Usaa wa jipu na vyeti bandia utasambaa nchi nzima

NJALI

JF-Expert Member
Jan 9, 2014
1,534
1,089
Serikali imefanya jambo jema la kuwaondoa watumishi hewa kwenye Payroll, Hongera kwa hilo. Japo sijasikia hatua stahiki kwa waliowaweka au kuwabeba. Pia waliochukua pesa hizo wamefanywa nini?

Nirudi kwenye mada, Rais akitumbua vyeti feki nchi itatikisika. Sio kwamba natisha au natania hili ni janga. Atafungua milango miwili tu atakachokikuta humo ndani, he he hee atarudi Chato kula ugali na sato mapumzikoni. Hembu aende JWTZ, TANAPA, MAGEREZA, POLISI na AFYA upande wa manesi, kada za chini yaani certificate, diploma atajionea.

Kwa kuwa Rais wangu mpendwa ulisema hutafukua makaburi hata hili la vyeti feki Sio makaburi tu Bali ni Jehanamu ya watumishi wengi wa umma ukilivalia njuga. Nusu tutaondoka hata Mimi huenda nitakuwemo.

Ukiamua kusamehe samehe wote mkuu, usibague baadhi ya idara zingine ukaziacha utaleta nanung'uniko watakao kumbwa na kokoro hili wakubali matokeo, hata walivyokula vinatosha japo nina imani vibaka, wezi, majangili, majambazi, malaya, makahaba na matapeli watajaa mtaani ukilitekekeza hili Rais wangu. Najua unahekima sana kaa na wazee kadhaa unao waamini ili wakushauri namna bora ya kutumbua jipu hili, liko pabaya linahitaji umakini mkubwa.
 
Kumbe kuna namna bora ya kushughulika na waalifu zaidi ya sheria , basi hata wezi/majambazi tuone namna ya ku deal nao. sio kuwalaza chini kama ilivyo pendekezwa.
 
Kumbe kuna namna bora ya kushughulika na waalifu zaidi ya sheria , basi hata wezi/majambazi tuone namna ya ku deal nao. sio kuwalaza chini kama ilivyo pendekezwa.
Huu ni wakati wa kujijenga upya! Kuanza upya siyo ujinga.
Kashifa yoyote inayohusu udanganyifu ni kosa la jinai. Hao walioghushi vyeti wanajua kabisa kuwa walitenda kosa, hawakufanya kwa bahati mbaya.
Ufisadi upo wa aina nyingi,siyo wa kupora Mali pekee, ni pamoja na hivyo vyeti magumashi.
Kama serikali imeamua kutumia panga ama msumeno, basi wakate kate kweli bila kujali fisadi papa au dagaa,fyekelea mbali uozo uliokuwa umetamalaki nchi hii.
Wezi na matapeli walihalalishwa kwa namna sheria zilivokuwa kuntu,kukosa meno kung'ata maharamia wa maendeleo!
Mtoa mada fikra zake finyu akidhani serikali inamtegemea mfanyakazi batili. Aelewe wafanyakazi wanaitegemea serikali na siyo serikali kutegemea wafanyakazi. Aangalie jinsi watu wanavotumbuliwa bila kujali serikali imemgharamikia kiasi gani kumsomesha. Tens kwa majigambo kabisa kuwa nchi hii inahazina ya wasomi wengi wasio na ajira!
Leo inakuja "kilaza" m1 aliyepata ajira kwa figisufigisu za baba "kantuma" kwa "kimemo" bila Sifa eti nchi itatikisika ikifukuza wafanyakazi wasio na Sifa kwa nafasi walizonazo kwa kuwa hawakuzipata kihalali,siyo kweli.
Ni kuupotosha umma kwa maslahi ya tumbo make.
 
Back
Top Bottom