawa Maning Nice, tulishawahi kutoka Morogoro saa 12 alfajiri, kwanza wanapakia maasai wote wanaoenda kuchunga vijiji kati ya Dar na Mlandizi, Ubungo tukafika saa 4-5,
Tukapelekwa garage Tandika sijui Temeke, wakachomelea weeh, walipochoka, wakatubadilishia gari, Mbagala saa 8, kudadadeki niliapa NEVER again, Ikwiriri saa10-11, Mtwara sijui walifika saa ngapi!

Bora kuunga Moro Dar BM, Abood saa 3 Korogwe unadandia mwendokasi saa 4 unusu uko Mbagala, stendi ya Shamba, gari za Muhoro, dk 0 zinajaa, Ikwiriri 7-8 ulishafika!

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Mkoa wa Lindi wenyewe bado hauna basi direct kutoka stand yake kuu, wanategemea mabasi ya mtwara, newala, masasi tunduru nachingwea na songea .
Hata uwe na mishe zako za mjini huwezi kupata Basi la saa kumi na mbili asubuhi kutoka Lindi , itabidi usubirie basi la kwanza kutoka mtwara amabalo linafika Lindi kuanzia saa moja asubuhi
Abiria bado wachache sana lindi
Kuna Baraka ilikua inaanzia Lindi to Dar na kurud Lindi the same same day.
 
Back
Top Bottom