Urusi yapiga toka kwako mpaka Syria

neo1

JF-Expert Member
Sep 1, 2013
577
838
Jeshi la Anga la Urusi limetumia makombora sita ya masafa marefu kupiga majeshi ya magaidi kwenye maeneo yenye mafuta nchini Syria.

-Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kuwa, kikosi cha kurusha makombora hayo cha Tu-22M3, kimefanikisha zoezi hilo kwa kurusha makombora toka mpakani mwa Urusi hadi maeneo yaliyolengwa na kusababisha maafa kwa magaidi wa IS(wanaoujulikana kama ISIS), huko jirani mji wa Palmyra.

Tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria, kati ya Serikali ya Rais wa nchi hiyo Bashir Assad,na waasi nchini humo, Urusi imekuwa ikipigana kuisaidia Syria dhidi ya waasi hao.

Syria na Urusi ni nchi zilizo na ushirikiano wa karibu zaidi, kuliko uhusiano ilionao Urusi na nchi nyingine Mashariki ya Kati. Kwa upande wa pili, Marekani na washirika wake, wako kinyume na Serikali ya Assad, huku wakiwaunga mkono waasi wa nchi hiyo
9c2a3f11bcd0b62d2ab18b0a915f9ec0.jpg

22bf053eda13795ee10f0a38f0a6f087.jpg
 
Source of information?, ni hatari kwa kombora kutembea hivyo kwani kuna ndege za abiria na vizingiti vya angani kama upepo, kumbunga vinaweza badili muelekeo.
 
Mkuu Neo1

Naomba nikusahihishe. Sio kwamba wametuma makombora. Walichorusha ni Long Range Bombers T-22. Zilisafiri toka Russia na zika shusha mabomu Syria.

Kama yangekuwa ni makombora yangeitwa ICBM - InterContinental Ballistic Misilles.


"Russia used six long-range bombers to target terrorist forces and oil sites in Syria, the Russian Defense Ministry reported, saying it is intensifying airstrikes near Palmyra.

The Tu-22M3 bombers flew all the way from Russian territory to deliver their deadly cargo, the report said. "
 
Jeshi la Anga la Urusi limetumia makombora sita ya masafa marefu kupiga majeshi ya magaidi kwenye maeneo yenye mafuta nchini Syria.

-Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kuwa, kikosi cha kurusha makombora hayo cha Tu-22M3, kimefanikisha zoezi hilo kwa kurusha makombora toka mpakani mwa Urusi hadi maeneo yaliyolengwa na kusababisha maafa kwa magaidi wa IS(wanaoujulikana kama ISIS), huko jirani mji wa Palmyra.

Tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria, kati ya Serikali ya Rais wa nchi hiyo Bashir Assad,na waasi nchini humo, Urusi imekuwa ikipigana kuisaidia Syria dhidi ya waasi hao.

Syria na Urusi ni nchi zilizo na ushirikiano wa karibu zaidi, kuliko uhusiano ilionao Urusi na nchi nyingine Mashariki ya Kati. Kwa upande wa pili, Marekani na washirika wake, wako kinyume na Serikali ya Assad, huku wakiwaunga mkono waasi wa nchi hiyo
9c2a3f11bcd0b62d2ab18b0a915f9ec0.jpg

22bf053eda13795ee10f0a38f0a6f087.jpg
angalia source yako vizuri..ni long range bombers zilizofly non stop mpk syria kustrike then zika turn back
 
Jeshi la Anga la Urusi limetumia makombora sita ya masafa marefu kupiga majeshi ya magaidi kwenye maeneo yenye mafuta nchini Syria.

-Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kuwa, kikosi cha kurusha makombora hayo cha Tu-22M3, kimefanikisha zoezi hilo kwa kurusha makombora toka mpakani mwa Urusi hadi maeneo yaliyolengwa na kusababisha maafa kwa magaidi wa IS(wanaoujulikana kama ISIS), huko jirani mji wa Palmyra.

Tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria, kati ya Serikali ya Rais wa nchi hiyo Bashir Assad,na waasi nchini humo, Urusi imekuwa ikipigana kuisaidia Syria dhidi ya waasi hao.

Syria na Urusi ni nchi zilizo na ushirikiano wa karibu zaidi, kuliko uhusiano ilionao Urusi na nchi nyingine Mashariki ya Kati. Kwa upande wa pili, Marekani na washirika wake, wako kinyume na Serikali ya Assad, huku wakiwaunga mkono waasi wa nchi hiyo
9c2a3f11bcd0b62d2ab18b0a915f9ec0.jpg

22bf053eda13795ee10f0a38f0a6f087.jpg
KWAKWELI UJINGA NI MZIGO, YAANI WAKAZI WA MASHARIKI YA KATI SASA WAMEGEUZWA 'PUNCHING BAG' YA MAREKANI NA URUSI!
 
Source of information?, ni hatari kwa kombora kutembea hivyo kwani kuna ndege za abiria na vizingiti vya angani kama upepo, kumbunga vinaweza badili muelekeo.

Uko sahihi...aliyeleta uzi huu huenda hakuelewa maana ya stori kuhusu tukio hili...haya ni masuala ya kijeshi na wengi hawaelewi sana..ninavyoelewa mimi hiyo TU-22M3 siyo kombora bali ni aina ya mi-dege ya masafa marefu (ambayo kwa kiingereza yanaitwa bombers) ya URUSI ambalo linaweza likaruka umbali wa maelfu ya kilomita likiwa limebeba missles au makombora na kwenda kupiga targets kwa maadui...Hicho ndicho ilichofanya RUSSIA ambapo siku mbili zilizopita ambapo midege yake hiyo kama TU-160 na TU-22M3 yaliruka kutoka kwenye viwanja vya ndege vya kijeshi vilivyoko RUSSIA yakaruka kwa kasi yakipitia maeneo mengi kama IRAK na IRAN na kwenda Syria na kuachia makombora yake kwa maadui yaani wale wanaompinga ASSAD na serikali yake...Baada ya kutupa makombora hayo yakarejea tena nchini Russia....midege ya aina hii yaani long range bombers ina uwezo wa kusafiri maelfu ya kilomita bila kujaza mafuta na wakati mwingine yanajaziwa mafuta angani huko huko....Midege hii imetengenezwa kubeba pia silaha za nyuklia...Marekani ndiyo yenye madege mengi ya aina hii yakiwemo B-52 yaliyotumika sana wakati wa vita vya Vietnam, na pia B-1 na B-2 dege ambalo ni stealth yaani halionekani kwenye radar, na mengine mengi.
 
Back
Top Bottom