Sina mazoea ya kupanda Daladala Dar, kuna siku nimetumia usafiri huu jijini Dar, sikuwa na jinsi kusubiria gari lenye nafasi maana yote yalionekana kujaa nikaamua nifuate wenye mazoea kushikilia bomba mwendo mrefu na hatukuwa wengi kiasi cha kufanyiana mambo ya kipuuzi.
Mbele yangu alisimama dada mmoja ambaye aalionekana mtulivu na mstaarabu, hata hivyoi baadaye kilichoendelea sikuamini kama anafanya kwa akili timamu. Ingawa hatukuwa tumebanana, kilichonishangaza ni pale hata gari lisiposimama ghafla kuendelea na mazoezi ya kujipigisha kwangu makali yake kwa awamu, awali nilidhani bhati mbaya, na nilipoona mchezo unaendelea nikaamua kutafuta nafasi nyuma kwa wastaarabu, nikatoa lugha ya matani kwamba tumechanganyika humu wengine wana yao utafikiri wanakoishi ni wapweke na hivyo kumalizia yanayowasibu ya upwekeni humu garini, ndio maana ukimwi hauishi ndio sababu ya kukimbia niliposimama. Konda alicheka kisha akaniambia; 'Mkuu tuachie wenyewe hiyo ndiyo raha tuliyozoea, bahati mbaya wengine hawachagui mtu."
Nilisemalo si masikhara yamenikuta, yule dada aliposikia kauli yangu alishuka kituo kilichofuata maana aliona naendeleza story na watu walishaona aliyekuwa amesimama mbele yangu. Naona ustaarabu upo likizoni, maadili nayo ni haba, elimu ya jamii imeshakoma, tuna kazi na sasa ni ulimwengu tu kubaki kutuelimisha. Mzee mmoja wa makamo aliyeongozana na kijana wake aliponikirimia seat yake, aliniasa mengi, na kwamba kuna kila aina ya utongozaji siku hizi, matendo kama haya ndiyo yanayowafanya vijana waparamie kila anayemtamanisha kwa njia mbalimbali bila kujua wengine hawajatakata wamechafuka kwa dinga zenye uchafu wenye vijidudu hatari vinavyopenya ngozi hadi damuni.