Usafiri daladala abiria watumiapo kujiridhisha ngono bila gharama wala ridhaa

Njele

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
275
121
e.jpg
Sina mazoea ya kupanda Daladala Dar, kuna siku nimetumia usafiri huu jijini Dar, sikuwa na jinsi kusubiria gari lenye nafasi maana yote yalionekana kujaa nikaamua nifuate wenye mazoea kushikilia bomba mwendo mrefu na hatukuwa wengi kiasi cha kufanyiana mambo ya kipuuzi.

Mbele yangu alisimama dada mmoja ambaye aalionekana mtulivu na mstaarabu, hata hivyoi baadaye kilichoendelea sikuamini kama anafanya kwa akili timamu. Ingawa hatukuwa tumebanana, kilichonishangaza ni pale hata gari lisiposimama ghafla kuendelea na mazoezi ya kujipigisha kwangu makali yake kwa awamu, awali nilidhani bhati mbaya, na nilipoona mchezo unaendelea nikaamua kutafuta nafasi nyuma kwa wastaarabu, nikatoa lugha ya matani kwamba tumechanganyika humu wengine wana yao utafikiri wanakoishi ni wapweke na hivyo kumalizia yanayowasibu ya upwekeni humu garini, ndio maana ukimwi hauishi ndio sababu ya kukimbia niliposimama. Konda alicheka kisha akaniambia; 'Mkuu tuachie wenyewe hiyo ndiyo raha tuliyozoea, bahati mbaya wengine hawachagui mtu."

Nilisemalo si masikhara yamenikuta, yule dada aliposikia kauli yangu alishuka kituo kilichofuata maana aliona naendeleza story na watu walishaona aliyekuwa amesimama mbele yangu. Naona ustaarabu upo likizoni, maadili nayo ni haba, elimu ya jamii imeshakoma, tuna kazi na sasa ni ulimwengu tu kubaki kutuelimisha. Mzee mmoja wa makamo aliyeongozana na kijana wake aliponikirimia seat yake, aliniasa mengi, na kwamba kuna kila aina ya utongozaji siku hizi, matendo kama haya ndiyo yanayowafanya vijana waparamie kila anayemtamanisha kwa njia mbalimbali bila kujua wengine hawajatakata wamechafuka kwa dinga zenye uchafu wenye vijidudu hatari vinavyopenya ngozi hadi damuni.
 
yeye ww kupanda daladala siku moja tu malalamiko kibao je sie ambao kila siku asbh na jion lazima tupande tufanyaje?

Kitendo kile si cha kawaida hata ungekuwa wewe, kwa wastaarabu tunatunza heshima zetu na nilipanda gari kwa lengo la kufika niendako si mambo ya upuzi aliyokuwa ananifanyia, serious ni kitu ambacho kimenifikirisha na pengine wengine hawana nafasi ya kuyaweka hadharani kama nilivyofanya mie pengine kuna makubwa zaidi ya yaliyonipata.
 
Mbona kuna wanaume pia wenye tabia hzo aisee hata pasipokuwa na mbanano unaskia kitu kinakugusa kwa nyuma tena makusudi! Cjui hawanaga wakuwafanyia hayo au wanawazaga nini cjui! they are so stupid than ever!!
 
Kitendo kile si cha kawaida hata ungekuwa wewe, kwa wastaarabu tunatunza heshima zetu na nilipanda gari kwa lengo la kufika niendako si mambo ya upuzi aliyokuwa ananifanyia, serious ni kitu ambacho kimenifikirisha na pengine wengine hawana nafasi ya kuyaweka hadharani kama nilivyofanya mie pengine kuna makubwa zaidi ya yaliyonipata.

Candid Scope ndio huyohuyo Njele?????!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
View attachment 124222
Sina mazoea ya kupanda Daladala Dar, kuna siku nimetumia usafiri huu jijini Dar, sikuwa na jinsi kusubiria gari lenye nafasi maana yote yalionekana kujaa nikaamua nifuate wenye mazoea kushikilia bomba mwendo mrefu na hatukuwa wengi kiasi cha kufanyiana mambo ya kipuuzi.

Mbele yangu alisimama dada mmoja ambaye aalionekana mtulivu na mstaarabu, hata hivyoi baadaye kilichoendelea sikuamini kama anafanya kwa akili timamu. Ingawa hatukuwa tumebanana, kilichonishangaza ni pale hata gari lisiposimama ghafla kuendelea na mazoezi ya kujipigisha kwangu makali yake kwa awamu, awali nilidhani bhati mbaya, na nilipoona mchezo unaendelea nikaamua kutafuta nafasi nyuma kwa wastaarabu, nikatoa lugha ya matani kwamba tumechanganyika humu wengine wana yao utafikiri wanakoishi ni wapweke na hivyo kumalizia yanayowasibu ya upwekeni humu garini, ndio maana ukimwi hauishi ndio sababu ya kukimbia niliposimama. Konda alicheka kisha akaniambia; 'Mkuu tuachie wenyewe hiyo ndiyo raha tuliyozoea, bahati mbaya wengine hawachagui mtu."

Nilisemalo si masikhara yamenikuta, yule dada aliposikia kauli yangu alishuka kituo kilichofuata maana aliona naendeleza story na watu walishaona aliyekuwa amesimama mbele yangu. Naona ustaarabu upo likizoni, maadili nayo ni haba, elimu ya jamii imeshakoma, tuna kazi na sasa ni ulimwengu tu kubaki kutuelimisha. Mzee mmoja wa makamo aliyeongozana na kijana wake aliponikirimia seat yake, aliniasa mengi, na kwamba kuna kila aina ya utongozaji siku hizi, matendo kama haya ndiyo yanayowafanya vijana waparamie kila anayemtamanisha kwa njia mbalimbali bila kujua wengine hawajatakata wamechafuka kwa dinga zenye uchafu wenye vijidudu hatari vinavyopenya ngozi hadi damuni.

Weka picha mkuu
 
Candid Scope ndio huyohuyo Njele?????!!!!!!!

NImeonjeshwa na kitendo hicho, nimesoma mada fulani hapa kuna kijana pia alikuwa na mazoea hayo, ni mdau niliyeonja tukio hilo mimi najitambulisha wazi natetea watetea maadili hata kama sio mimi niliyepatwa lakini najisikia mwanajmii niliyepatwa.

Huyo yamemkuta huo Dar - Tanzania wakati mie Candid niko safarini nje ya bara la Afrika na nilishaweka bandiko hapa wiki iliyopita tuliongozana na Mama Pinda toka Da -Zanzibar - Ethiopia kisha tukaachana na kila mmoja na mwelekeo wake.
 
candidscope=@njele

Tukio limetokea Dar TAnzania ambako mlalamikaji yupo wakati mie niko nje ya nchi nilishasafiri sasa karibu wiki mbili zinakaribia kuisha, jadilini mada msikwepe madhaifu hayo ni aibu kwa jamii yetu, tafuteni wapenzi au amueni kuoa/kuolewa badala ya kuamua kujibamiza kwenye miili ya wengine bila ridhaa.
 
NImeonjeshwa na kitendo hicho, nimesoma mada fulani hapa kuna kijana pia alikuwa na mazoea hayo, ni mdau niliyeonja tukio hilo mimi najitambulisha wazi natetea watetea maadili hata kama sio mimi niliyepatwa lakini najisikia mwanajmii niliyepatwa.

Huyo yamemkuta huo Dar - Tanzania wakati mie Candid niko safarini nje ya bara la Afrika na nilishaweka bandiko hapa wiki iliyopita tuliongozana na Mama Pinda toka Da -Zanzibar - Ethiopia kisha tukaachana na kila mmoja na mwelekeo wake.

Author anaandika wasomaji wana attach meaning!!!!!
 
I did mkuu siku ileile lakini umeona muunganiko wa post na comment yako!!!????

Sio issue anyway,tuipotezee tu kaa

Niwapo online niko mwepesi na nina kinasibu cha kubaini mada za kugusa jamii haraka sana, na ndio maana naijadili kwa mapana na marefu. Leo siku ya Ukimwi duniani, tujadili hilo jambo muhimu limeua watu balaa.

Hakuna kati yetu asiyeguswa na mmojaja wapo awe kutoka familia, rafiki, classmate, mjuaji, jrani nk, wengi tumeshuhudia makaburi tu ya watu tuliowazoea, kusaidia na hata kujenga malengo ya kiuchumi pamoja. Imebaki historia tu.

Kufikia hatua hiyo ya kujirishidha kujibamiza kwa mtu asiyeridhia kitendo hicho ni dalili tosha kwamba wengi tumejirahizisha mno hadi kukosa self control kwenye public. Ni aibu wasioiaibikia wengi wetu na ndio wengi tunatafuta weak point kupoteza dhana ya mada.
 
Mwaka Jana kuna Dada alikuja mbio humu akilia kuwa kuna jamaa alikuwa anagusisha uume wake kwa huyo dada,sasa leo ni hadithi nyingine ya jamaa aliyepanda daladala siku moja na kukutana na mwenye mahaba na kila mtu.
Nasubiri kesho mwingine aje na stori ya jamaa kumfungulia zip kwenye osienya yake
 
Back
Top Bottom