Huu ni ujumbe wa pili wa US kuonya kuhusu Tukio tarajiwa la Ugaidi, achilia mbali la siku za usoni ambapo balozi wa Marekani aliitwa Wizara ya Mambo ya Ndani na kuonywa lkini wamerudia tena. Wenye akili wamenielewa.Tatizo letu ni wanasiasa hasa jiwe kukumbatia siasa za kuligawa taifa kati ya wapinzani na CCM. Tunashuhudia matendo machafu kabisa yakifanywa dhidi ya baadhi ya raia. Ni wazi kuwa hao Marekani wanatahadharisha raia wao kwa kuzingatia habari na matukio halisi yanayoyokea kwa watu mbalimbali.
Mifano ipo mingi, hasa ya matukio ya utekaji na mauaji ambayo hayajatolewa maelezo yanayoridhisha.
Kama maiti zinaweza kuokotwa kisha polisi wanadai kuna watu wasiojulikana, ni wazi kuwa nchi imekaliwa na magaidi ambayo yamewashinda polisi na majeshi mengine.