Ngao ya Sponji
JF-Expert Member
- Jul 26, 2018
- 341
- 541
Ubalozi wa Tanzania mjini Stockholm Sweden pamoja na Ubalozi wa Tanzania ulio nchini Urusi zimesema kwamba kupitia njia za kidiplomasia, serikali ya Urusi imeridhia wanafunzi wa Kitanzania walioko Chuo Kikuu Sumy State kutoka nchini Ukraine kwa kupitia mpaka wa Urusi.
Taarifa ya Ubalozi wa Tanzania mjini Stockholm na Ubalozi wa Tanzania mjini Moscow inasema zoezi la kutoa wanafunzi kutoka Sumy hadi kwenye mpaka wa Urusi linaratibiwa na serikali ya Urusi na tayari mipango ya utekelezaji imeanza.
''Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi utawapokea kwa taratibu nyingine za kurejea nyumbani'' ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa ya Ubalozi wa Tanzania mjini Stockholm na Ubalozi wa Tanzania mjini Moscow inasema zoezi la kutoa wanafunzi kutoka Sumy hadi kwenye mpaka wa Urusi linaratibiwa na serikali ya Urusi na tayari mipango ya utekelezaji imeanza.
''Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi utawapokea kwa taratibu nyingine za kurejea nyumbani'' ilisema sehemu ya taarifa hiyo.